Serikali ianzishe "Maafisa Kodi wa Kata" na TRA ianzishe "mawakala" wa TRA

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,114
115,937
Huu mzozo wa Kodi Kariakoo ni sehemu ndogo Sana ya matatizo ya Kodi nchini.

Matokeo yake kuna wasiolipa Kodi wakiamini ni ujanja. Kuna wanaolipa Kodi zaidi ya kiwango wakikosa elimu husika. Kuna wasiolipa Kodi stahiki pia wakikosa elimu stahiki ya Kodi n.k..

Ushauri wangu Kwa serikali lazima hasa Kwa majiji makubwa kama Dar na mengine akawepo "afisa Kodi WA kata".. huyu kazi yake kubwa kuelimisha mwananchi Umuhimu WA Kodi na why alipe Kodi na Kodi stahiki Kwa Aina ya kipato chake ni ipi......akiwepo afisa Kodi WA kata atasaidia pia kuishauri serikali Kodi kero za kufutwa ....huyu afisa Kodi atahusika na Kodi zote .ziwe za TRA, za manisapaa... ushuru, tozo... kazi yake ni kuishauri serikali kupanga viwango husika na kutoa elimu Kwa mwananchi...

Kingine TRA sasa wawe na mawakala wa TRA... kazi Yao ni kuisaidia tra makusanyo Kwa ukaribu... mawakala since itawalipa hiyo kazi Kwa commission wanaweza kuwa Wengi mitaani... TRA ikawa train na kuwapa miiko ya kazi ...na wakawa wanafanya kazi chini ya afisa Kodi WA kata... cha muhimu ni system nzuri itakayokuwa transparent na itasaidia sana kuepusha migogoro na watu kukwepa kodi....

Mwisho kila Mtanzania sasa alipwe tax returns na aelimishwe faida za Kodi Kwa Taifa ...hii pia itasaidia sana watu kutokukwepa Kodi ..
 
Naunga mkono hoja
 
Yaani mnacho shauri huwa mna exclude Halmashauri, utafikiri Halmashauri siyo sehemu ya Serikali.

Tatizo kubwa la nchi hii, hakuna Muunganiko.

Serikali Kuu na taasisi zake inajipendelea kwenye kila kitu (nadhani isipokuwa Maafisa Tarafa) wanaofanya kazi chini ya DC.

Watumishi unaowasema waote wanaweza kupatikana chini ya Halmashauri.

Halmashauri zinaendeshwa Kama watu hawakwenda shule.

Ziko zig zag, Kwasababu serikali inathamini zaidi watu wanaoifadisha na siyo watu wanaofaidisha jamii.


Yaani wewe Mhasibu unayehudumia watu 3,000 huko TAMISEMI huna maana, ila Mhasibu mwenye elimu kama wewe huko TRA anaishi ulimwengu mwingine kabisa.

Shida kubwa kwa sheria za fedha za nchi hii.

  • Halmashauri zinakaa zinatunga Sheria ndogo.
  • Serikali kuu (Mof) inakaa inatunga sheria
  • Taasisi (TMDA, TBS, TMDA,NEMC, Bodi ya Nyama, Bodi ya KOROSHO, Bodi ya Pamba, Bodi ya Kahawa, Ufuta nk) wanakaa wanatunga sheria.


Hawa wote kila mmoja anakaa anatunga kwa wakati wake, bila kumhusisha mwenzake na TARGET ni mtu MMOJA yule yule. Lazima aumie.

Suluhisho kubwa:

- Kuwekwe utaratibu (mmoja) suala lolote linalohusu kukusanya mapato kutoka kwa mtu litokee sehemu moja, ili kuepeuka kukomaa na mtu kwa Kodi 1,000 bila kujia.

- Kuongeza wigo wa Kodi ( hii itapunguza ukubwa wa Kodi, kwa mtu mmoja mmoja).
 
Good idea
 

Afisa Kodi WA kata si ataripoti Halmashauri?but akihusika na Kodi zote including za TRA ndo maana nimesema Afisa Kodi wa kata ahusike na Kodi zote...na ashauri viwango..
 
Kwani hawa viongozi wetu wanaodhurura huko nje huwa wanajifunza nini..

Si waangalie kwa wazungu huko mifumo ya kikodi inavyoowana baina ya taasisi na taasisi za serikali bila kumbukudhi mfanyabiashara wala mwananchi.

viongozi wetu wanashida gani jamani?
 
 
Kwa sasa Halmashauri na serikali kuu, ni SERIKALI MBILI tofauti na haziingiliani.

Halmashauri Zina mtunza hazina wake na TRA Wana taratibu zao na ofisi zao.

Yes ..sasa huyu afisa Kodi WA kata anapaswa kuwa kiunganishi..
Akija Kwa mfanyabiashara anakuelekeza.... kila kitu.but mostly important tuwe na mfumo mmoja wa kulipa Kodi .... Taasisi zioane kimfumo ..masuala ya makato wajue wenyewe ipi inaenda tra na ipi inabaki manispaa
 
Ni kweli kabisa.
Yani unakuta mtu unalipa kodi ya mapato TRA halafu nao halmashauri wanakuja kukutoza kodi kama Ya LESENI na SERVICE LEVY..What the Fu......!bado kuna Fire Xtinguisher nk

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Sheria za huko nje za kodi ni kali sana. Ukikwepa kodi unafungwa bila mzaha. Nchi kama USA, maafisa wa kodi wa IRS ni kama jeshi, na hata bastola wanabeba.
 
Sasa nadhani tafsiri yako, unapendekeza Hazina ya Halmashauri iwe na madirisha ya Halmashauri na TRA?

Kwasababu sasa hivi, hata mfumo wa mapato ya Halmashauri unaelekea kuwa SELF SERVICE.
Hata leseni siku hizi, Wana mfumo unaitwa TAUSI.TAMISEMI.GO.TZ.

Binafsi, naona suala gumu ni ushirikiano.
Unajua hata utaratibu wa Leseni ya biashara kabla ya kutoa inatakiwa ipite kwa Wenyeviti wa vijiji,Afisa Afya,Afisa Ardhi.

Lakini huo utaratibu haufuatwi
Kwahiyo, hata ukiwa na TRA kata, huo ushirikiano atapewa??
 
Welll noted

Ukisikia hiii ndo Intelligence!!!
 

Wakipewa maelekezo washirikiane ...itawezekana Sana but mostly important mawakala wa kodi ambao wao wanapata commission...wakimsaidia mtu kulipa Kodi zake stahiki bila kwenda tra wala manispaa wakiwepo watasaidia sana...pamoja na kutoa elimu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…