Serikali iingilie kati suala la ulevi Moshi Mjini

We kijana, unaposema pesa zao zinapotelea kwenye pombe unataka sisi wauza pombe familia zetu zisiende chooni sio??

Acha roho mbaya ndgu yangu.
 
Pamoja na kwamba tuna serikali isiyofuata utawala wa kisheria lakini Sina budi kutoa wito kuwa unywaji wa pombe Moshi umevuka mipaka yani si wazee si watoto unakuta wote wanalewa halafu bila kuzingatia muda wa kufungua bar.

Ajabu zaidi mkoa huu bar zinafunguliwa asubuhi Sawa na mtu anayeuza Nyanya Sokoni. Kwakweri serikali fanyeni hima mnusuru kipato cha wachaga hawa maana asilimia nyingi ya fedha zao zinapotea kwenye pombe.

Natumai mtalisikia hili asanteni saaana.
#mbowesiogaidi View attachment 2002023

Sent from my Infinix X606D using JamiiForums mobile app
Mbowe mwenyewe mlevi.
 
icho kifungu kipo lakini kwa ukweli kimepitwa na wakati dunia ya sasa inatakiwa izunguke masaa 24 watu wapeane shift uchumi wa kulala kama burundi nadhani unayaona madhara yake taifa hilo ni duni mno kiuchumi kwa ajili ya kulala ovyo
Ha ha watu wanaendekeza sana kulala hii bongo
 
20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu. (Mithali 23:20-21)
 
Wahehe wanakuangalia halafu wanacheka kwa chini chini.
Huko Iringa ulanzi umeanza hadi mwezi wa saba mwakani ndio utaanza kupungua.
 
20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu. (Mithali 23:20-21)
Amen amen mtumishi wa Bwana.
 
Sidhani kama mangi watakuacha salama.
Tunakunywa bia maana tuna hela na maendeleo,maskini anakunywaga bia?
Kampuni ya TBL inaongoza kwa kulipa kodi kuzidi kampuni yoyote,na tbl wateja wao namba 1 ni Kilimanjaro
Sisi Kilimanjaro tuna maendeleo ni mkoa wa pili tz watu wake kuwa na kipato kikubwa,maisha bora,miundombinu borana makazi bora(bila kusahau makanisa ya kisasa vijijin) mm namshauri mtoa mada akawasaidie wale wa mikoa maskini (hasa kagera) wajikwamue na umaskini wao wa kipato Sisi Kilimanjaro bia hazina tatizo.
 
Tunakunywa bia maana tuna hela na maendeleo,maskini anakunywaga bia?
Kampuni ya TBL inaongoza kwa kulipa kodi kuzidi kampuni yoyote,na tbl wateja wao namba 1 ni Kilimanjaro
Sisi Kilimanjaro tuna maendeleo ni mkoa wa pili tz watu wake kuwa na kipato kikubwa,maisha bora,miundombinu borana makazi bora(bila kusahau makanisa ya kisasa vijijin) mm namshauri mtoa mada akawasaidie wale wa mikoa maskini (hasa kagera) wajikwamue na umaskini wao wa kipato Sisi Kilimanjaro bia hazina tatizo.
Sasa Kagera hapa inahusikaje na uzi wenu na huo ulevi wenu. Wewe ndugu ukabila umekutawala. Yaani bila kuisema au kujilinganisha na Kagera hamujisikiagi vizuri et.
 
Back
Top Bottom