Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,821
- 71,274
Hii kauli ya kuzaa bila kufuata uzazi wa mpango ambayo ni Sera ya taifa ni kuvuruga watu.
Sasa mkuu wa mkoa wa Mwanza ana hamasisha wananchi masikini vijijini kuzaana sana "eti kuwa na Magufuli wengi" ni upotoshaji mkubwa sana, labda nia yake ni kuongeza idadi ya kaya masikini zinazo hudumiwa na TASAF.
Tabia hii ya viongozi kuropoka ropoka ili kutafuta sifa za kumuunga mkono Rais zinazidi kulipotosha taifa na kufanya hata hao wahisani kutuona mazuzu.