Serikali ipige marufuku shule Binafsi kulazimisha Watoto wa darasa la Nne na la Saba kukaa Bweni

ministrant

JF-Expert Member
Jan 17, 2014
554
1,134
Wakuu kumekuwa na hii changamoto iliyojitokeza hivi karibuni kwa Shule nyingi za Msingi zinazomilikiwa na Watu au Taasisi binafsi kulazimisha wazazi wawalipie watoto wao wakae Boarding kwa kisingizio cha kupata muda wa kutosha wa kujiandaa na Mitihani ya Taifa ya Darasa la Nne na la Saba.

Binafsi sioni tija ya jambo hili kwakuwa kulala shule hakumfanyi mwanafunzi kuwa bora zaidi ni kuwaongezea tu wazazi gharama za maisha zisizo na mantiki yoyote ile.

Pia kulingana na mmomonyoko wa maadili uliokithiri hasa vitendo vya usagaji na ushoga vijana wa rika hili wako hatarini zaidi hivyo wanahitaji ukaribu zaidi na wazazi ili kuratibu malezi na ulinzi wa watoto hawa ukizingatia. Hii ni kwasababu vijana wa rika hili hawana ujasiri wa kujitetea ikitokea aidha walimu, walinzi au wahudumu wengine wa shule za bweni wakiwashawishi kufanya vitendo hivyo na hata kuna uwezekano wa kufanyiana wao kwa wao.

Nitoe wito kwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu iingilie kati jambo hili na kizipiga marufuku shule zinazolazimisha jambo hili na badala yake liwe hiyari kwa mzazi kuamua kama anataka mwanae akae Bweni ama la.
Shule hizi zinapatikana zaidi katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
 
Hili suala wizara inayohusika na ulinzi wa watoto isipolikemea nina uhakika tutakuja kulia huko mbeleni.
 
Wakuu kumekuwa na hii changamoto iliyojitokeza hivi karibuni kwa Shule nyingi za Msingi zinazomilikiwa na Watu au Taasisi binafsi kulazimisha wazazi wawalipie watoto wao wakae Boarding kwa kisingizio cha kupata muda wa kutosha wa kujiandaa na Mitihani ya Taifa ya Darasa la Nne na la Saba.

Binafsi sioni tija ya jambo hili kwakuwa kulala shule hakumfanyi mwanafunzi kuwa bora zaidi ni kuwaongezea tu wazazi gharama za maisha zisizo na mantiki yoyote ile.

Pia kulingana na mmomonyoko wa maadili uliokithiri hasa vitendo vya usagaji na ushoga vijana wa rika hili wako hatarini zaidi hivyo wanahitaji ukaribu zaidi na wazazi ili kuratibu malezi na ulinzi wa watoto hawa ukizingatia. Hii ni kwasababu vijana wa rika hili hawana ujasiri wa kujitetea ikitokea aidha walimu, walinzi au wahudumu wengine wa shule za bweni wakiwashawishi kufanya vitendo hivyo na hata kuna uwezekano wa kufanyiana wao kwa wao.

Nitoe wito kwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu iingilie kati jambo hili na kizipiga marufuku shule zinazolazimisha jambo hili na badala yake liwe hiyari kwa mzazi kuamua kama anataka mwanae akae Bweni ama la.
Shule hizi zinapatikana zaidi katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Serikali ya Tanzania huwa haichukui hatua hadi maafa au janga litokee ndo inakurupuka na shuka mkononi
 
Hakuna shule inayolazimisha,tena mi ka sina mda ni bora mtoto akae bweni kuliko uraiani,vitendo vya ushoga ulaiani,bangi,wizi (panya road)uchawi,vishawishi vibovu maana kuna mitoto haijapelekwa shule mitukutu, boarding ni bora,mayaya wenyeww wanaua watoto
 
  • Bweni kwa ujumla haifai hasa kwa shule ya msingi.
  • Serikali ya Kenya wameshtuka, wamefuta huo upumbavu
 
  • Thanks
Reactions: Cyn
Back
Top Bottom