Serikali ipoge marufuku ulazima wa mzazi kununua sare shuleni

From Sir With Love

JF-Expert Member
Sep 13, 2010
2,076
3,797
Heri ya mwaka mpya.

Kama mzazi, nawiwa kukinzana na ulazima wa mzazi kununua uniform za shule kwenye shule ambayo mtoto amepata nafasi tena kwa bei kubwa.

Kwa wale wazazi au walezi ambao hawasomeshi watoto shule za private, mchezo upo hivi!

Mwanao ukimpeleka shule ya private na akatahiniwa na kufaulu, shule husika huwa inamlazimu mzazi anunue uniform na vikorombwezo vyake pale pale. Kwa udadisi wangu, bei za uniform kwenye shule husika huwa ni kubwa kuliko maduka ya kawaida.

Kibaya zaidi, mzazi analazimika anunue uniform kwenye shule husika kwa sababu ya MUHURI wa shule. Shule nyingi za private zina mihuri kwenye masweta, koti, kaptula, au shati za shule husika.

Kununua uniform shuleni, kunafanya wafanyabiashara wenye maduka ya nguo kutopata biashara kwa sababu ya kutokua na mihuri husika, hivyo nguo zao kukosa soko japo zinafanana na shule husika.

Ninaomba serikali yetu sikivu, ipige marufuku shule kuwauzia uniform wazazi kwa ulazima, lakini pia iweke bei elekezi za uniform ili wazazi wapate value for money, kama walivyoweka bei elekezi kwenye vitabu vya shule.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama motto anasoma boarding MUHURI wa Nini kwenye uniform yake?!
Hii mihuri ililetwa zamani , baadaye ikaondolewa ,baadaye tena ikarudishwa.

Wangefanya kuwe na ulazima wa muhuri tu lakini siyo uniform.

Shule ya msingi niliyosoma mimi, tulikuwa tunanunua kila kipande cha muhuru tu unampelekea fundi charahani anakubandikia juu ya mfuko wa shati, hakukuwa na ulazima wa kununua uniform shuleni, uniform tulinunua popote isipokuwa kugongewa muhuri au kitambaa chenye muhuri ndicho tulilipia.
 
Ni kweli shule nyingi hasa za private wako hivyo, ila mi nashukru anaposoma mwanangu hawana mambo ya mihuri sana isipokuwa kwenye nguo za michezo tu.
Sweta, school uniform na soksi nanunua mwenyewe kwa bei ya kawaida madukani.
Mf soksi shuleni ni elfu 7 ila madukani ni elfu 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau, mkuu hapa amount maana pia ni usumbufu kwetu wazazi. Unakuta shule inawanafunzi wengi...na hivyo uniform zinakuja kwa awamu .. sasa ikitokea mwanao kawa Wa mwisho ndio balaaa...anakuja pata uniform March au April wakati kama wangeruhusu..dec tungewashonea.
Serikali inabidi kusimamia kutoka muongozo kwenye haya mashule...hata kama hii ni miradi Yao ya kuongeza kipato basi waangalie na kero kama hizi.
 
Katiba na sheria ni moja. Kama usemi wako unasimama, basi hakuna haja ya kusimamia bei za mafuta. Si Private? EWURAya nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Shule za private Zina utaratibu wa kuandaa watu wa Aina flani kwa kuzingatia maadili ya Aina ya watu wanaotaka kuandaa Sasa wewe unataka wakuandalie mwanao vizuri ila hutaki gharama ?


Mkuu are you serious ?


Vizuri vina gharama


Hoteli nazo ni private vipi serikali inapanga Aina ya huduma utakazo pata kulingana na Bei uliyotoa ?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ijihusishe na shule zake za bure. Haya mambo ya kila kitu serikali iingilie, sijui ipige marufuku, inatengeneza watawala wanaojiona wao wako sahihi na wanajua kila kitu, matokeo yake ni kuvuruga kila kitu hasa vinavyohitaji weledi wa taaluma na utii wa sheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom