Serikali isisubiri vifo zaidi kufanyia upanuzi wa barabara ya Kilwa kuanzia Mbagala

nzahaksm

Member
Dec 2, 2018
14
29
Hii njia sasa imeshakuwa kero kwa wananchi. Haipiti siku bila kutokea ajali eneo la mzinga darajani mpaka kongowe. Wiki iliyopita lori lilifeli breki na kusomba wapita njia na kuwaingiza mtoni. Zaidi ya watu 5 walifariki hapo hapo. Wiki iliyopita nyuma yake lori liliangukia bajaji na wakapotea abiria watatu na dereva papo hapo.

Leo lori tena limefeli na kuingia kwenye mtaro na kufunga njia kabisa zaidi ya masaa magari yapo kwenye foleni

Changamoto ni njia nyembamba na kuna mlima. Lakini pia kwa chini kuna daraja ambalo linafanya hata service road isiweze kufanya kazi mpaka labda daraja litanuliwe.

Niiombe Serikali kuitupia jicho hii njia na kuipanua walau kuanzia mbagala mpaka kisemvule kwa hatua ya mwanzo . Wakianza na utanuzi wa daraja liruhusu service road ziweze kuunganisga kupita darajani itasaidia sana .

Wananchi wameshachoshwa na kero hii kuna sku wataonesha hisia zao kwa pamoja na itakuwa too late kwa kuwa madhara mengi yameshatokea. Serikali inahitaji vifo vingapi ili kulifanyia kazi hili??
 
Hii njia sijui kwann haionekani wakati ni karibu kabisa na mjini ! Mpaka najiuliza huku hakuna hata mbunge wa kuliona hili??? Njia inaongoza kwa foleni na ni nyembamba sana. AJALI ZA MARA KWA MARA PALE KWENYE KILIMA ALAFU SASA NJIA MBADALA UPITE CHEKECHEA KULE UJE KUTOKEA KONGOE NI NOMA SANA.

LAKINI CHA KUSHANGAZA WANAJENGA BARABARA ZA MITAA ZA LAMI MWANANYAMALA NA GOMBA HUKO ILA HUKU WAMEKUSAHAU KWAKUWA WANAKAA MAKABILA AMBAYO HAYANA MVUTO KWENYE NCHI.
 
Hii njia sasa imeshakuwa kero kwa wananchi. Haipiti siku bila kutokea ajali eneo la mzinga darajani mpaka kongowe. Wiki iliyopita lori lilifeli breki na kusomba wapita njia na kuwaingiza mtoni. Zaidi ya watu 5 walifariki hapo hapo. Wiki iliyopita nyuma yake lori liliangukia bajaji na wakapotea abiria watatu na dereva papo hapo.

Leo lori tena limefeli na kuingia kwenye mtaro na kufunga njia kabisa zaidi ya masaa magari yapo kwenye foleni

Changamoto ni njia nyembamba na kuna mlima. Lakini pia kwa chini kuna daraja ambalo linafanya hata service road isiweze kufanya kazi mpaka labda daraja litanuliwe.

Niiombe Serikali kuitupia jicho hii njia na kuipanua walau kuanzia mbagala mpaka kisemvule kwa hatua ya mwanzo . Wakianza na utanuzi wa daraja liruhusu service road ziweze kuunganisga kupita darajani itasaidia sana .

Wananchi wameshachoshwa na kero hii kuna sku wataonesha hisia zao kwa pamoja na itakuwa too late kwa kuwa madhara mengi yameshatokea. Serikali inahitaji vifo vingapi ili kulifanyia kazi hili??
hakuna sababu ya kuchoka wala kuitishia serikali kwa hivi au vile 🐒

umetoa maoni, mtazamo na ushauri mzuri sana.

itoshe tu kusema umeskikia, umeeleweka vizuri. Serikali za mitaa, halmashauri, tanroads mkoa, tarura na tanroads Taifa na idara husika chukueni Jambo hili kwa uzito unaostahili, ni muhimu sana 🐒
 
Hii njia sijui kwann haionekani wakati ni karibu kabisa na mjini ! Mpaka najiuliza huku hakuna hata mbunge wa kuliona hili??? Njia inaongoza kwa foleni na ni nyembamba sana. AJALI ZA MARA KWA MARA PALE KWENYE KILIMA ALAFU SASA NJIA MBADALA UPITE CHEKECHEA KULE UJE KUTOKEA KONGOE NI NOMA SANA.

LAKINI CHA KUSHANGAZA WANAJENGA BARABARA ZA MITAA ZA LAMI MWANANYAMALA NA GOMBA HUKO ILA HUKU WAMEKUSAHAU KWAKUWA WANAKAA MAKABILA AMBAYO HAYANA MVUTO KWENYE NCHI.
Hilo eneo kuna TARURA/TANROAD/DC/DAS/DED/MBUNGE/Diwani wote wana vitambi na hakuna anayejali maisha ya wananchi
 
Barabara ya Kilwa ni Moja ya barabara zenye magari mengi sana kwa Dar es salaam.

Wakati wanaanza kujenga system ya mwendokasi,ilitakiwa angalau itanuliwe iwe lane 3 Kila upande. Vinginevyo huu uliofanyika ni utoto.

Leo gari Moja likikwama tu foleni inaamzia kongowe hadi mtongani. Kuna siku magari ya mvagala yalitoka city center yakawa yanapitia Buza kwa mparange,kisa Kuna lori lilianguka pale Mbagala Mission. Masaa manne halijatolewa.
 
Barabara ya Kilwa ni Moja ya barabara zenye magari mengi sana kwa Dar es salaam.

Wakati wanaanza kujenga system ya mwendokasi,ilitakiwa angalau itanuliwe iwe lane 3 Kila upande. Vinginevyo huu uliofanyika ni utoto.

Leo gari Moja likikwama tu foleni inaamzia kongowe hadi mtongani. Kuna siku magari ya mvagala yalitoka city center yakawa yanapitia Buza kwa mparange,kisa Kuna lori lilianguka pale Mbagala Mission. Masaa manne halijatolewa.
Aibu kubwa sn
 
Hii njia sijui kwann haionekani wakati ni karibu kabisa na mjini ! Mpaka najiuliza huku hakuna hata mbunge wa kuliona hili??? Njia inaongoza kwa foleni na ni nyembamba sana. AJALI ZA MARA KWA MARA PALE KWENYE KILIMA ALAFU SASA NJIA MBADALA UPITE CHEKECHEA KULE UJE KUTOKEA KONGOE NI NOMA SANA.

LAKINI CHA KUSHANGAZA WANAJENGA BARABARA ZA MITAA ZA LAMI MWANANYAMALA NA GOMBA HUKO ILA HUKU WAMEKUSAHAU KWAKUWA WANAKAA MAKABILA AMBAYO HAYANA MVUTO KWENYE NCHI.
Makabila gani Mkuu? Walisha sema makabila yamebakia na kazi moja tu, nayo ni KUTAMBIKIA TU. Kwa mantiki hiyo, hakuna suala la upendeleo katika maendeleo ya NCHI yetu yanayo tekelezwa ki-kabila
 
Kile ki daraja, eti ndiyo kinapitisha magari yote ya kuja kusini kutoka Dar 🤔🤔🤔.

Tena ukiongeza na magari ya abiria na wakazi wa hapo hapo aiseee.....
 
Back
Top Bottom