Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
16,310
Reaction score
33,784
UPOTOSHAJI KUHUSU KILICHOJIRI SCOTLAND

KURA NI ‘NO' MABADILIKO NI ‘YES'

UK KUBADILI MUUNDO WA MUUNGANO

TANZANIA, ULAGHAI, UBABAISHAJI NA UHUNI


Wanajamvi, Niwatake radhi kwa mabandiko marefu
Nyakati tulizo nazo haziruhusu kuacha vitu hewani
Wababaishaji, wapotoshaji na mashabiki hutumi mwanya huo kwa azama zao

Tangu matokeo ya kura ya maoni Scotland kutolewa, yamekuwepo maelezo ya kupotosha wananchi kwa kuficha ukweli wa kilichotokea

Kura ya maoni ya Uingereza imekuwa kielelezo cha mabadiliko katika tawala za dunia. Imechukuliwa kama kipimo ''yard stick''

Mfan, kuna nchi zinaiangalia Scotland kama mfano, Tanzania ikiwemo

  1. Spain na Catalonia
  2. Denmark na Feroe Island
  3. Italia na Vaneto

Historia ya Uingereza ni ndefu, ikihusisha mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, muungano wa falme na mabadiliko yaliyofuata.

Hatutaweza kueleza kwa ukamilifu, tutachukua ya muhimu kwa ufahamu tu,wakati huu mazingira yetu yanapowiana na yaliyotokea.

Tuifahamu Uingereza kwa uchache.

Hili ni taifa kubwa lililomiliki makoloni mengi na hadi sasa.
Idadi ya watu ni Milioni 64, ikiwa na uchumi namba 6 duniani

Uingereza ni muungano wa falme kutoka nchi za England na Wale na Scotland zinazotengeneza Great Britain na North Ireland.

Muungano ni wa takribani miaka 300, ukiwa umepitia hatua za mageuzi na mabadiliko. Uingereza haina katiba, hutawali kwa constitutional monarchy.

Mfumo unaotawala ni Unitary system,serikali kuu yenye mamlaka.
Mfumo wao hujulikana kama Westminster

Pamoja na ufalme, Uingereza inaendeshwa kidemokrasia kwa mabunge 2(bicameral).

Bunge la Makabwela (House of common) na bunge la Mamwinyi(House of lords)

Unitary system huongoza nchi kama kituo kimoja(single unit), serikali kuu ikiwa imeshika hatamu

Mfumo wa Unitary unatumika na nchi nyingi duniani, nao pia umegawanyika

Uingereza ina Monarch unitary system malikia akiwa na mamlaka makuu.

Bunge la Mamwinyi limepunguziwa nguvu na sasa hudurusu sharia zitokazo katika bunge la Makabwela(House of Common) na kasha kuridhiwa na Malikia

Uteuzi wa house of lords hufanywa na malikia kwa ushauri wa waziri mkuu, au kamisheni maalumu inayomshauri malikia.

Mtindo wa uteuzi kwa urithi ‘herditary' umeondelewa.
Mageuzi hayo yalianzishwa na chama cha Labor wakati wa Tonny Blair

Kuna nchi zenye mfumo wa Unitary kama Uingereza, nyingine hufuata mfumo huo kama Repulic na hapa zipo nchi nyingi za common wealth ikiwemo Tanzania

Tofauti na unitary,mfumo wa confederation una malengo maalumu kama ulinzi ukiacha mamlaka kwa nchi husika, wakati Federal ni shirikisho litoalo mamlaka kwa washirika

Devolution ni mfumo unaotoa mamlaka kwa maeneo kama mikoa, serikali za mitaa au vinchi washirika kwa maana ya decentralization.

Hata hivyo serikali kuu inabaki kuwa na nguvu za kupangua sharia katika ngazi za chini.

Federalism ni mfumo ambao nguvu za washirika zipo kikatiba, na hapa tunasisitiza

Inaendelea…….

cc MwanaDiwani Nape Nnauye Alinda Mag3 Anna Tibaijuka HKigwangalla Dr.F.Ndugulile John Mnyika Remote JokaKuu gfsonwin Mwalimu Bongolander Kichuguu Buchanan Mwigulu Nchemba AshaDii Paul Makonda Gwalihenzi Kichuguu Ritz EMT MJINI CHAI Pasco Mkandara Mchambuzi MNYISANZU mohamed Mtoi Ogah Kimweri
 
Last edited by a moderator:
UINGEREZA

Nchi ya England( makao makuu London) iliungana na Wales(Cardiff) kwanza katika miaka ya 1200, kisha zikaungana na Scotland(Edinburg) na Ireland
Great Britain inahusisha nchi tatu, England, Wales na Scotland.

Mwaka 1922 Ireland ilijitenga kukatokea Republic of Ireland and Northern Ireland
Northern Ireland ikabaki ndani ya Uingereza.

Hivyo kwa ufasaha Uingereza inaitwa the The Great Britain and Ireland

Muungano wa awali ulikuwa wa falme tatu, England, Scotland na Wales 1707 kisha Ireland miaka ya 1800.

Katika nchi nne, tatu zimepewa mamlaka ya kuendesha mabunge yao wakiwa na viongozi kama First minister n.k.

Tusema kwa uchache kuwa tangu Northern Ireland ijitenge kutoka Ireland mwaka 1921, kumekuwa na misuguano inayoendelea

Waziri mkuu wa UK ni mmoja tu ndani ya bunge la Uingereza.

Kutokana na maadiliko ya kimadaraka, kuongeza au kupunguza nguvu, bunge la Westminster linabaki kushughulikia sehemu mahusiano ya kimataifa.

Nguvu za mambo yanayohusu wananchi zimeachwa kwa bodies zilizopewa madaraka kwa mfumo wa devolution

Hili limeleta sintofahamu miongoni mwa wabunge hasa wa Scotland na Ireland wanaohisi, kutumikia mfumo wa serikali kuu kunawatenga na wananchi katika maisha ya kawaida.

Kwa mfano, shughuli na huduma zimepewa bodi za maeneo kwa kile kilichoitwa devolution na wabunge kbaki katika mijadala ya kimataifa

Kwasasa Uingereza inaelekea katika mfumo wa Quasi federalism.
Maana yake,kuna mfumo wa shirikisho katika mfumo wa umoja (Unitary system).

Tumeeleza hapo juu kuhusu unitary system na kadri tulivyosonga mbele tumeona federalism kiaina na hicho ndicho kinachoitwa Quasi federalism.

Inaendelea…..
 
TAMADUNI,TARATIBU NA MAJINA

Pamoja na Uingereza kuwa nchi moja,nchi washirika hazikupoteza utamaduni au majina . Hadi leo tunajua England , Scotland, Wales na Northen Ireland kama zilizvyokuwa

Muungano wa UK wenye miaka Zaidi ya 300, haukupoteza utaifa wa eneo lolote wala utamaduni wake, na wala hakuna hatia au kosa kujiita walesh, scotch, au English

SCOTLAND
Mzozo wa kujitenga ni mrefu, lakini mageuzi hasa yametokea miaka 1997 na kuendelea ambako Tonny Blair alianzisha mabadiliko katika maeneo kadhaa ya tawala.

Kujitenga kwa Glasgow kumechagizwa zaidi na rasilimali za mafuta, wakitamani wawe kama nchi za Norway na Sweden. Idadi ya raia wake ni milioni 5+.

Na pengine ni mfano wa Zanzibar baada ya fununu za uwepo wamadebe 30 ya mafuta

Kutokana na mazoea na muungano wa muda mrefu yametokea makundi mawili, moja kikitaka libaki ndani ya muungano(Unionist) na jingine lijitoe(Nationalist)

WESTMINSTER WAKALIONA TATIZO

Bunge la Uingereza likaanzisha mchakato wa Scotland kuamua kama inabaki ndani ya Uingereza au inatoka. Ni mchakato huo ndio uliozaa kura ya maoni.

Hapa halikuwa suala la muundo wa nchi, kilichokuwepo ni ima kuwepo au kutoka katika muungano wa Uingereza.

SCOTLAND WAGAWANYIKA

Wapo walioamini umoja ni nguvu na kwamba Scot ni imara ndani ya himaya ya malikia.

Wapo waliodhani ni bora kujiondoa ili kujitawala, hata hivyo walitaka kubaki na passport ya Uingereza na pesa za malkia(Pound).

Nchi washirika zikatoa kauli kuwa Scotland wakijitoa basi iwe jumla hakuna nusu nusu.

Pengine nao walifikiria kuwa na muungano wa mkataba kwa hofu ile ile ya kuwa nje ya taifa kubwa, kiulinzi na kiuchumi.

Hili liliChagiza sana kupunguza idadi ya wanaotaka kujitoa kwa hofu ya kuwa na taifa linalojitgemea ambalo nguvu zake kiuchumi na kijeshi hazijulikani uzani wake.

Inaendelea….
 
KURA YA MAONI

Matoke ya Yes, wale wanaotaka kubaki ikawa ni aslimia 55 na wale wanaotaka kujiondoa asilimia 45, hivyo wanaotaka kubaki ndani ya Uingereza wameshinda.

Bila kujali itikadi za kisiasa, vyama vyote vikuu vilisimama katika utaifa.

Utaifa si kutetea muungano, bali ukweli. Vyama vimeeleza haja ya kuwa na maridhiano ya kitaifa, kukaa pamoja na kutafuta suluhu ya matatizo kwa haki na usawa

CAMERON AELEZA UKWELI

Waziri mkuu alitoa hotuba baada ya matokeo.

Hotuba yake ilijaa uzalendo, ukweli na maono ya siku za baadaye.

Cameron hakuwapendeza Wascot wala kuwanyanyasa England, Wales na Ireland

Sikiliza hapa


(Ikihitajika tafsiri tutaiweka rasmi)
Scottish Independence: How David Cameron Will Tackle The Awkward Issue Of Constitutional Change

Alichokisema ni kuwa ahadi walizoto scotland watazifanyia kazi.

Hata hivyo ni muhimu pia kufanya vivyo hivyo kwa washirika waliobaki.

Waziri mkuu ameona hatari ya upendeleo kwa upande mmoja.

Hofu yake ni siku moja England, Wales na Ireland nao kudai haki zaidi za kujitawala kama Scotalnd. Na pengine uwezekano wa washirika 3 kumuondoa Scotland ukatokea

CHANGAMOTO ZA EU ZINATISHIA UINGEREZA ZAIDI

Scotland wamepewa mamlaka zaidi ya washirika wenzao

Wakati washirika wakitarajia kupewa haki yao, Uingereza ina changamoto nyingine. Kura kuhusu kujitoa EU ipo mbioni.

Scotland kwa mamlaka yao wanaweza kutaka kubaki, Uingereza kuondoka au kinyume chake. Hilo litazua sintofahamu zaidi na haijulikani muafaka utakuwaje.

Hali hiyo ni sawa na Tanzania ambapo Zanzibar inapewa mamlaka zaidi.

Tunakoelekea EAC znz imedai ushiriki tofauti na Tanzania.

Swali linakuja tunawezaje kuondoa sintofahamu hiyo katika Unitary system inayoboreshwa? S2 Maboresho?

Inaendelea……
 
HOJA POTOFU ZA WATANZANIA
Kwamba, Scotaland imemua kubaki katika muungano.
Ukweli ni kuwa imeabaki kwa masharti ya kutimiziwa madai yao ikiwa ni kuwapa mamlaka kamili.

Mamlaka hayo ndiyo yatabadili muundo wa muungano wa Uingereza kutoka
Unitary system kwenda quasi federalism na kuelekea katika federation kamili

Kwa Tanzania, wazanzibar naWatanganyika hawajakataa muungano.
Wanacholitaka ni kuwa na mfumo kutoka ‘pseudo unitary' kwenda katika federation.

Madai ya S3 hayana maana kuvunja muungano kama inavyopotoshwa, bali kubadili mfumo kama alivyosema David Cameron ili kuleta utengamano

Cameron kasema baada ya kushughulikia madai ya Scotland, ni wakati wa kushughulikia ya washirika.

Tanzania badala ya kufikiria hilo, imejikita kuwafurahisha wazanzibar na kuudhi Watanganyika. Hilo litavunja muungano tukizingatia kuwa sisi ni nchi mbili.

Uingereza ni nchi nne hivyo kutoa nafasi ya majadiliano.
Sisi ni suala la Tanganyika kuamua tu na muungano unakoma.

Kuna upotoshaji kuwa muungano maana yake ni kuua utaifa.
Kama ilivyoua Tanganyika na tamaduni zake hilo halipo Uingereza.

Na hapa ndipo pa kujiuliza kwanini Uingereza tulikoiga mfumo bado kuna England, Wales, Scotland na Ireland zikiwa na majina, taratibu na tamaduni zao?
Kwanini Tanganyika ifutike na si England,Wales au Ireland?

Tumeona upotofu kuhusu S2 maboresho.
Ukweli tuliouona na unaoendelea duniani ni nchi kutoka katika Unitary system kwenda Federation.

Tumetaja nchi zinazoelekea huko. Hii S2 ni kuaminisha watu tunatoka katika weak Unitary system kwenda katika strong unitary system.
Swali, ni wapi hilo limetokea duniani

Kwamba kunahitajika kura ya maoni Tanzania. Hilo lina mantiki, lakini swali la kujiuliza ni nani dhidi ya nani. Tanganyika haipo izingatiwe.

Waziri mkuu wa Tz aliwahi kusema angalijua kura ya maoni ingetangulia, kwanini sasa hivi hawawaulizi Wazanzibar wanendelea na maboresho Dodoma?
Kwanini Wanaogopa Tanganyika kuzinduka, na ni nani atajadiliana na znz

Kwanini mabadiliko ya muundo Tanzania yapotoshwe ni kuvunja muungano.
Uingereza inabadilika, je, ina maana wanavunja muungano wao?
Kwanini iwe Tanganyika kuvunja muungano na si UK inayobadili mfumo?

S2 maboresho zinatokana na maoni yapi ya wananchi?
Kwanini Westminster haikujadili na kufikia tamati, ilibidi watu waulizwe?

Je, tume ya Warioba ilifanya kipi tofauti na hiki kilichofanywa Uingereza?
Na kwanini tuone Waingereza wamefanikiwa na siyo sisi kutengeneza mazingira ya kufanikiwa tukiwa taifa huru?

Kwanini Scotland walioungana miaka 300 wasiogope kuoleana, leo tutishwe muungano wetu umeweka kwa kuoa au kuoleana?
Nguvu ya hoja kuoa au kuoleana inatoka wapi kwa kuangalia UK na yaliyotokea?

Je, kampeni za kulinda muungano , zimeenda samba mba na kutoa autonomy kwa both constituents au zimelenga kudanganya na kufunika matatizo ya pande husika



Inaendelea……

 
TUMEJIUFUNZA NINI
Kwamba;
-Hakuna mfumo duniani uliotoka katika federal kwenda unitary bali kinyume chake.

-wananchi wasikilizwe na wapewe haki ya kuamua hatima za mataifa

-Mageuzi ni matakwa ya wananchi , hayakwepeki kwa ulaghai au ubabaishaji

-Muungano hauna maana ya kuua tamaduni au utaifa wa washirika

-Mabadiliko hayana maana kuua muungano, ni hatua muhimu ya kuimarisha

-Mageuzi ni kitu endelevu na hakizuiliki

-Uingereza inaelekea katika mfumo wa shirikisho kutokana na nyakati

-Tatizo halimalizwi kwa kuangali, udanganyifu au ubabaishaji.

-Muungano unaweza kubaki katika miundo tofauti, kudai mabadiliko si kuvunja muunagano bali kuimarisha ili kukidhi mabadiliko ya dunia

-Tatizo letu si muungano au muundo, ni kukokesekana kwa viongozi, waadilifu, wakweli, wanaosimamia utaifa na wenye maono ya taifa hili

-Matatizo yanakabiliwa, hayaishi kwa viongozi kuyafukia katika kapeti au kuyakimbia kwa kisingizio cha kumaliza muda.

Inaendelea……



 
HITIMISHO

Kura ya Scotland itazaa mfumo na mabadiliko UK.
Wananchi wamesikilizwa na hoja kuzingatiwa
Wachache wamezingatiwa wengi wameamua

Matakwa yamezingatiwa kwa uwiano,usawa na kipaumbele kujenga misingi imara

Mabadiliko ya uchumi na siasa za dunia yanagusa na kubadili jinsi tunavyoishi.

Miaka 300,UK imetikiswa, ni ujinga kudhani mataifa madogo yatahimili vishindo.

UK wameangalia masilahi ya vizazi vijavyo kuishi kwa utangamano

Siasa za vyama ziliwekwa pembeni, utaifa ukatamalaki.

Waziri mkuu ameongea dakika 7 kama kiongozi wa taifa.

Hakubabaisha, kulaghai, kubadilika au kuyumbisha wananchi.
Hotuba ni nzito iliyoangaliwa duniani na kusifiwa na vyombo vya habari

Wenzetu wanafanikiwa kukaa mezani kwa mustakabali wa taifa

Cameron hakusubiri aondoke madarakani,aache mzigo kwa mrithi wake.

Si kwa siasa za kipuuzi, uchama au utaifa.
Hatuwezi kubaki kama tulivyo, mabadiliko yanatulazimisha tubadilike.

Kwetu, mfumo wa utawala na muundo wa nchi umeshindwa kukidhi kwa miaka 50.

Kuendelea kung'ang'ania ni kujidanganya na kutega bomu kwa vizazi vijavyo.

Muundo wa muungano ni maridhiano si kanuni za bunge au uchama wa wabunge.

Tukimiskiliza Camaeron, tunaona fahari ya kuwa na viongozi mwenye maono.
Tunajiuliza, Waafrika tuna laana gani?

Republic of Ireland (siyo Northen Ireland) ilijitoa katika muungano kwa kunyimwa autonomy, je yunasubiri hilo litokee ndipo tukurupuke kukiwa kumekucha tayari

Miaka 50 ya kujitawala hatuwezi kujivunia viongozi wetu wenyewe.

Ile thamani ya Tanzania iliyojijengea sasa imeyeyuka.

Hatuna watu wa kutuweka pamoja kama taifa. Tunakwenda kama nguruwe mwituni.

Hili la kuua Tanganyika yenye urithi wake na kupendelea Zanzibar si suluhisho.

Na wala picha ya Karume katika coin ya sh 500 haitamaliza tatizo, ni suluhu za wapumbavu na wehu tu.

Uhuni unaoendelea Dodoma ni hatari kwa taifa.

Ipo siku tutamsikiliza Cameron akihutubia taifa lake,tukiuguza madonda,tukizika

Hatuhitaji mtabiri au Nabii, huko ndiko tuendako.

David Cameron atazaliwa lini Tanzania ili tutoke kwenye mkwamo wa fikra, upuuzi, uzezeta, uchumia tumbo na ujuha?

Kwanini Cameron asijifunze kwetu eti tujifunze kutoka kwake.
Ukoloni utaisha lini akilini mwetu.

Je, tunamsubiri Cameron atuletee wanafunzi wa chuo kujadili katiba ya nchi yetu kwasababu tu viongozi wetu wanasema '' kazi itamalizika wakiondoka madarakani?

Ahsanteni

 
Naunga mkono hoja ya Nguruvi3 kwamba - hatua ya wananchi wa Scotland kupiga kura ya "HAPANA "Kujitoa katika Muungano wao, haimaanishi kwamba hii ni kura ya HAPANA kwa "Mabadiliko" ndani ya muungano wao. Kura ya hapana imekuja baada ya wananchi wa Scotland kupewa ahadi zaidi juu ya ‘devolution'. Wananchi hawakuwa na sababu za kutuamini ahadi hizi kwani kama ilivyojadiliwa huko juu, wananchi tayari waliona juhudi hizi zaidi ya mika kumi iliyopita, tena chini ya utawala wa chama ambacho leo ni cha upinzani (Labor party under Tony Blair 1997-2010). Ni katika hali hii, nguruvi3 amejadili juu ya umuhimu wa viongozi kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko ya vyama katika mambo kama haya, sio kama sisi ambapo kiongozi wa nchi anaenda kufungua bunge la katiba kwa kuweka bayana msimamo wa chama chake.

Kwa wenzetu UK, hata katika election manifestos za vyama vilivyounda coalition government iliyopo sasa, vyama vyote hivi vilikuwa na msimamo mmoja na usio yumba juu ya umuhimu wa "devolution" ndani ya muungano wa nchi yao (UK). Ni aina hii ya uongozi ndio umesaidia kuwaleta wananchi pamoja kuliko kuwagawanya, hivyo kufanya kila mwananchi kujiona kama ana wajibu mkubwa wa kuwa ‘mlinzi wa muungano'. Bila ya kujalisha itikadi za vyama, vongozi wa UK wamefanikiwa kuwafanya wananchi wao kuwa "United in Diversity", suala ambalo viongozi wetu wameshindwa. Kwetu sisi, 50 years later, we are more of a ‘disunited republic of Tanzania', and less of a united republic.

Kama alivyojadili mleta mada, ni muhimu sana kwa wanasiasa wetu wakaelewa haya badala ya kuanza kupotosha umma aidha kwa kujua au kutokujua KWANINI wananchi wa Scotland wamesema HAPANA ‘kujitenga'. Kura ya Scotland maana yake ni kwamba they are less interested in ‘SEPARATION', and instead, they are more interested in ‘DEVOLUTION'. That's the bottom line. Kwa maana nyingine, wanachotaka wananchi wa Scotland, na ambacho watakipata ni pamoja na:


  • Uhuru wa kikatiba juu ya kujiamulia sera zao za kiuchumi na maendelo.
  • Uhuru wa kikatiba juu ya kutumia mapato yao ili kufanikisha malengo yao ya kiuchumi na maendeleo.

Kama alivyogusia nguruvi3, wananchi wa – Feroe Island, Catalonia, Vaneto, and increasingly even Tanganyika (or ‘Tanzania Bara', that's if you prefer it that way), wote hawa hawana vilio tofauti na Scotland. Wanacho hoji ni - the stream of financial transfers baina ya washirika wa muungano kwa sababu; wananchi hawa wanaona kwamba kuna upande au pande ambazo zina ‘drain' their financial resources, kwahiyo wanataka mabadiliko makubwa in the distribution of financial and fiscal competencies. Kwa maana nyingine, kinachopiganiwa na wananchi hawa ni ‘fiscal autonomy' yani – freedom to determine one's own taxes and budgets based on competencies and self determined priorities, tastes and preferences. Basi!

Benefits hizi zinakuja na mfumo wa shirikisho (federalism), sio unitary systems. Ndio maana watu wengi duniani wanazidi kuvutiwa na pia kupenda zaidi kuishi ndani ya mfumo wa federalism kuliko unitary system. Isitoshe, leo nusu ya idadi yote ya watu duniani wanaishi chini ya federalism, NOT unitary system. Hata CHINA, this nation has become a de facto federation by devolving more and more autonomy kwa majimbo yake, huku pia ikitoa guarantee kwa Hong Kong semi-independent status as an autonomous region. Yote haya yanatueleza kitu kimoja cha msingi, nacho ni kwamba:
Watu wengi duniani wanazidi kuelimika kwamba - federalism inawa wezesha kupata "The Best of Both Worlds" kwa maana ya kupata faida za – SHARED RULE (National Government) and SELF RULE (sub national government), kwa wakati mmoja. Wengi duniani wanazidi kuvutiwa na federalism kwa sababu wanaona ‘prosperity', ‘stability and ‘longevity' ndani ya major democratic federations kama vile – USA, States, Canada, Australia, Switzerland, n.k. Hata mabadiliko makubwa ya kiuchumi nchini China ni matokeo ya taifa hili kuamua kuwa ‘a defacto federation' kwani wamegundua kwamba its federalism that bears prosperity and stability, not unitary system. Ndio maana, kama alivyojadili mleta mada, ‘no federation has ever changed to a unitary system', instead, it is unitary systems that have shifted towards federalism. Na kama kuna sehemu yoyote ile ambayo federation changed to unitary system, then it was a result of a totalitarian takeover, sio kwa matakwa ya wananchi, that's why such changes didn't sustain!

Iwapo wanasiasa wa Tanzania wangekuwa watafiti japo kidogo, badala ya kukaa na kusubiri kulishwa maneno au kusokomezwa matambara midomoni na CCM, wangesoma na kujifunza mengi, kwa mfano utafiti kwamba - kama Uingereza ingefuata mfumo wa shirikisho mapema kama walivyofanya wenzake katika karne ya ishirini, Jamhuri ya Ireland (hii ni tofauti na Ireland ya Kaskazini), isingejitoa UK. Lakini sio hivyo tu, pia United Kingdom isingekumbwa na ugaidi uliotishia kuisambaratisha UK baada ya mzozo wa muda mrefu baina ya Westminster na Ireland ya Kaskazini. Ni baada ya Westminster kukubaliana na Ireland ya kaskazini juu ya umuhimu wa devolution, amani ikapatikana. Pia, kura ya maoni ya Scotland ambayo ilitishia usalama wa taifa la UK pamoja na sekta yake ya biashara, haya yote yasingetokea iwapo UK ingeamua kuiga wenzake na kufuata mfumo wa shirikisho. Baada ya kujifunza makosa, leo UK is more of a federation than a unitary system.

Wanasiasa wetu wana haja ya kuelewa kwamba kabla ya utawala wa Labor party chini ya Tony Blair kuingia madarakani (1997), UK's unitary system was slowly disintegrating for over a century. Kwa mfano:


  1. It is because of the unitary system, violent struggle for home rule gained strength in the 1880s
  2. It is because of the unitary system, Ireland became independent in 1922.
  3. It is unitary system that led to Scottish and Welsh nationalism.
  4. It is unitary system that led to Civil war in Northern Ireland.

Baada ya kujifunza na kukubali mapungufu ya mfuko wa unitary, Serikali chini ya Tony Blair ikaamua kuchukua maamuzi magumu mwaka 1998, ambapo a ‘semi-federal' structure ikaanza kuwa implemented in the UK ili kukidhi mahitaji ya devolution for Scotland and Northern Ireland. Pamoja na juhudi hizi, wananchi wa Scotland bado hawakuridhika na mabadililo kwani bado- it was more like a self-governing colony arrangement, na kufikia kiwango cha kuwa na judicial appeals to the Privy Council katika masuala ya kikatiba. Hali hii ikaanza kuonyesha dalili za instability na kutishia muungano uliopo, ndio maana haukupita muda mrefu, wanasiasa wengi wa Uingereza bila ya kujalisha itikadi zao za vyama, wakaanza kuona kwamba ‘an independent Scotland' was a real possibility kupitia kura ya maoni, na hii ilikuwa miaka kumi iliyopita. Hata wale viongozi waliokuwa upinzani wakati ule (Conservatives), ambao awali they voted against devolution of scotland, wakaamua kuweka utaifa mbele na kuungana na Blair katika kuhakikisha kwamba muungano unadumishwa through more devolution. Hii ni kwa sababu viongozi hawa wapo kutumikia wananchi, sio vyama vyao vya siasa. Hii ni tofauti na kwetu ambapo kiongozi anaogopa/anakwepa kuongoza mabadiliko. Iwapo kiongozi anafikia hatua hiyo, ana sifa gani ya maana aliyobakia nayo kuitwa kiongozi?
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono hoja ya Nguruvi3 kwamba - hatua ya wananchi wa Scotland kupiga kura ya “HAPANA “Kujitoa katika Muungano wao, haimaanishi kwamba hii ni kura ya HAPANA kwa “Mabadiliko” ndani ya muungano wao. Kura ya hapana imekuja baada ya wananchi wa Scotland kupewa ahadi zaidi juu ya ‘devolution’. Wananchi hawakuwa na sababu za kutuamini ahadi hizi kwani kama ilivyojadiliwa huko juu, wananchi tayari waliona juhudi hizi zaidi ya mika kumi iliyopita, tena chini ya utawala wa chama ambacho leo ni cha upinzani (Labor party under Tony Blair 1997-2010). Ni katika hali hii, nguruvi3 amejadili juu ya umuhimu wa viongozi kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko ya vyama katika mambo kama haya, sio kama sisi ambapo kiongozi wa nchi anaenda kufungua bunge la katiba kwa kuweka bayana msimamo wa chama chake.

Kwa wenzetu UK, hata katika election manifestos za vyama vilivyounda coalition government iliyopo sasa, vyama vyote hivi vilikuwa na msimamo mmoja na usio yumba juu ya umuhimu wa “devolution” ndani ya muungano wa nchi yao (UK). Ni aina hii ya uongozi ndio umesaidia kuwaleta wananchi pamoja kuliko kuwagawanya, hivyo kufanya kila mwananchi kujiona kama ana wajibu mkubwa wa kuwa ‘mlinzi wa muungano’. Bila ya kujalisha itikadi za vyama, vongozi wa UK wamefanikiwa kuwafanya wananchi wao kuwa “United in Diversity”, suala ambalo viongozi wetu wameshindwa. Kwetu sisi, 50 years later, we are more of a ‘disunited republic of Tanzania’, and less of a united republic.

Kama alivyojadili mleta mada, ni muhimu sana kwa wanasiasa wetu wakaelewa haya badala ya kuanza kupotosha umma aidha kwa kujua au kutokujua KWANINI wananchi wa Scotland wamesema HAPANA ‘kujitenga’. Kura ya Scotland maana yake ni kwamba they are less interested in ‘SEPARATION’, and instead, they are more interested in ‘DEVOLUTION’. That’s the bottom line. Kwa maana nyingine, wanachotaka wananchi wa Scotland, na ambacho watakipata ni pamoja na:


  • Uhuru wa kikatiba juu ya kujiamulia sera zao za kiuchumi na maendelo.
  • Uhuru wa kikatiba juu ya kutumia mapato yao ili kufanikisha malengo yao ya kiuchumi na maendeleo.

Kama alivyogusia nguruvi3, wananchi wa – Feroe Island, Catalonia, Vaneto, and increasingly even Tanganyika (or ‘Tanzania Bara’, that’s if you prefer it that way), wote hawa hawana vilio tofauti na Scotland. Wanacho hoji ni - the stream of financial transfers baina ya washirika wa muungano kwa sababu; wananchi hawa wanaona kwamba kuna upande au pande ambazo zina ‘drain’ their financial resources, kwahiyo wanataka mabadiliko makubwa in the distribution of financial and fiscal competencies. Kwa maana nyingine, kinachopiganiwa na wananchi hawa ni ‘fiscal autonomy’ yani – freedom to determine one’s own taxes and budgets based on competencies and self determined priorities, tastes and preferences. Basi!

Benefits hizi zinakuja na mfumo wa shirikisho (federalism), sio unitary systems. Ndio maana watu wengi duniani wanazidi kuvutiwa na pia kupenda zaidi kuishi ndani ya mfumo wa federalism kuliko unitary system. Isitoshe, leo nusu ya idadi yote ya watu duniani wanaishi chini ya federalism, NOT unitary system. Hata CHINA, this nation has become a de facto federation by devolving more and more autonomy kwa majimbo yake, huku pia ikitoa guarantee kwa Hong Kong semi-independent status as an autonomous region. Yote haya yanatueleza kitu kimoja cha msingi, nacho ni kwamba:
Watu wengi duniani wanazidi kuelimika kwamba - federalism inawa wezesha kupata “The Best of Both Worlds” kwa maana ya kupata faida za – SHARED RULE (National Government) and SELF RULE (sub national government), kwa wakati mmoja. Wengi duniani wanazidi kuvutiwa na federalism kwa sababu wanaona ‘prosperity’, ‘stability and ‘longevity’ ndani ya major democratic federations kama vile – USA, States, Canada, Australia, Switzerland, n.k. Hata mabadiliko makubwa ya kiuchumi nchini China ni matokeo ya taifa hili kuamua kuwa ‘a defacto federation’ kwani wamegundua kwamba its federalism that bears prosperity and stability, not unitary system. Ndio maana, kama alivyojadili mleta mada, ‘no federation has ever changed to a unitary system’, instead, it is unitary systems that have shifted towards federalism. Na kama kuna sehemu yoyote ile ambayo federation changed to unitary system, then it was a result of a totalitarian takeover, sio kwa matakwa ya wananchi, that’s why such changes didn’t sustain!

Iwapo wanasiasa wa Tanzania wangekuwa watafiti japo kidogo, badala ya kukaa na kusubiri kulishwa maneno au kusokomezwa matambara midomoni na CCM, wangesoma na kujifunza mengi, kwa mfano utafiti kwamba - kama Uingereza ingefuata mfumo wa shirikisho mapema kama walivyofanya wenzake katika karne ya ishirini, Jamhuri ya Ireland (hii ni tofauti na Ireland ya Kaskazini), isingejitoa UK. Lakini sio hivyo tu, pia United Kingdom isingekumbwa na ugaidi uliotishia kuisambaratisha UK baada ya mzozo wa muda mrefu baina ya Westminster na Ireland ya Kaskazini. Ni baada ya Westminster kukubaliana na Ireland ya kaskazini juu ya umuhimu wa devolution, amani ikapatikana. Pia, kura ya maoni ya Scotland ambayo ilitishia usalama wa taifa la UK pamoja na sekta yake ya biashara, haya yote yasingetokea iwapo UK ingeamua kuiga wenzake na kufuata mfumo wa shirikisho. Baada ya kujifunza makosa, leo UK is more of a federation than a unitary system.

Wanasiasa wetu wana haja ya kuelewa kwamba kabla ya utawala wa Labor party chini ya Tony Blair kuingia madarakani (1997), UK’s unitary system was slowly disintegrating for over a century. Kwa mfano:


  1. It is because of the unitary system, violent struggle for home rule gained strength in the 1880s
  2. It is because of the unitary system, Ireland became independent in 1922.
  3. It is unitary system that led to Scottish and Welsh nationalism.
  4. It is unitary system that led to Civil war in Northern Ireland.

Baada ya kujifunza na kukubali mapungufu ya mfuko wa unitary, Serikali chini ya Tony Blair ikaamua kuchukua maamuzi magumu mwaka 1998, ambapo a ‘semi-federal’ structure ikaanza kuwa implemented in the UK ili kukidhi mahitaji ya devolution for Scotland and Northern Ireland. Pamoja na juhudi hizi, wananchi wa Scotland bado hawakuridhika na mabadililo kwani bado- it was more like a self-governing colony arrangement, na kufikia kiwango cha kuwa na judicial appeals to the Privy Council katika masuala ya kikatiba. Hali hii ikaanza kuonyesha dalili za instability na kutishia muungano uliopo, ndio maana haukupita muda mrefu, wanasiasa wengi wa Uingereza bila ya kujalisha itikadi zao za vyama, wakaanza kuona kwamba ‘an independent Scotland’ was a real possibility kupitia kura ya maoni, na hii ilikuwa miaka kumi iliyopita. Hata wale viongozi waliokuwa upinzani wakati ule (Conservatives), ambao awali they voted against devolution of scotland, wakaamua kuweka utaifa mbele na kuungana na Blair katika kuhakikisha kwamba muungano unadumishwa through more devolution. Hii ni kwa sababu viongozi hawa wapo kutumikia wananchi, sio vyama vyao vya siasa. Hii ni tofauti na kwetu ambapo kiongozi anaogopa/anakwepa kuongoza mabadiliko. Iwapo kiongozi anafikia hatua hiyo, ana sifa gani ya maana aliyobakia nayo kuitwa kiongozi?

Nimeipenda hii post yako.Lakini umepotea sana kaka upo?
 
Tatizo letu kubwa ni kutopata elimu yenye uhakika kuhusu masuala ya elimu ya siasa na hasa sheria za mwananchi husika.Na pili rushwa,umaskini unaotumika sana na watawala wetu,na tukumbuke kuwa hatuna viongozi bali tunawatawala.Viongozi walishakufa wote.Hakuna UZALENDO tukauona bali kuna uzalendo wa maneno matamu ambayo sababu ya elimu duni za watu wetu tunakosa kwenda mbele bali kurudi nyuma.Na mbaya zaidi watakuja kushtuka pale balaa la vurugu na mauaji ya wenyewe kwa wenyewe yakianza na sababu ya wao wanapesa watatukimbia wao na familia zao na sisi tukabaki kwenye vurugu letu.Kama tuonavyo leo SUDAN kusini kinachotokea.Watawala wamekosa uvumilivu kisiasa,utashi,busara na weledi.Wote wapo kwa kujinufaisisha zaidi wao na familia zao.wametuacha watanzania tukiendelea kuw amaskini wakutupwa.Na nina uhakika wanajua kuwa likitokea la kutokea wao na familia zao watakimbia na kukaa ughaibuni.

Watu kama Nguruvi na Mchambuzi mngeweza kutusaidia kama mnaweza kupata vipindi kwenye TV ili tuweze kujifunaza zaidi,maana mara nyingi hoja zenu zina mshiko kuliko kawaida.

Asanteni sana.
 
HOTUBA YA CAMERON NA MAZINGAOMBWE YA CCM

''Just as the people of Scotland will have more power over their affairs, so it follows that the people of England, Wales and Northern Ireland must have a bigger say over theirs,"
Hapa anasema(Tafsiri isiyo rasmi), kama ambavyo Scotland itakavyokuwa na mamlaka zaidi juu ya mambo yao,vivyo hivyo watafuata watu wa England, Wales na Nothern Ireland kuwa na kauli juu ya mambo yao.


Cameron ametambua kuwa kuwapa nguvu Zaidi Scotland kunajenga chuki na kuimarisha upinzani dhidi yake kutoka mataifa mengine.

Waziri mkuu kasimama katika ukweli na si ubabaishaji.
CCM wanachezesha vidole haraka na kusema ni mazingaombwe( Mzee Mwanakijiji )

Wanaamini kuwapa Zanzibar Zaidi ni kuimarisha na si kuua muungano.
Laiti wangelikuwa na ufahamu na akili kidogo, ingewaingia akilini kuwa tangu wamejikita kutoa zawadi kwa Zanzibar, hali ya Utanganyika ndivyo inavyopata nguvu Zaidi.

Leo Watanganyika ni united kuliko nyakati za Jumbe, G55 n.k. baada ya kugundua upendeleo usio na kikomo kwa wazanzibar. Na hapo waziri mkuu anaendelea

It is absolutely right that a new and fair settlement for Scotland should be accompanied by a new and fair settlement that applies to all parts of the United Kingdom

Ni haki kabisa muafaka mpya na maridhiano kwa Scotland yaambatane na muafaka na maridhiano yanayotakiwa kwa pande zote za United Kingdom

Msikilize Cameron anavyotema hekima
"In Wales, there are proposals to give the Welsh Government and Assembly more powers.

"And I want Wales to be at the heart of the debate on how to make our United Kingdom work for all our nations.
"In Northern Ireland, we must work to ensure that the devolved institutions function effectively.
I have long believed that a crucial part missing from this national discussion is England.

"We have heard the voice of Scotland - and now the millions of voices of England must not go ignored.
Mistari ya mwisho anasema, ninaamini kwa muda mrefu kuwa sehemu inayokosekana katika mjadala wa kitaifa ni England. Tumesikia kauli za watu wa Scotland, na sasa mamilioni ya sauti za England hayapaswi kupuuzwa.

Pengine maneno haya angeyasema Rais wetu. Kwa muda mrefu tumesikia kelele za Wazanzibar, na ni muda sasa sauti za Watanganyika zisipuuzwe.

Hili CCM hawalioni, hata katika bunge la Sitta-comedy leo wanaenda kupiga kura kuhalalisha rasimu ya CCM ya mafichoni.
Rasimu hiyo imeandikwa bila vifungu 1 na 6 ambavyo ni moyo wa katiba.

Endapo vifungu hivyo havipo na havikujadiliwa, muundo wa katiba ya nchi unapatikanaje? Hii ina maana moja, rasimu yao ilikuwa tayari kama tulivyowahi kuandika huko nyuma, kinachofanyika ni kuhalalisha kwa kutumia bunge lenye ‘uharamu'' kwa kukosa muafaka wa kisiasa.

Na mwisho, kiongozi wa UK mwenye maono, akili na busara anasema haya
"So, just as Scotland will vote separately in the Scottish Parliament on their issues of tax, spending and welfare, so too England, as well as Wales and Northern Ireland, should be able to vote on these issues - and all this must take place in tandem with, and at the same pace as, the settlement for Scotland."
Hivyo, kwavile Scotland itaamua ndani ya bunge lao kuhusu mamo ya kodi, matumizi na shuhuli za kijamii, vile vile England, Wales na Northern Ireland zinapaswa kuamua mambo yao. Haya yatafanyika kwa kufuatana na kasi na maridhiano ya Scotland

Naweza kusema kwa dhati kabisa kuwa Cameron alipaswa kuja kusimamia mchakato wa katiba na hasa serikali yetu.
Tume ya Warioba iliona mbali kuliko Cameron, leo Cameron ni shujaa na Warioba ni msaliti.


Ndio maana tunasema, tatizo la Tanzania si umasikini wa rasilimali, ni umasikini wa viongozi wetu akina Stta JK na wabunge wa CCM walioskmezwa maambara. Inasiitisha sana.

Leo wanachezesha vidole kw kura za fax na internet ili wapewe vyeti na Rais. Hawa ndio umasikini wa Tz
 
Nape na mwigulu pitia uzi huu tafadhali
Hawataki kusikia ukweli, wanaongozwa na utashi.

Leo wanaendelea kujidanganya na kuwadanganya Watanzania.

Cameron aliwaeleza watu wake ukweli, sijui lini tutapata Cameron wetu.

Tanzania si masikini, umasikini wetu ni kutokuwa na viongozi na hao waliopo hawana maarifa, ni majuha, mazezeta. Kiongozi anayehamisha magoli kila dakika heshima yake ni kama haipo.

Waingereza wajivunie akina Cmaeron
 
Nakubaliana na nguruvi kasoro uhalali wa tume ya warioba...labda tungeanza na kura ya maoni...
 
Back
Top Bottom