Mbunge wa jimbo la Nzega na mmoja kati ya wale walioitwa wapambanaji wa ufisadi Lucas Lumambo Selelii kesho saa nane mchana atahutubia wakazi wa mji wa Nzega kuonyeshwa kufurahishwa kwake na kitendo cha ujasili cha aliyekuwa mpambanaji mwenzie wa ufisadi na mbunge wa kishapu mpendazoe cha kujitoa CCm na kuhamia CCj akisema kitendo hicho hakipaswi kupita bila kupongezwa.
Selelii aliyasema hayo mara baada ya mkutano wa kumsimika kamanda wa vijana wa nzega Ndg mbozu kijijini kwa ke Isanzu! akiwa amezungungukwa na baadhi ya wasaidizi wake akiwemo katibu wake ambaye pia ni katibu mwenezi wa nzega bwana Mayunga Selelii alisema" najua kuna watu watataka kujua nini msimamo wangu juu ya alichokifanya Mpendazoe nasema hivi yule bwana Mwanaume, haogopi cha nini wala nini na zaidi ametumia haki yake ya kikatiba na kesho nitakuwa na mkutano mkuwa wa kutangaza nia yangu ya kugombea tena jimbo la nzega lakini muda ukiruhusu sitasita kumzungumzia mwanaume wa Mbegu Mpendazoe"
Mkutano huo ambao utafanyika katika viwanja vya "Parking Nzega' utahudhuriwa na wana CCM kadha wa jimbo la nzega ambao Selelii hakutaka kuwataja zaidi ya kusema utakuwa mkutano wa kihistoria!
Nitawajuza kila litalojiri kwani nitakuwepo Nzega.
Selelii aliyasema hayo mara baada ya mkutano wa kumsimika kamanda wa vijana wa nzega Ndg mbozu kijijini kwa ke Isanzu! akiwa amezungungukwa na baadhi ya wasaidizi wake akiwemo katibu wake ambaye pia ni katibu mwenezi wa nzega bwana Mayunga Selelii alisema" najua kuna watu watataka kujua nini msimamo wangu juu ya alichokifanya Mpendazoe nasema hivi yule bwana Mwanaume, haogopi cha nini wala nini na zaidi ametumia haki yake ya kikatiba na kesho nitakuwa na mkutano mkuwa wa kutangaza nia yangu ya kugombea tena jimbo la nzega lakini muda ukiruhusu sitasita kumzungumzia mwanaume wa Mbegu Mpendazoe"
Mkutano huo ambao utafanyika katika viwanja vya "Parking Nzega' utahudhuriwa na wana CCM kadha wa jimbo la nzega ambao Selelii hakutaka kuwataja zaidi ya kusema utakuwa mkutano wa kihistoria!
Nitawajuza kila litalojiri kwani nitakuwepo Nzega.