Serikali ipige marufuku huu Ujinga, kudhalilisha watu wetu!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,787
Hawa watu jamii ya Wahdazabe na Wasandawe, Serikali iingilie na ipige marufuku kuishi kama wanavyoishi na badala yake wapelekewe Shule, wafundishwe Kiswahili na kuchanganywa na sisi, tuache kuwatumia ndugu zetu kama experiments, najua hapa mtakuja kutoa povu sijui Utamaduni blah blah wakati hapo ulipo umekaa kwenye computer au smart phone, umevaa Jeans na sneakers ukifika nyumbani unakula unawasha jiko la umeme au gesi kupika chakula na kula kijiko, lkn unataka wenzako ndiyo waendeleza huo unaouita Utamaduni, kwa faidia ya nani?

Hawa watu pmj na Wamasai bila ya kujua wanatumiwa na Wazungu kwa ajili ya experiments, (human experiments), Wazungu wakitaka kulinganisha tabia za Binadamu wa kale/ujima na wa sasa huenda kwa hawa watu, hivyo ndiyo maana ukitaka kuwapa nguo au kuwafundiosha Kiswahili na kuwachanganya na sisi Mzungu anakuja juu, kama sisi wote tulikuwa hivyo lkn leo hii hatuko hivyo kwa nini tunafikiri wenzetu ndiyo wanaopaswa kudumisha Utamaduni wao?

unnamed%2B%252856%2529.jpg


unnamed%2B%252857%2529.jpg


(Picha kwa hisani ya blogu ya Michuzi!)
 
Mwenyekiti hataki kupangiwa wewe mwanachama unakuja kumshauri aanze kupangia wenzake.

Unafiki nao shida pia.
 
How re they used as experiment?fafanua. Siyo ukiwa na bundle tu unakuja kujaza server. Mpka sasa umechukua wahdzabe au wamasai wangap?ukishiba uji na maharage unakuja kutapikia humu. Wale hawatak maisha ya kujichanganya.. Wameshafanyiwa utaratibu huo several times wanarud porin. Hawatak mashida yenu duniani huku. Uwe unauliza kwa wataalam
 
How re they used as experiment?fafanua. Siyo ukiwa na bundle tu unakuja kujaza server. Mpka sasa umechukua wahdzabe au wamasai wangap?ukishiba uji na maharage unakuja kutapikia humu. Wale hawatak maisha ya kujichanganya.. Wameshafanyiwa utaratibu huo several times wanarud porin. Hawatak mashida yenu duniani huku. Uwe unauliza kwa wataalam


Unajua wewe Wazazi wako walitolewaje porini mpaka leo hii uko hapo ulipo?
 
tatizo una generalize. wazaz wako wewe walikuwa porini huko ambako pengine ndo umezaliwa. hawakupenda maisha ya kule wakachukuliwa kuletwa mjini. lakini kwa sasa wenye ufaham wanatoka mjini wanaenda kuishi maisha ya utulivu sehemu kama hizo zenye uutulivu.
umesema wanafanyiwa experiment. elezea experiment gani? maana usije ukawa tu umelisikia hilo neno nawe unaona upate sehemu ya kuzungumzia. wanafanyiwa experiment gani? haya mambo kama huyajui uliza.
Unajua wewe Wazazi wako walitolewaje porini mpaka leo hii uko hapo ulipo?
 
Ungekuwa mwerevu lazima ungejua kuwa tangu enzi ya ukoloni na hata baada ya uhuru kumekuwa na majaribio mengi ya kuwabadilisha hawa watu na yote zimeshindikana. Unaanzaje kumlazimisha binadamu kubadilisha njia yake ya maisha ambayo anaamini ndio bora kuliko zote? Its always survival for the fittest huku duniani, sidhani kama nusu karne itaisha kabla hawajachanganyika na watu wengine. Let nature take its course.
 
Its their culture.... just like wamasai, wasukuma na makabila mengine yalivyo na tamaduni zao.

Alaf hii ni life style yao.. kama unaishi arusha na unatembea sana mikoa ya kusini.. usingeleta hii mada. Wamasai wa sasa wameelimika ..wanapiga english safi.. lakin life style wanayoishi ndio hiyo waliyochagua. Ku preserve mila na desturi za kwao.

Wewe unasema ni experiment...?
How.. wakat wazungu wanakuja africa waliwakuta waafrica wakiishi porin.. na maisha yalikuwa safi tu...
 
Hii naunga mkono. Huwezi kuwa na Taifa baadhi ya watu wanaishi maisha ya kijinga na kijima kiasi hiki.
 
Serikali ipo busy kula rambi rambi. kuna vijana wengi tu wameaachwa kuajiriwa baada ya dikiteta uchwara kuingia. Sijui . Huyo bwana na roho mbaya yake sijui km atawasaidia.
Msukule wa chama cha majambazi chukua wawili ukaishi nao
 
Unajua wewe Wazazi wako walitolewaje porini mpaka leo hii uko hapo ulipo?
Wewe naona akili zako zilibaki porini. Ni kitu kama hujatahiriwa hivi.

Wale Wahadzabe kuli waliko wanaishi raha mustarehe, hawakwaziki na Bashite wala hawajui Baikoko. Hebu wakome!
 
sio lazima waache utamaduni wao wanaweza ku-adapt baahi ya mambo ya muhimu kutuka kwetu na bao wakaendelea na utamaduni wao
 
haelewi huyu anajisemea tu na ndo maana sisi wenye akili tukimwuliza anashindwa kuelewa. wao wanaishi maisha ambayo wameyachagua . mleta mada analazimisha eti waletwe mjini. kisa yeye aliletwa mjini akiwa na wazazi wake. wahadzabe hawatai maisha haya ya umjini. wanagoma wakipelekwa shule, hawataki wapewe nyama ya ng'ombe ya butchani. wanataka wakawinde wenyewe. jamaa anaongea vitu havifaham kabisa.

Ungekuwa mwerevu lazima ungejua kuwa tangu enzi ya ukoloni na hata baada ya uhuru kumekuwa na majaribio mengi ya kuwabadilisha hawa watu na yote zimeshindikana. Unaanzaje kumlazimisha binadamu kubadilisha njia yake ya maisha ambayo anaamini ndio bora kuliko zote? Its always survival for the fittest huku duniani, sidhani kama nusu karne itaisha kabla hawajachanganyika na watu wengine. Let nature take its course.
 
Aiseee... jamiiforums watu huwa wanaandika vitu vingine hawaulizi. mimi nimefanya research ya prof (anthropology) mmoja toka marekan nimekaa nao hao wahadzabe huko mongoamono,yaeda chini, mangola, na maeneno mengine mengine. ni watu ambao ndo maisha wanayoyataka wao waishi. si kwamba wamelazimishwa . wana furaha na maisha yao. hawajali na haiwahusu rais wa nchi hii ni nani, mbunge ni nani, mkuu wa wilaya au mkoa wao hawahusu. wao wana maisha yao ya furaha kabisa wakiwinda, kuchimba mizizi na kuchuma matunda. wagemaji wazuri sana wa asali na kuwinda kila aina ya wanyama na ndege.

serikali ilijaribu mara nyingi kuwaleta katika dunia hii mleta mada atakayo kwa kuwapeleka shule ambako walitoroka, na kuwatengenezea makazi na kuwapa nyama walitoroka pia. hawataki kuchangamana na makazi ya watu wengine. na kila wanaposogelewa na wamang'ati wao huhama kuhamia sehemu za mbali.

katiba ya nchi inasema kila mtu ana uhuru wa kuishi popote atakapo ili mradi havunji sheria. wewe unasema waletwe mjini kwa lazima huoni kuwa unaonesha kuwa na uelewa mdogo wa haya mambo? watu wale wanaishi kwa maisha yao raha mustarehe....kwa nini unadhani nao wanapaswa waletwe mjini kama wewe? wewe hukupenda maisha ya porini kwenu. hawa wanayapenda na hawana tatizo nayo.

waache watu waishi maisha yako. siku ukilazimishwa nawe kurudishwa kijijini sababu huna kazi au sababu ya makazi utalalamika sana.
 
Back
Top Bottom