Serikali iangalie upya sheria iliyofuta kiinua mgongo kwa wastaafu

uchumi2018

JF-Expert Member
Mar 4, 2018
1,424
1,966
Amani kwenu wana jamvi,

Nimetafakari sana nikaona kupitia jukwaa hili nipeleke ombi kwa serikali juu ya kiinua mgongo kwa wastaafu. Nikiri wazi kuwa mimi ni mfanyakazi kwenye makampuni ya watu binafsi, nimeshuhudia watu wakistaafu miaka ya nyuma na wengine waliostaafu miaka ya hivi karibuni ikiwemo mwaka huu baada ya sheria kubadilishwa.

Kule nyuma kulikuwepo kiinua mgongo kilitajwa kwenye sheria ya kazi, nakumbuka yakafanyika marekebisho
kutoka viwango vilivyokuwepo mpaka kikawekwa mstaafu kulipwa kiwango cha mshahara wa siku saba kwa kila mwaka.

aliofanyakazi kwa muda usiozidi miaka kumi hata kama umetumika zaidi ya miaka kumi,ikiwa na maana unalipwa siku sabini kama kiinua mgongo. Baadaye yakafanyika marekebisho mengine,hizo siku saba nazo zikafutwa kwenye sheria kwa maelezo kwamba mwajiri.

Anamchangia mfanyakazi kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii na hivyo akistaafu atapewa mafao yake huko.
Jambo hili limeendelea kufanyika hivyo hasa kwenye makampuni yetu yanayotegemea sheria za nchi zinasemaje,
sheria ikileta neema mnaneemeka ikileta balaa mnalipata, ilimradi ni kwa mujibu wa sheria.

Mshangao wangu namba moja ni huu,mtumishi anaitumikia kampuni kwa uaminifu, anastaafu kwa heshima
anaambiwa nenda kwa amani, utapata haki yako kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii. Na mtumishi mwingine anaenda kinyume na maadili anafukuzwa kwa mujibu wa sheria, huyu haagwi wala kuambiwa neno lolote la heri, lakini wanakutana na aliyeagwa kwa maneno ya heri kibao wote wanakutana kwenye benchi moja la mfuko wa hifadhi ya jamii kupata iliyo haki yao.

Mshangao wangu namba mbili, ni kwamba kwa sasa mifuko ya hifadhi ya jamii haitoi hayo mafao kwa wastaafu kwa wakati. watu wanakaa miezi tisa na kuendelea bila ya kupata chochote,huku hawana mshahara, maana wameishatoka kweye pay rolls za kampuni zao na hakuna fedha yoyote waliyopewa kama kiinua mgongo cha kuwasaidia wakati wanasubiri mifuko ya hifadhi ya jamii kufanya kazi zao. Matokeo yake utakuta pale kwenye benchi la ufuatiliaji wa mafao, aliyefukuzwa kazi au kwa kula rushwa au kuiibia kampuni iwe mali au muda kwa kwenda kwenye mishe zake ana hali bora kuliko mstaafu aliyestaafu kwa heshima. Hili jambo linaacha urithi mbaya kwa jamii.

Nihitimishe kwa kushauri,serikali irejeshe kisheria,fao la kiinua mgongo. Kama itaonekana linaongeza mzigo kwa wenye makampuni, basi ile fedha ya maafa anayotoa (WCF) ambayo mwajiri anamlipia kila mfanyakazi kila mwezi,endapo mfanyakazi huyo atafikia muda wa kustaafu bila kupatwa na maafa, basi serikali impatie sehemu ya ile fedha kama sehemu ya kiinua mgongo. Ili kumpunguzia makali ya kukosa mshahara na mafao muda wa miezi hiyo ya kusubiri.

Naomba kuwasilisha,
Kama una maoni zaidi unaweza kuongezea ili kuboresha.
lengo ni kwamba tujenge mfumo wa kuwafanya watumishi kufanyakazi.
kwa weredi na uaminifu wakijua hata wakistaafu hawataenda kuadhirika. Lakini pia kuwarithisha vijana
imani ya kwamba ukitumika kwa uaminifu unatunzwa, badala ya kushuhudia baba/ mama zao wakivuna mabaya
kwa utumishi wao uliotukuka.
 
Kwani hiyo mifuko ya Pensheni kwa sasa ina kitu chochote?
Kwa sehemu kubwa inaaminika kuwa ilishafirisiwa kimtindo fulani na serikali.

Kwa sasa ukiona mtu analipwa kiinua mgongo kipindi hiki ujue ni pesa iliyotoka kwenye makato ya wafanyakazi wengine wa wakati huu, kile alichochangia mstaafu husika wakati akiwa kazini, hakipo na hakita kuja kuwepo milele.
 
Kwani hiyo mifuko ya Pensheni kwa sasa ina kitu chochote?
Kwa sehemu kubwa inaaminika kuwa ilishafirisiwa kimtindo fulani na serikali.

Kwa sasa ukiona mtu analipwa kiinua mgongo kipindi hiki ujue ni pesa iliyotoka kwenye makato ya wafanyakazi wengine wa wakati huu, kile alichochangia mstaafu husika wakati akiwa kazini, hakipo na hakita kuja kuwepo milele.
Hoja yangu ni tofauti kidogo na hili uliloeleza hapo juu,Ni kwamba zamani kiinua mgongo ni tofauti na pesa iliyowekwa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.

Mfano sheria iliyofutwa kabla ya utaratibu wa sasa ilikuwa inataja kabisa kwamba mstaafu atalipwa mshahara wake wa siku saba kwa kila mwaka aliotumika kazini kwa kipindi kisichozidi miaka kumi.Hii fedha mstaafu alikuwa anapewa na ndipo anaanza process za kufuatilia pension.

Hiyo fedha ilisaidia sana kumtunza mhusika wakati akisubiria hayo mafao ya mifuko ya hifadhi ya jamii tofauti na hali ilivyo kwa sasa.
 
Maoni yako mazuri sana sana.
Isipokuwa hapo kwenye mtu aliye fukuzwa au kuachiashwa kazi.

Mtu aliyefukuzwa kazi kwa makosa ya uadilifu au kukiuka sheria na kanuni za kampuni unashindwaje kumlipa mafao yake yaliyotokana na makato ya mishahara wake na aliyolipiwa na mwajiri wakati uliopita alipokuwa hajatenda kosa, alipokuwa mwadilifu?

kwanini ahukumiwe hadi muda uliopita kwa makosa ya sasa?
Tukikubali hili suala basi watu watafukuzwa kazi ovyo ili kukoseshana mafao kwa kukomoana au mwajiri kukwepa makato ya mifuko ya kijamii.

Labda useme aliyefukuzwa kwa wizi ndiye ashitakiwe mahakamani akikutwa na kosa labda akatwe kwenyeafao yake sawa thamani ya alichoiba kama hakukirudisha baada ya kukamatwa na wizi.
Kama alirudisha hapo hapo asikatwe kitu, afukuzwe lakini alipwe mafao yake yote.

Tuache ubinafsi.
 
Kwani hiyo mifuko ya Pensheni kwa sasa ina kitu chochote?
Kwa sehemu kubwa inaaminika kuwa ilishafirisiwa kimtindo fulani na serikali.

Kwa sasa ukiona mtu analipwa kiinua mgongo kipindi hiki ujue ni pesa iliyotoka kwenye makato ya wafanyakazi wengine wa wakati huu, kile alichochangia mstaafu husika wakati akiwa kazini, hakipo na hakita kuja kuwepo milele.
 
Maoni yako mazuri sana sana.
Isipokuwa hapo kwenye mtu aliye fukuzwa au kuachiashwa kazi.

Mtu aliyefukuzwa kazi kwa makosa ya uadilifu au kukiuka sheria na kanuni za kampuni unashindwaje kumlipa mafao yake yaliyotokana na makato ya mishahara wake na aliyolipiwa na mwajiri wakati uliopita alipokuwa hajatenda kosa, alipokuwa mwadilifu?

kwanini ahukumiwe hadi muda uliopita kwa makosa ya sasa?
Tukikubali hili suala basi watu watafukuzwa kazi ovyo ili kukoseshana mafao kwa kukomoana au mwajiri kukwepa makato ya mifuko ya kijamii.

Labda useme aliyefukuzwa kwa wizi ndiye ashitakiwe mahakamani akikutwa na kosa labda akatwe kwenyeafao yake sawa thamani ya alichoiba kama hakukirudisha baada ya kukamatwa na wizi.
Kama alirudisha hapo hapo asikatwe kitu, afukuzwe lakini alipwe mafao yake yote.

Tuache ubinafsi.
Ndugu yangu kwa namna tulivyozoea taratibu zilivyo,ukifanya kosa linalostahili kufukuzwa kazi(hapa siongelei kuonewa)
endapo inadhihirika kwamba ni kosa mfano kuiba mali ya mwajiri wako n.k hakuna mafao unayostahili kupewa,ndo maana ya kupoteza haki zako.Isipokuwa hiyo fedha uliyokwishapelekewa kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.
Hoja yangu/swali langu ni kwamba ''endapo hakuna kiinua mgongo kwa wastaafu,nini tofauti ya aliyetumika mpaka akastaafu kwa heshima na aliyefukuzwa kazi kwa kuvunja maadili ilihali wote wanakutana kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kulipwa iliyo haki yao?

Nilitegemea huyu aliyevumilia mpaka akastaafu, apewe chochote kama ishara ya kutambua uvumilivu wake.
Huenda kuna mashirika au taasisi zinazofanya hivyo,siongelei hayo,naongelea makampuni yaliyokuwa yanatoa
kiinua mgongo wakati haki hiyo ilipokuwa inatajwa kwenye sheria ya kazi.Na kuondoa fao hilo mara tu
baada ya kuondolewa kwenye sheria za kazi.Hapa kutofautisha aliyefukuzwa kazi na aliyestaafu kwa heshima ni shughuli.
 
450908765.jpg
 

SEVERANCE PAY​

The Employment and Labour Relations Act 2004 provides for Severance Pay. Worker is entitled to the severance pay if he/she has completed at least a year of a service with the employer. Severance pay in Tanzania is equal to at least 7 days basic wage for each completed year of employment up to a maximum of ten years.

Severance pay is not payable if an employment is terminated on account of misconduct, incapacity and incompatibility with requirements of business but who unreasonably refuses to accept alternative employment with that employer or any other employer, and if the worker has reached the retirement age or if the employment contract has expired or ended by reason of time. Payment of severance pay does not affect the rights of a worker to any other payable amount.

Source: §42 of Employment and Labour Relations Act 2004
Hii ndo ya zamani
Mtu aliyefukuzwa kazi kwa makosa ya uadilifu au kukiuka sheria na kanuni za kampuni unashindwaje kumlipa mafao yake yaliyotokana na makato ya mishahara wake na aliyolipiwa na mwajiri wakati uliopita alipokuwa hajatenda kosa, alipokuwa mwadilifu?

SEVERANCE PAY​

The Employment and Labour Relations Act 2004 provides for Severance Pay. Worker is entitled to the severance pay if he/she has completed at least a year of a service with the employer. Severance pay in Tanzania is equal to at least 7 days basic wage for each completed year of employment up to a maximum of ten years.

Severance pay is not payable if an employment is terminated on account of misconduct, incapacity and incompatibility with requirements of business but who unreasonably refuses to accept alternative employment with that employer or any other employer, and if the worker has reached the retirement age or if the employment contract has expired or ended by reason of time. Payment of severance pay does not affect the rights of a worker to any other payable amount.

Source: §42 of Employment and Labour Relations Act 2004
 
Back
Top Bottom