Ni kuzuia usilale. Inapanua mishipa ya damu na inaufanya moyo kusukuma damu kwa wingi hivyo mtu unajisikia una nguvu kwa muda. Vijana wa kisasa hunywa hizi drinks wakipaka vumbi lao la Kongo ili eti wapige show za kibabe!
Ukiwa addicted hii hali ya kuwa alert na nguvu ikiisha inabidi unywe tena na tena; tena kwa wingi zaidi. Matumizi yake kwa muda mrefu hatimaye huweza kuleta matatizo ya moyo, presha na hata kisukari. Wengine pia huharibu hata figo japo haijajulikana ni kwa nini hasa.
Marekani na sehemu zingine duniani energy drinks zote zimeanza kuwekewa warning ili watu wazitumie kwa uangalifu.