Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
Siku chache zilizopita, mdau wa JF aligusia juu ya Pombe hii kuwa hatarishi kwa wananchi. Serikali imechukua hatua mapema ili kuwalinda wananchi.
Hoja ya mdau inapatikana hapa Unywaji wa pombe aina ya Banana inaathiri nguvu kubwa sana ya vijana
==========
Serikali imesitisha uzalishaji wa pombe aina ya Banana inayozalishwa na kiwanda cha Tanbasi Investment kilichoko Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro baada ya kubainika kushindwa kukidhi viwango vya ubora.
Jana Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, alitangaza kufungwa kwa kiwanda hicho kutokana na ripoti ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Kagaigai alifikia uamuzi huo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wataalamu wa TBS.
“Ripoti ya TBS inaonyesha kuwa sampuli za pombe hiyo zilizopelekwa huko hazifai kwa matumizi ya binadamu kutokana na kuongezwa kiwango kikubwa cha kemikali ya Asetic Acid.
“Nilivyokuja Kilimanjaro, niliambiwa na viongozi wa dini kwamba Rombo kuna viwanda vingi vya kutengeneza pombe, ambazo hazina ubora na zinaleta madhara kwa binadamu.
“Nikaelezwa zipo zilizosababisha baadhi yao kupoteza maisha ndio maana nikafanya ziara maalum huko ya kutembelea viwanda hivyo na nilipochukua sampuli katika moja ya viwanda, hayo ndio majibu yake," alisema.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa, mara nyingi imekuwa vigumu kubaini pombe ambazo hazifai kwa matumizi ya binadamu kutokana na udanganyifu unaotumiwa na baadhi ya watendaji wasio waaminifu.
Alisema wilaya hiyo imekuwa na matumizi makubwa ya pombe zisizo rasmi ambazo zinachangia kupoteza nguvu kazi ya taifa, ongezeko la matukio ya kihalifu na migogoro ya ndoa.
Akizungumzia zaidi madhara ya pombe hiyo, Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini, Happy Kanyeka, alisema sampuli waliyopokea kutoka kwenye kiwanda hicho imeonyesha pombe hiyo haikidhi kiwango cha ubora.
“Pombe hiyo aina ya Banana inayozalisha kiwandani hapo haitauzwa mpaka pale TBS itakapofanya uchunguzi wa kina, tutaangalia mchakato mzima wa uzalishaji, tutachukua sampuli nyingine tena na kiwanda hicho kitakuja kufunguliwa baada ya kujiridhisha na ubora wake.
“Pia tumekubaliana tutapitia viwanda vyote vinavyozalisha pombe aina hiyo katika mkoa wa Kilimanjaro na mikoa jirani kuangalia kama vinakidhi viwango.
"Ingawa tulifanya ukaguzi Septemba mwaka huu, tutarudia hasa kwenye viwanda vya Banana, tutafanya utafiti kuona madhara yanayowakumba watu wa wilaya ya Rombo yanatokana na nini kinachowekwa kwenye pombe hiyo," alifafanua.
Alisema katika sampuli iliyochukuliwa awali imeonyesha uwapo wa (Asetic Acid) nyingi hali inayopelekea kushindwa kukaa kwa muda uliokusudia.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo waliozungumza na Nipashe, akiwamo Deogratus Tarimo, walisema hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuchukua sampuli katika viwanda kutasaidia kuleta mabadiliko.
“Kwa sasa hatuna vijana, wengi wamejiingiza kwenye pombe, matukio ya uhalifu na mauaji yamekithiri na migogoro ya kifamilia imeongezeka.
"Tunaomba serikali ifungie viwanda vyote ambavyo havikidhi matakwa ya kitaalamu na kisha wafanyabiashara wawekewe utaratibu maalum wa kuomba vibali ili kufungua biashara hizo upya,” alisema.
Chanzo: NIPASHE
Hoja ya mdau inapatikana hapa Unywaji wa pombe aina ya Banana inaathiri nguvu kubwa sana ya vijana
==========
Serikali imesitisha uzalishaji wa pombe aina ya Banana inayozalishwa na kiwanda cha Tanbasi Investment kilichoko Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro baada ya kubainika kushindwa kukidhi viwango vya ubora.
Jana Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, alitangaza kufungwa kwa kiwanda hicho kutokana na ripoti ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Kagaigai alifikia uamuzi huo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wataalamu wa TBS.
“Ripoti ya TBS inaonyesha kuwa sampuli za pombe hiyo zilizopelekwa huko hazifai kwa matumizi ya binadamu kutokana na kuongezwa kiwango kikubwa cha kemikali ya Asetic Acid.
“Nilivyokuja Kilimanjaro, niliambiwa na viongozi wa dini kwamba Rombo kuna viwanda vingi vya kutengeneza pombe, ambazo hazina ubora na zinaleta madhara kwa binadamu.
“Nikaelezwa zipo zilizosababisha baadhi yao kupoteza maisha ndio maana nikafanya ziara maalum huko ya kutembelea viwanda hivyo na nilipochukua sampuli katika moja ya viwanda, hayo ndio majibu yake," alisema.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa, mara nyingi imekuwa vigumu kubaini pombe ambazo hazifai kwa matumizi ya binadamu kutokana na udanganyifu unaotumiwa na baadhi ya watendaji wasio waaminifu.
Alisema wilaya hiyo imekuwa na matumizi makubwa ya pombe zisizo rasmi ambazo zinachangia kupoteza nguvu kazi ya taifa, ongezeko la matukio ya kihalifu na migogoro ya ndoa.
Akizungumzia zaidi madhara ya pombe hiyo, Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini, Happy Kanyeka, alisema sampuli waliyopokea kutoka kwenye kiwanda hicho imeonyesha pombe hiyo haikidhi kiwango cha ubora.
“Pombe hiyo aina ya Banana inayozalisha kiwandani hapo haitauzwa mpaka pale TBS itakapofanya uchunguzi wa kina, tutaangalia mchakato mzima wa uzalishaji, tutachukua sampuli nyingine tena na kiwanda hicho kitakuja kufunguliwa baada ya kujiridhisha na ubora wake.
“Pia tumekubaliana tutapitia viwanda vyote vinavyozalisha pombe aina hiyo katika mkoa wa Kilimanjaro na mikoa jirani kuangalia kama vinakidhi viwango.
"Ingawa tulifanya ukaguzi Septemba mwaka huu, tutarudia hasa kwenye viwanda vya Banana, tutafanya utafiti kuona madhara yanayowakumba watu wa wilaya ya Rombo yanatokana na nini kinachowekwa kwenye pombe hiyo," alifafanua.
Alisema katika sampuli iliyochukuliwa awali imeonyesha uwapo wa (Asetic Acid) nyingi hali inayopelekea kushindwa kukaa kwa muda uliokusudia.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo waliozungumza na Nipashe, akiwamo Deogratus Tarimo, walisema hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuchukua sampuli katika viwanda kutasaidia kuleta mabadiliko.
“Kwa sasa hatuna vijana, wengi wamejiingiza kwenye pombe, matukio ya uhalifu na mauaji yamekithiri na migogoro ya kifamilia imeongezeka.
"Tunaomba serikali ifungie viwanda vyote ambavyo havikidhi matakwa ya kitaalamu na kisha wafanyabiashara wawekewe utaratibu maalum wa kuomba vibali ili kufungua biashara hizo upya,” alisema.
Chanzo: NIPASHE