Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,818
- 62,027
Tumeshuhudia yaliyotokea nchini, kilichotokea pale siyo uchaguzi ni uchafuzi. Ni kikundi cha watu wachache kikilindwa na vyombo vya ulinzi kikafanya mapinduzi dhidi ya Jamhuri. kwa kujitwalia madaraka bila ridhaa ya wananchi. Idadi ya walipiga kura ni feki, idadi ya kura zilizotangazwa ni feki, na hata mchakato mzima wa uchaguzi uligubikwa na rafu nyingi. Kwa hiyo ni sahihi kusema kuwa SERIKALI ILIYOJIPACHIKA MADARAKANI SIYO SIYO SERIKALI YA WATU, INAYOTOKANA NA WATU NA KWA AJILI YA WATU. Ni serikali feki.
Zipo athari kadha wa kadha za kuwa na serikali isiyotokana na ridhaa za wananchi ambazo ni hatari mno kwa usalama wa Taifa nitazitaja.
1. Serikali isiyotokana na wanachi haina uhalali wa kuingia mikataba kwa niaba ya wananchi
Tunafahamu, moja ya kazi za serikali ni kuingia mikataba mbalimbali na taasisi tofautitofauti duniani au nchi mbalimbali duniani.Mikataba hii inaweza kuwa ya mashirikiano, ya kiuchumi na hata ya kiulinzi. Mikataba hii huwa ni kwa niaba ya wananchi. Sasa inapotokea kikundi cha watu wachache kikapoka madaraka bila ridhaa ya wananchi kinakosa uhalali wa kuingia mikataba hiyo kwa niaba yao. Uhalali huo unakosekana kwa sababu kwanza hakijapewa dhamana ya kufanya hivyo lakini pili ni vigumu kikundi hicho kuweka mbele maslahi ya wananchi ambao kimsingi hakiwaheshimu
2. Serikali isiyotokana na ridhaa ya wananchi haina uwezo wa kupigana vita na adui wa nje ikashinda
Kama wananchi wameikataa serikali husika, hawajampa ridhaa rais aliyeko madarakani, basi nchi hiyo ikivamiwa tegemea nchi hiyo kupata shida mno katika hiyo vita. Asijidanganye mtu kuwa eti lipo jeshi litaenda kupigana, Iko hivi Engine ya Ulinzi wa Taifa lolote ni wananchi, Hata sisi nchini mwetu, wakati wa vita vya Kagera, Majority ya askari waliokwenda msitari wa mbele ni wananchi wa kawaida waliopewa mafunzo maalumu ya muda mfupi. Inakadiriwa kulikuwa na wapiganaji rasmi wa Jeshi 15000, huku raia walipoewa mafunzo ya muda mfupi wakikadiriwa kuwa ni 25000 ambao jumla waliunda jeshi strong la watu 40000. Amiri Jeshi mkuu asiyetokana na ridhaa ya wananchi hawezi kuliongoza Taifa kikamilifu kukabiliana na adui wa nje, maana wananchi hawana radhi naye.
3. Serikali isiyotokana na ridhaa za watu huongoza nchi kwa hofu na hivyo kujikuta inafanya uharibifu mkubwa wa misingi ya Taifa
Ili serikali hiyo iweze kusurvive lazima ivuruge mahakama ili wale watu inaowaonea wasichomoke kupitia huko, huvuruga bunge ili hoja yoyote ya kuitikisa isipite huko, huvunja katiba bila hofu maana uwepo wake wenyewe madarakani kimsingi ni kinyume cha katiba, itateka watu, itapoteza watu. Kwa hiyo itajikuta inafnya mambo mengi ya ajabuajabu ya kuharibu misingi ya Taifa matokeo yake Taifa litakuwa si taifa la haki, na hii itazidisha chuki na hasira za umma kitu kiachoweza kupelekea vurugu na umwagaji damu wa kutisha. Kiufupi Serikali isiyotokana na wananchi ni mbegu kuu ya vurugu na uvunjifu wa amani.
4. Serikali isiyotokana na ridhaa za wananchi ni serikali dhaifu, ni rahisi kufanya chochote hata kuuza rasilimali za nchi ili iweze kusurvive
Serikali isiyo na ridhaa ya wananchi ni serikali dhaifu, ni very vulnerable ni rahisi sana kuiblackmail ili iweze kusurvive. Ili ijaribu kutafuta legitimacy, itajaribu kufanya vitu ambavyo inaamini vitawatuliza wananchi, itajaribu kutafuta fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali lakini kwa kuwa wakubwa wa dunia wanajua kuwa serikali hiyo haikubaliki watawapa terms ngumu ambazo wakizitekeleza watapatiwa fedha. Na terms zenyewe zinaweza ni kuuza rasilimali kwa bei chee, au hata kuweka rehani ardhi, maji au hata anga ya nchi ilimradi tu kuwaridhisha wakubwa wa dunia waipatie fedha au wasiwachukulie hatua kutokana na uhalifu wao.
5. Serikali isiyotokana na ridhaa ya wananchi haina moral authority ya kusimamia nidhamu
Wewe kama umeiba kura ili uingie madarakani una uhalali gani kusimamia nidhamu serikalini?. Unawezaje kuwashughulika wezi wa fedha za umma wakati na wewe mwenyewe umeiba dhamana ya uongozi ambao wananchi hawakukupatia kwa ridhaa zao?. Utawashughulikiaje majangili wakati wale askari utakaowatuma wafanye kazi hiyo wanajua kuwa wewe uliiba kura kuwa hapo na upo hapo madarakani kwa ridhaa ya mitutu yao?. Utalaani vipi walimu wanaovujisha mitihani wakati walimu hao wanajua kuwa wewe mwenyewe upo hapo kwa sababu walimu hao walikusaidia kutiki pale wananchi walipogoma kujitokeza kwa wingi kupiga kura?.
6, Serikali isiyo na ridhaa ya watu, basi watu hao huwa hawaitumikii kwa mioyo yao yote na akili zao zote na nguvu zao zote
Mara nyingi kukiwa na serikali isiyotokana na watu, wananchi hujiweka katika survival mode, wale watumishi wa serikali hufanya mambo kwa kuangalia survival yao zaidi, hufanya "vichache" huwa hawafanyi "vingi". Wananchi huamua kuwa watazamaji, shuguli maofisini huenda taratibu, rushwa hutamalaki, "unanijua mimi nani" huinua kichwa chake. Kiufupi ule uharamu wa juu husambaa mpaka chini.
7. Seriklai isiyo na ridhaa ya wananchi inakaribisha migongano endelevu na wananchi
Watu watairesist kijamii, kisiasa na kiuchumi. Migomo ya wafanyakazi, Wananchi wanaweza kufanya mbinu nyingi kukwepa kulipa kodi kwa dhana ya HUWEZI KULIPA KODI BILA UWAKILISHI, watu wanaweza kususia biashara kadha wa kadha ili kuinyima serikali mapato. Kiufupi serikali isiyo na ridhaa ya umma ni hatari mno kwa ustawi wa Taifa.
MWISHO
Hakuna future ya maana nchi inaweza kupata kama serikali iliyoko madarakani haina radhi za wananchi. hata huko katika nchi za kifalme, ambazo ni tajiri, japo hakuna kupiga kura lakini mara nyingi unakuta zile falme zina ridhaa za watu kwa asilimia kubwa. Ridhaa ikikosekana falme hizo huanza kuyumba mpaka kuanguka.
Ni hatari mno kuwa na uongozi usiokubaliwa na wananchi, hii ni kweli kuchumi, na hata kiulinzi na usalama, maana adui anaweza kutumia mianya hiyo ya "dissatisfaction" kufanya ujasusi dhidi ya nchi husika
Zipo athari kadha wa kadha za kuwa na serikali isiyotokana na ridhaa za wananchi ambazo ni hatari mno kwa usalama wa Taifa nitazitaja.
1. Serikali isiyotokana na wanachi haina uhalali wa kuingia mikataba kwa niaba ya wananchi
Tunafahamu, moja ya kazi za serikali ni kuingia mikataba mbalimbali na taasisi tofautitofauti duniani au nchi mbalimbali duniani.Mikataba hii inaweza kuwa ya mashirikiano, ya kiuchumi na hata ya kiulinzi. Mikataba hii huwa ni kwa niaba ya wananchi. Sasa inapotokea kikundi cha watu wachache kikapoka madaraka bila ridhaa ya wananchi kinakosa uhalali wa kuingia mikataba hiyo kwa niaba yao. Uhalali huo unakosekana kwa sababu kwanza hakijapewa dhamana ya kufanya hivyo lakini pili ni vigumu kikundi hicho kuweka mbele maslahi ya wananchi ambao kimsingi hakiwaheshimu
2. Serikali isiyotokana na ridhaa ya wananchi haina uwezo wa kupigana vita na adui wa nje ikashinda
Kama wananchi wameikataa serikali husika, hawajampa ridhaa rais aliyeko madarakani, basi nchi hiyo ikivamiwa tegemea nchi hiyo kupata shida mno katika hiyo vita. Asijidanganye mtu kuwa eti lipo jeshi litaenda kupigana, Iko hivi Engine ya Ulinzi wa Taifa lolote ni wananchi, Hata sisi nchini mwetu, wakati wa vita vya Kagera, Majority ya askari waliokwenda msitari wa mbele ni wananchi wa kawaida waliopewa mafunzo maalumu ya muda mfupi. Inakadiriwa kulikuwa na wapiganaji rasmi wa Jeshi 15000, huku raia walipoewa mafunzo ya muda mfupi wakikadiriwa kuwa ni 25000 ambao jumla waliunda jeshi strong la watu 40000. Amiri Jeshi mkuu asiyetokana na ridhaa ya wananchi hawezi kuliongoza Taifa kikamilifu kukabiliana na adui wa nje, maana wananchi hawana radhi naye.
3. Serikali isiyotokana na ridhaa za watu huongoza nchi kwa hofu na hivyo kujikuta inafanya uharibifu mkubwa wa misingi ya Taifa
Ili serikali hiyo iweze kusurvive lazima ivuruge mahakama ili wale watu inaowaonea wasichomoke kupitia huko, huvuruga bunge ili hoja yoyote ya kuitikisa isipite huko, huvunja katiba bila hofu maana uwepo wake wenyewe madarakani kimsingi ni kinyume cha katiba, itateka watu, itapoteza watu. Kwa hiyo itajikuta inafnya mambo mengi ya ajabuajabu ya kuharibu misingi ya Taifa matokeo yake Taifa litakuwa si taifa la haki, na hii itazidisha chuki na hasira za umma kitu kiachoweza kupelekea vurugu na umwagaji damu wa kutisha. Kiufupi Serikali isiyotokana na wananchi ni mbegu kuu ya vurugu na uvunjifu wa amani.
4. Serikali isiyotokana na ridhaa za wananchi ni serikali dhaifu, ni rahisi kufanya chochote hata kuuza rasilimali za nchi ili iweze kusurvive
Serikali isiyo na ridhaa ya wananchi ni serikali dhaifu, ni very vulnerable ni rahisi sana kuiblackmail ili iweze kusurvive. Ili ijaribu kutafuta legitimacy, itajaribu kufanya vitu ambavyo inaamini vitawatuliza wananchi, itajaribu kutafuta fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali lakini kwa kuwa wakubwa wa dunia wanajua kuwa serikali hiyo haikubaliki watawapa terms ngumu ambazo wakizitekeleza watapatiwa fedha. Na terms zenyewe zinaweza ni kuuza rasilimali kwa bei chee, au hata kuweka rehani ardhi, maji au hata anga ya nchi ilimradi tu kuwaridhisha wakubwa wa dunia waipatie fedha au wasiwachukulie hatua kutokana na uhalifu wao.
5. Serikali isiyotokana na ridhaa ya wananchi haina moral authority ya kusimamia nidhamu
Wewe kama umeiba kura ili uingie madarakani una uhalali gani kusimamia nidhamu serikalini?. Unawezaje kuwashughulika wezi wa fedha za umma wakati na wewe mwenyewe umeiba dhamana ya uongozi ambao wananchi hawakukupatia kwa ridhaa zao?. Utawashughulikiaje majangili wakati wale askari utakaowatuma wafanye kazi hiyo wanajua kuwa wewe uliiba kura kuwa hapo na upo hapo madarakani kwa ridhaa ya mitutu yao?. Utalaani vipi walimu wanaovujisha mitihani wakati walimu hao wanajua kuwa wewe mwenyewe upo hapo kwa sababu walimu hao walikusaidia kutiki pale wananchi walipogoma kujitokeza kwa wingi kupiga kura?.
6, Serikali isiyo na ridhaa ya watu, basi watu hao huwa hawaitumikii kwa mioyo yao yote na akili zao zote na nguvu zao zote
Mara nyingi kukiwa na serikali isiyotokana na watu, wananchi hujiweka katika survival mode, wale watumishi wa serikali hufanya mambo kwa kuangalia survival yao zaidi, hufanya "vichache" huwa hawafanyi "vingi". Wananchi huamua kuwa watazamaji, shuguli maofisini huenda taratibu, rushwa hutamalaki, "unanijua mimi nani" huinua kichwa chake. Kiufupi ule uharamu wa juu husambaa mpaka chini.
7. Seriklai isiyo na ridhaa ya wananchi inakaribisha migongano endelevu na wananchi
Watu watairesist kijamii, kisiasa na kiuchumi. Migomo ya wafanyakazi, Wananchi wanaweza kufanya mbinu nyingi kukwepa kulipa kodi kwa dhana ya HUWEZI KULIPA KODI BILA UWAKILISHI, watu wanaweza kususia biashara kadha wa kadha ili kuinyima serikali mapato. Kiufupi serikali isiyo na ridhaa ya umma ni hatari mno kwa ustawi wa Taifa.
MWISHO
Hakuna future ya maana nchi inaweza kupata kama serikali iliyoko madarakani haina radhi za wananchi. hata huko katika nchi za kifalme, ambazo ni tajiri, japo hakuna kupiga kura lakini mara nyingi unakuta zile falme zina ridhaa za watu kwa asilimia kubwa. Ridhaa ikikosekana falme hizo huanza kuyumba mpaka kuanguka.
Ni hatari mno kuwa na uongozi usiokubaliwa na wananchi, hii ni kweli kuchumi, na hata kiulinzi na usalama, maana adui anaweza kutumia mianya hiyo ya "dissatisfaction" kufanya ujasusi dhidi ya nchi husika