Sendeka amesimama kuhesabiwa kuhusu Tanganyika

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
"Waziri amesema moja kati ya mambo yaliyosababisha mabadiliko ya Katiba, ni mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar. Mabadiliko yale yameifanya Zanzibar kuwa nchi kamili. Na sisi tudai Serikali ya Tanganyika. Mwambieni Rais (Jakaya) Kikwete hivyo," alisema Sendeka

Mwanzo wa G55 nyingine?

MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, wamezozana hadharani wakipishana maneno kuhusu Muswada wa Mabadiliko ya Katiba. Mzozo huo ulizuka juzi kwenye mkutano wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (Alat) uliofanyika Kunduchi, Dar es Salaam juu ya mada ya Mabadiliko ya Katiba.

Baada ya Masaju kumaliza kuelezea madhumuni ya muswada huo, Sendeka alisimama na kuhoji kuhusu kauli iliyotolewa awali kwenye mkutano huo na Waziri Kombani kuwa, moja ya sababu za kuandikwa kwa Katiba mpya ni mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar iliyounda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Sendeka alisema mabadiliko hayo yameifanya Zanzibar kuwa nchi kamili, hivyo ni muhimu sasa kwa Watanganyika nao wadai serikali yao. "Waziri amesema moja kati ya mambo yaliyosababisha mabadiliko ya Katiba, ni mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar. Mabadiliko yale yameifanya Zanzibar kuwa nchi kamili. Na sisi tudai Serikali ya Tanganyika. Mwambieni Rais (Jakaya) Kikwete hivyo," alisema Sendeka.

Hata hivyo, wakati wa kujibu maswali, Masaju alisema Zanzibar siyo nchi kwa maana ya dola, bali ni kwa maana ya mipaka.
"Siyo kweli kwamba Zanzibar ni nchi kwa maana ya dola, bali ni nchi kutokana na mipaka yake," alisema Masaju kwa hasira huku akinukuu baadhi ya vifungu vya Katiba ya Zanzibar na kuongeza:"Someni Katiba ya Zanzibar na hati za muungano."

Baada ya Masaju kukaa, Sendeka alisimama tena na kusema: "Sawa, yaani unatujibu kwa hasira hivyo? Katiba ya Zanzibar imetoa madaraka makubwa. Zamani kwa kesi za Mahakama ya Rufaa walikuwa wakija huku (Tanzania Bara), lakini siku hizi mahakama yao ina mamlaka ya mwisho. Wewe si umesoma sheria na sisi hatujui sheria, basi tunakwenda kutunga sheria na wewe utaitumia tu. Kidumu Chama Cha Mapinduzi."

Kauli hiyo ya Sendeka iliibua shangwe kutoka kwa wajumbe wa mkutano huo.

My take:

Kauli ya Sendeka kuwa yeye(Masaju) ni mwanasheria lakini wao(kina Sendeka) ni watunga sheria watatunga na Masaju lazima ataitumia tu inaacha maswali mengi badala ya majibu kuwa wakati wa kujadili muswada huu kutakuwa na mvutato mkubwa sana baina ya wabunge wa pande zote.
 
Watu wanaonyeshana ubabe, zaidi kwa maana ya kuonyesha powers alizo nazo, na si kwa maslahi ya waliowatuma kwenye huo mkutano!

Just as a reminder, ..Hivi huyu Sendeka hakuwepo kwenye semina Elekezi ya Dodoma eeh?...otherwise asingetamka kauli nzito namna hiyo (ya maslahi ya Taifa)kwa kujiamulia peke yake...Unless kama kuna jungu la siri linapita kichinichini!
 
Wangapi wanaitaka Tanganyika?

Kama wapo nani kawanyima?

Hivi kudai Tanganyika kwasababu eti Zanzibar imepewa madaraka zaidi kikatiba ni akili au tope?

Tudai Tanganyika kwakuwa ikiwa tuna sababu za msingi bila kuwanyima haki ya msingi wazanzibar waishi wapendavyo...
 
Wangapi wanaitaka Tanganyika?

Kama wapo nani kawanyima?

Hivi kudai Tanganyika kwasababu eti Zanzibar imepewa madaraka zaidi kikatiba ni akili au tope?

Tudai Tanganyika kwakuwa ikiwa tuna sababu za msingi bila kuwanyima haki ya msingi wazanzibar waishi wapendavyo...

Hapa hatudai Tanganyika, tunataka muungano uvunjwe
 
tena napendekeza nchi yangu ya tanganyika ifahamike kikatiba kama jamuhuri ya kidemokrasia ya watu wa tanganyika " Peoples democratic Republic of Tanganyika-PDRT" na sie wananchii tuishio ndani ya tanganyika kama raia tuitwe TANGANYIKANS...ahahaha VIVA TANGANYIKAAA VIVA AFRIKA VIVA NYERERE....am sorry nilikuwa naota ndoto MUNGA atanijaalia iwe kweli siku moja
 
Hapa hatudai Tanganyika, tunataka muungano uvunjwe

tangu nimejiunga humu jukwaani leo ndio nimekubaliana na post yako!
Nakubaliana na wewe kwa 100%. Ninachotaka ni muungano uvunjwe. Mengine yatakuja yenyewe!
 
hoja ya utanganyika, uzanzibari na utanzania tunaweza iweka kapuni for some time, kwani inapoteza dira na malengo ya mtanzania wa chini kabisa ambaye mahitaji yake muhimu ni chakula, mavazi, elimu, mahala pa kulala n.k. matatizo ni mengi sana tz yetu hii, hatuwezi fanya kila kitu ni priority, nadhani tungekomaa na mambo machache then mengine yatakuja baadaye, hapa ufisadi, hapa katiba mpya, hapa kilimo kwanza hakitekelezeki, hapa elimu duni, hapa uongozi mbaya, hapa kila kila kitu. yani ambacho si kizuri ndio kipo hapa. muda umefika wananchi tuamue priority ni nini kwetu na tuanze mapigano hadi kieleweke..
 
Mwanzo wa G55 nyingine?

MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, wamezozana hadharani wakipishana maneno kuhusu Muswada wa Mabadiliko ya Katiba. Mzozo huo ulizuka juzi kwenye mkutano wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (Alat) uliofanyika Kunduchi, Dar es Salaam juu ya mada ya Mabadiliko ya Katiba.

Baada ya Masaju kumaliza kuelezea madhumuni ya muswada huo, Sendeka alisimama na kuhoji kuhusu kauli iliyotolewa awali kwenye mkutano huo na Waziri Kombani kuwa, moja ya sababu za kuandikwa kwa Katiba mpya ni mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar iliyounda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Sendeka alisema mabadiliko hayo yameifanya Zanzibar kuwa nchi kamili, hivyo ni muhimu sasa kwa Watanganyika nao wadai serikali yao. "Waziri amesema moja kati ya mambo yaliyosababisha mabadiliko ya Katiba, ni mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar. Mabadiliko yale yameifanya Zanzibar kuwa nchi kamili. Na sisi tudai Serikali ya Tanganyika. Mwambieni Rais (Jakaya) Kikwete hivyo," alisema Sendeka.

Hata hivyo, wakati wa kujibu maswali, Masaju alisema Zanzibar siyo nchi kwa maana ya dola, bali ni kwa maana ya mipaka.
"Siyo kweli kwamba Zanzibar ni nchi kwa maana ya dola, bali ni nchi kutokana na mipaka yake," alisema Masaju kwa hasira huku akinukuu baadhi ya vifungu vya Katiba ya Zanzibar na kuongeza:"Someni Katiba ya Zanzibar na hati za muungano."

Baada ya Masaju kukaa, Sendeka alisimama tena na kusema: "Sawa, yaani unatujibu kwa hasira hivyo? Katiba ya Zanzibar imetoa madaraka makubwa. Zamani kwa kesi za Mahakama ya Rufaa walikuwa wakija huku (Tanzania Bara), lakini siku hizi mahakama yao ina mamlaka ya mwisho. Wewe si umesoma sheria na sisi hatujui sheria, basi tunakwenda kutunga sheria na wewe utaitumia tu. Kidumu Chama Cha Mapinduzi."

Kauli hiyo ya Sendeka iliibua shangwe kutoka kwa wajumbe wa mkutano huo.

My take:

Kauli ya Sendeka kuwa yeye(Masaju) ni mwanasheria lakini wao(kina Sendeka) ni watunga sheria watatunga na Masaju lazima ataitumia tu inaacha maswali mengi badala ya majibu kuwa wakati wa kujadili muswada huu kutakuwa na mvutato mkubwa sana baina ya wabunge wa pande zote.

hahaa!

ivi unajua uwa najiulizaga kila nikitizama vituko, midomo na sharubu za sendeka.

ivi atumii majani kweli?
 
Watu wanaonyeshana ubabe, zaidi kwa maana ya kuonyesha powers alizo nazo, na si kwa maslahi ya waliowatuma kwenye huo mkutano!

Just as a reminder, ..Hivi huyu Sendeka hakuwepo kwenye semina Elekezi ya Dodoma eeh?...otherwise asingetamka kauli nzito namna hiyo (ya maslahi ya Taifa)kwa kujiamulia peke yake...Unless kama kuna jungu la siri linapita kichinichini!

vyovyote vile! Iwe kuna jungu au hakuna, liwe kichini chini au kijuu juu, tunachokitaka kwa sasa ni serikali yetu ya Jamuhuri ya Tanganyika! Thats all and not otherwise. Afadhali Sendeka amefufuka.
 
Kama ndoa ya mke na mume huwa inavunjika, ndio ije kuwa muungano? tunataka muungano uvunjwe na sio vinginevyo.
 
hahaa!

ivi unajua uwa najiulizaga kila nikitizama vituko, midomo na sharubu za sendeka.

ivi atumii majani kweli?

anapiga jani live!!!! si unaona mdomo ulivoungua kaka ...kijiti cha arusha kile kikali acha kabisa
 
..Hivi huyu Sendeka hakuwepo kwenye semina Elekezi ya Dodoma eeh?...
Mkuu, huyu hakuwepo kule. Lakini hata wale ambao walikuwepo, wapo baadhi ambao hawawezi kukubaliana na upuuzi ingawa wamelazimishwa hivyo kwa dhana ya collective responsibility. Hii nyumba serikali na CCM imeshawaangukia, wanachoweza kukifanya hivi sasa si kushika paa na kuta zisianguke, waangalie jinsi watakavyojiokoa kutoka kwenye jumba bovu wasije wakafia humo. And if you ask me, wanatakiwa ku-think outside the box... wajue kwua maisha yapo hata kule ambako wao hawapo
 
nashangaa kupeleka mswada uliokataliwa na kila mdau ili ujadiliwe na wadau!! Hivi tuna akili kweli!!.
 
Back
Top Bottom