Kwangu mimi maisha ya ndoa ni tofauti na maisha ya kawaida. Sina uhuru tena niliokuwa nao kabla. Nimepoteza haki ya kufanya maamuzi peke yangu. Nimepoteza uhuru wa kubaki ofisini mpaka saa nne usiku. Kupigiwa au kupiga simu saa nne, tano usiku nakatazwa. Sili tena kwa mama ntilie. Hapa nipo jf na mwenzangu kanilalia.
Ila nafurahi sana. Mwili umerudi. Napata mda mwingi wa kufikiria maendeleo badala ya kufikiria nakula nini.