Sensa 2022: Serikali iwe makini, suala la takwimu halihitaji mzaha!

Lanlady

JF-Expert Member
Feb 27, 2019
1,422
4,730
Katika zoezi la uwekaji wa anuani za makazi, bila shaka kila mmoja wetu ameshuhudia baadhi ya kasoro zilizojitokeza.
Wengi wamelaumu wizara ya habari na mawasiliano kwa kuwa waziri wake alionekana kufuatilia kwa karibu zoezi hilo.

Lakini tuseme ukweli, watekelezaji wa mwisho (watendaji, wenyeviti wa mtaa/vijiji, na mawakala wa sensa ngazi za mtaa) ndio hasa walipaswa kulaumiwa.
Japo na wao pia wangeweza kujitetea.
Kazi ilikuwa ngumu, malipo kidogo. Iliitwa kazi ya KIZALENDO.

Sasa basi, wito wangu ni kwenye zoezi la kukusanya takwimu (sensa) hapa hapahitaji kabisa mzaha. Endapo taifa litashindwa kupata takwimu sahihi za watu wake katika kila kipengele kilichokusudiwa, ni vigumu sana kuweka mipango sahihi (Proper planning).
Zoezi la kupata takwimu sahihi linahitaji uaminifu na uzalendo wa kweli.

Ushauri: kama serikali itaona haina uwezo wa kuwalipa vizuri mawakala wa sensa, ni afadhali kusitisha zoezi hilo au kutafuta mbinu nyingine ya kupata takwimu hata kama itachukua muda mrefu. Mfano kuwatumia mabalozi na wenyeviti wa mtaa. Kuliko kushuhudia kile kilichofanyika kwenye zoezi la anuani za makazi.

Ukweli ni kwamba,( kwa mujibu wa baadhi ya mawakala) 'walipika' taarifa ili kujiongezea malipo kwani walipaswa kulipwa kuanzia kaya 20 kwa siku moja.
Na hii inaweza kuwa kweli kwasababu baadhi ya mawakala hawakutumia simu kujaza taarifa; na wala hawakuchukua taarifa zote. Waliandika taarifa chache kwenye daftari na kisha kuondoka kwa madai kwamba watazi 'upload' baadae kwenye mfumo!

Suala la Takwimu halihitaji mzaha!
 
... nakumbuka sensa iliyopita (2012) baadhi ya makundi yaliisusia kwa sababu ya kipengele kilichojulikana kama "dini" kutokuwepo kwenye dodoso. Sensa hii kitakuwepo? Maana kelele hazijasikika so far! Kama bado hisia hizo bado zingalipo, serikali imejipangaje ili kupata takwimu sahihi tofauti na 2012 ambapo kwa vigezo vyovyote vile sensa ile ilifeli?
 
Katika zoezi la uwekaji wa anuani za makazi, bila shaka kila mmoja wetu ameshuhudia baadhi ya kasoro zilizojitokeza.
Wengi wamelaumu wizara ya habari na mawasiliano kwa kuwa waziri wake alionekana kufuatilia kwa karibu zoezi hilo.

Lakini tuseme ukweli, watekelezaji wa mwisho (watendaji, wenyeviti wa mtaa/vijiji, na mawakala wa sensa ngazi za mtaa) ndio hasa walipaswa kulaumiwa.
Japo na wao pia wangeweza kujitetea.
Kazi ilikuwa ngumu, malipo kidogo. Iliitwa kazi ya KIZALENDO.

Sasa basi, wito wangu ni kwenye zoezi la kukusanya takwimu (sensa) hapa hapahitaji kabisa mzaha. Endapo taifa litashindwa kupata takwimu sahihi za watu wake katika kila kipengele kilichokusudiwa, ni vigumu sana kuweka mipango sahihi. (Proper planning)
Zoezi la kupata takwimu sahihi linahitaji uaminifu na uzalendo wa kweli.

Mwisho, kama serikali itaona haina uwezo wa kuwalipa vizuri mawakala wa sensa, ni afadhali kusitisha zoezi hilo au kutafuta mbinu nyingine ya kupata takwimu hata kama itachukua myda mrefu. Mfano kuwatumia mabalozi na wenyeviti wa mtaa. Kuliko kushuhudia kile kilichofanyika kwenye zoezi la anuani za makazi.

Ukweli ni kwamba,( kwa mujibu wa baadhi ya mawakala) 'walipika' taarifa ili kujiongezea malipo kwani walipaswa kulipwa kuanzia kaya 20 kwa siku moja.
Na hii inaweza kuwa kweli kwasababu baadhi ya mawakala hawakutumia simu kujaza taarifa; na wala hawakuchukua taarifa zote. Waliandika taarifa chache kwenye daftari na kisha kuondoka kwa madai kwamba watazi 'upload' baadae kwenye mfumo!

Suala la Takwimu halihitaji mzaha!
Umekoroga sehemu moja tu... Nchi hii ujinga ulivuopitiliza ukisema neno uzalendo unamaanisha vitu wanaccm na wanaolipwa kidogo.
Hivyo unaweza kuwapa andiko la kujitetea kufanya kimojawapo au vyote viwili.
 
... nakumbuka sensa iliyopita (2012) baadhi ya makundi yaliisusia kwa sababu ya kipengele kilichojulikana kama "dini" kutokuwepo kwenye dodoso. Sensa hii kitakuwepo? Maana kelele hazijasikika so far! Kama bado hisia hizo bado zingalipo, serikali imejipangaje ili kupata takwimu sahihi tofauti na 2012 ambapo kwa vigezo vyovyote vile sensa ile ilifeli?
Kwa hiyo kukosekana tu kwa kipengele dini basi wakasusia... Dini ndo hizi zilizokuja na meli?
Wengine tuliwasubiria wahesabuji lakini hawakutokea... This time wasituhadae tena.
 
Believe me, wrong data will be obtained. I disliked jiwe, but in this issue he could do best.
Jiwe alitumia walimu kuiba kura angewezaje ku do the best? Ndugu amini mfumo uliopo pekee ndio unakuvusha kwa sasa kwa speed yoyote ile tulia tu.
 
Mama yangu ni mwalimu mstaafu na alikuwa hataki kwenda kuiba kura. Asilimia kubwa ya walimu ni vilaza wa kupelekeshwa.

Kazi wapewe vijana wenye weledi.
Na mama yako ni kilaza? Au wewe mwenyewe ni kilaza? Usiwatukane walimu waliokujengea uwezo ulionao hata namna ya kufikiri na kuongea. Jenga hoja isiyo na maneno makali dhidi ya wazazi wako ndugu?

Mfano. Baada ya kuwa askali wewe unaongoza operation ya kukamata wauza gongo usiku na mchana hulali na wakati kula kwako kusoma kwako kuvaa kwako kumetokana na mama yako kuuza gongo nakuthibitishia utapata laana mbaya sana unaweza kuwa unaongea peke yako barabarani mzee.
 
Na mama yako ni kilaza? Au wewe mwenyewe ni kilaza? Usiwatukane walimu waliokujengea uwezo ulionao hata namna ya kufikiri na kuongea. Jenga hoja isiyo na maneno makali dhidi ya wazazi wako ndugu?

Mfano. Baada ya kuwa askali wewe unaongoza operation ya kukamata wauza gongo usiku na mchana hulali na wakati kula kwako kusoma kwako kuvaa kwako kumetokana na mama yako kuuza gongo nakuthibitishia utapata laana mbaya sana unaweza kuwa unaongea peke yako barabarani mzee.
Sijasema walimu wote ni vilaza na nimemtaja mama kwasababu amekuwa mfano wa walimu waliokataa kutumika. Walimu wengi umasikini umejaa kichwani mpaka wamekuwa vilaza.

Wapewe vijana wenye digrii walioko mtaani.
 
Katika zoezi la uwekaji wa anuani za makazi, bila shaka kila mmoja wetu ameshuhudia baadhi ya kasoro zilizojitokeza.
Wengi wamelaumu wizara ya habari na mawasiliano kwa kuwa waziri wake alionekana kufuatilia kwa karibu zoezi hilo.

Lakini tuseme ukweli, watekelezaji wa mwisho (watendaji, wenyeviti wa mtaa/vijiji, na mawakala wa sensa ngazi za mtaa) ndio hasa walipaswa kulaumiwa.
Japo na wao pia wangeweza kujitetea.
Kazi ilikuwa ngumu, malipo kidogo. Iliitwa kazi ya KIZALENDO.

Sasa basi, wito wangu ni kwenye zoezi la kukusanya takwimu (sensa) hapa hapahitaji kabisa mzaha. Endapo taifa litashindwa kupata takwimu sahihi za watu wake katika kila kipengele kilichokusudiwa, ni vigumu sana kuweka mipango sahihi (Proper planning).
Zoezi la kupata takwimu sahihi linahitaji uaminifu na uzalendo wa kweli.

Ushauri: kama serikali itaona haina uwezo wa kuwalipa vizuri mawakala wa sensa, ni afadhali kusitisha zoezi hilo au kutafuta mbinu nyingine ya kupata takwimu hata kama itachukua muda mrefu. Mfano kuwatumia mabalozi na wenyeviti wa mtaa. Kuliko kushuhudia kile kilichofanyika kwenye zoezi la anuani za makazi.

Ukweli ni kwamba,( kwa mujibu wa baadhi ya mawakala) 'walipika' taarifa ili kujiongezea malipo kwani walipaswa kulipwa kuanzia kaya 20 kwa siku moja.
Na hii inaweza kuwa kweli kwasababu baadhi ya mawakala hawakutumia simu kujaza taarifa; na wala hawakuchukua taarifa zote. Waliandika taarifa chache kwenye daftari na kisha kuondoka kwa madai kwamba watazi 'upload' baadae kwenye mfumo!

Suala la Takwimu halihitaji mzaha!
Waweke mpunga tuu
 
Back
Top Bottom