Selcom vs Max Malipo

Selcom vs Max Malipo

Mkali_01

Senior Member
Joined
May 13, 2015
Posts
166
Reaction score
117
Habari wadau. Naomba niulize kati ya kampuni hizi mbili yaani Selcom na Max malipo, ni ipi ina commission nzuri katika miamala yake? Na je zote zinafanya kazi sawa au kuna moja inazidi mwenzake?
 
Bora ukauze karanga kuliko kuwatumia hao watu
 
Nimepata taarifa zao. Mfano ukiuza umeme wa sh. 100,000 faida ni 2,500 tu.
 
Niliwahi kufanya hiyo biashara nilikuwa na mashine ya selcom, baada ya miezi miwili ikabidi niiweke nyumbani hiyo mashine kama pambo nikachange biashara, yaani hao wote hamna kitu hakuna cha afadhali, yaani unakuwa kama msukule unayanufaisha makampuni ila wewe unachopata ni kichekesho
 
Tatizo watu hawapendi kupata taarifa sahihi kabla ya kuingia kwenye biashara.

iko hivi biashara ya commision bases inafaida ndogo sana kutokana na nature yake ilivyo kwani imekaa kihuduma zaidi na ina middle mens kadhaa kabla ya kumfikia mlaji.

Hivyo basi ni vema unayetaka kufanya biashara hii ukautazama kwa jicho la kama ni bidhaa ndani ya biashara nyingine mfano una duka la kuuza vyakula zaidi ya bidhaa nyingine unazouza weka hiyo maxmalipo? tigo pesa, mpesa, airtel money,mashine ya beeting na wakala wa bank kama equty nakadhalika hapo itaifurahia hiyo biashara.

Mfano mimi binafsi ndivyo ni biashara ya stationery natoa huduma hizo pamoja na uwakala wa equity bank nikichanganya commision zote kwa mwezi hazipungui 600,000 faida kwa mwezi nikijumlisha na mauzo ya stationery najikuta pato langu kwa mwezi ni around 1m. hivi.

Changamoto inahitaji mtaji wa kutosha ili upate faida hiyo pili risk upotevu wa hela na wizi ni tatizo.
 
Asante mkuu. You have a positive attitude
 
Unapotaka kufanya biashara lazima ufanye uchambuzi wa UMAFUTI
. Mambo yaliyo ndani ya biashara

Uwezo
Mapungufu
Fursa
Tishio
 
Back
Top Bottom