Registered_jf
JF-Expert Member
- Nov 27, 2024
- 1,173
- 1,991
Kusubiri sayansi ibatilishe uwepo wa Mungu ni kama kusubiri ramani ifute ardhi: ramani inapokuwa sahihi zaidi, ndivyo dunia inavyoonekana halisi zaidi.Waiting for science to disprove God is like waiting for a map to erase the land: the more accurate the map becomes, the more real the world appears.
Its like expecting a mirror to hide the face: the clearer the reflection, the more undeniable the presence.
It's like searching for darkness in the heart of the sun: the deeper you look, the more light you find.
Kuna kitabu Cha mwarabu kimejaa ngonjera nyingi na kinaitwa " kimekamilika" na tunskatazwa kusoma kitabu kingine eti chenyewe kina Kila kitu. Niwaulize wahitimu wa kitabu hicho bacho hukaririwa. Je waliwahi kugundua hata sindano kutumia ilim iliyopo kwenye chapisho hilo la mwarabu?Science is the Savior of Humanity
Imekuwa ni jambo la kawaida sana kukutana na maandiko ya watu wakisifu miungu yao na imani zao. Lakini ni mara chache sana kukutana na maandiko yanayoeleza mambo makuu na ya kishujaa yaliyofanywa na binadamu wachache waliojitolea kwa dhati kuisaidia jamii kupitia gunduzi na tafiti mbalimbali za kisayansi.
Ufuatao ni uchambuzi mfupi unaoeleza kwa nini sayansi inapaswa kutazamwa kama mkombozi wa kweli wa binadamu katika kutatua matatizo ya maisha ya kila siku.
1. Sayansi imeongeza umri wa kuishi wa binadamu
Sayansi imeweza na itaendelea kuwezesha binadamu kuishi maisha marefu zaidi ukilinganisha na karne zilizopita. Leo hii kuna chanjo nyingi dhidi ya magonjwa ambayo zamani yalikuwa tishio kubwa kwa maisha ya watu.
Bila ugunduzi wa “germ theory of disease”, hakuna ambaye angeelewa chanzo cha magonjwa mengi wala namna ya kuyatibu. Thibitisha hili kwa kulinganisha idadi ya watu (population) ya miaka ya 1990 na ya mwaka 2022 – utaona ongezeko kubwa sana la watu duniani.
Sasa jiulize: kama watu wangelitegemea tu maombi, ibada, kufunga, au hija, je magonjwa kama polio, tetekuwanga, surua na mengine yangeweza kutokomezwa kupitia chanjo?
2. Kupungua kwa vifo vinavyoweza kuzuilika
Vifo vilivyokuwa vinaepukika vimepungua kwa kiwango kikubwa. Mfano mzuri ni kupungua kwa kiwango cha vifo vya watoto wachanga (Infant Mortality Rate). Haya yote ni matokeo ya maendeleo ya sayansi na huduma za afya.
Leo hii mama mjamzito anaweza kuchagua kujifungua kwa njia ya kawaida au kwa upasuaji salama. Jiulize bibi zetu wa miaka ya 1500 walipitia changamoto kiasi gani wakati wa kujifungua, na ni watoto wangapi walipoteza maisha kutokana na kukosekana kwa tiba na teknolojia ya kitabibu?
Je, matatizo hayo yangetatuliwa kwa maombi peke yake, mafuta ya upako, au dua?
3. Nishati ya umeme – zao la fikra za kisayansi
Nishati ya umeme kwa sasa ni hitaji muhimu sana kwa binadamu. Maisha ya kisasa hayawezi kuendelea bila umeme: mawasiliano, hospitali, elimu, viwanda, usafiri na hata shughuli ndogo kama kupasi nguo au kuhifadhi chakula.
Haya yote ni matokeo ya kazi za watu waliotumia akili na utafiti wa kisayansi hadi kugundua misingi ya umeme kama “Direct Current (DC)” na “Alternating Current (AC)”.
Jiulize: kama Nikola Tesla na wanasayansi wenzake wangesubiri maono ya kimiujiza badala ya kufanya utafiti, je leo tungekuwa na umeme wa maji (Hydroelectric Power) au mitambo ya kisasa?
4. Mapinduzi katika sekta ya usafiri
Usafiri ni nguzo muhimu ya maisha ya binadamu, hasa mijini. Biashara, elimu, afya na shughuli za kijamii zote hutegemea usafiri.
Magari, meli na ndege havikutokea tu kwa bahati mbaya. Ni matokeo ya tafiti, majaribio na ubunifu wa kisayansi. Leo mabilioni ya watu wanatumia vyombo vya moto bila hata kufahamu kwa undani jinsi injini zinavyofanya kazi.
Kama ndugu Wright (Wright Brothers) wangelisubiri maono badala ya kufanya majaribio ya kisayansi, je leo tungekuwa na kitu kinachoitwa ndege?
5. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
Tunatumia simu na intaneti kila siku, lakini wengi hatujui namna mawimbi yanavyosafiri na kubadilishwa kuwa sauti au maandishi kwa umbali wa maelfu ya kilomita.
Leo mtu aliyeko Tanzania anaweza kuzungumza na mtu aliyeko Marekani, au hata kuwasiliana na chombo kilicho angani. Haya yote ni matokeo ya sayansi na teknolojia, si miujiza.
Maendeleo ya hivi karibuni kama Akili Unde (Artificial Intelligence) yanaonesha wazi kuwa mustakabali wa binadamu unategemea zaidi sayansi kuliko chochote kingine – hasa kwenye afya, elimu na biashara.
Hitimisho
Hayo ni machache tu kati ya maelfu ya mafanikio ya sayansi.
Maarifa ya kisayansi hayahitaji kuabudiwa wala kusifiwa kama dini. Yanahitaji kusherehekewa, kujadiliwa na kufundishwa kwa uhuru kwa ajili ya kujenga kesho iliyo bora zaidi.
Not by Almighty
But by Rationality
Not by Grace
But by Effort
Embrace Reality
Swadaktaaaaa!!Naunga mkono hoja, na jinsi muda unavyoenda sayansi itakuja kutoa majibu ya maswali magumu zaidi kwa njia ya uhakika zaidi, tuupe mda nafasi tu.
😂😂😂😂😂Usilete ulokole kwenye Physics
Mbona Ilim, 😂😂😂😂Kuna kitabu Cha mwarabu kimejaa ngonjera nyingi na kinaitwa " kimekamilika" na tunskatazwa kusoma kitabu kingine eti chenyewe kina Kila kitu. Niwaulize wahitimu wa kitabu hicho bacho hukaririwa. Je waliwahi kugundua hata sindano kutumia ilim iliyopo kwenye chapisho hilo la mwarabu?
Kuna kitabu Cha mwarabu kimejaa ngonjera nyingi na kinaitwa " kimekamilika" na tunskatazwa kusoma kitabu kingine eti chenyewe kina Kila kitu. Niwaulize wahitimu wa kitabu hicho bacho hukaririwa. Je waliwahi kugundua hata sindano kutumia ilim iliyopo kwenye chapisho hilo la mwarabu?
Baada ya miaka 50 ijayo jinsi sayansi inavyozidi kuleta mapinduzi na kuyafanya mambo mengi kuwa wazi na yaliyo kuwa yanaonekana kuwa ni miujiza Ya kimungu kuwa ni kitu Cha kawaida Hilo kundi la wakanyaga mafuta nalo lote litatoweka watu watakuwa wanahitaji fact tu na sio Imani za kidiniEmbrace the Madness, hutaki kunya BOGA, nimekuelewa mkuu hapo umechukua point 3 ila kwa wale wafuasi wa kukanyaga mafuta utapata tabu huwaambii kitu
😁Matumizi ya VPN ni dhambi, YESU akirudi leo jua kwamba moto wa Jehanamu unakuhusu.
Aliye muumba binadamu ni nani?Kabla hatujaisifu sayansi tumpe Kwanza sifa zake aliyemuumba BINADAMU alafu hyo binadamu ndo akagundua SAYANSI.
MWENYEZI mungu nani mwingine?kama sio yeyeAliye muumba binadamu ni nani?
ThibitishaMWENYEZI mungu nani mwingine?kama sio yeye
Soma Quran na biblia amesema mwenyewe.Thibitisha
Kwa hiyo kusoma kitabu cha ngoswe penzi kitovu cha uzembe ndio kina thibitisha uwepo wa mazoea kwenye ulimwengu wa hakika na sio wa simulizi?Soma Quran na biblia amesema mwenyewe.
So did Mohamed flew to heaven with a winged horse?Napenda vilaza kama nyinyi
Na najua huna elimu ulikimbia umande au ulipitishwa na kimajina
Kwanza twende kwenye uvumbuzi, kama lugha haipandi shauri yako, ndio hasara ya kuwa kilaza
Kwenye hesabu, hakuna hesabu isiyokuwa na Aljebra
- Algebra discipline: Al-Khwarizmi is considered the father of the algebra discipline. The word Algebra comes from the Arabic الجبر (al-jabr) in the title of his book Ilm al-jabr wa'l-muḳābala. He was the first to treat algebra as an independent discipline in its own right
Kwenye Utabibu, hii ndio ilikuwa encyclopaedia ya kufundishia udaktari mpaka ulaya miaka ile,
- The Canon of Medicine (Arabic: القانون في الطب, romanized: al-Qānūn fī l-ṭibb) is an encyclopedia of medicine in five books compiled by Avicenna (ابن سینا, ibn Sina) and completed in 1025.It presents an overview of the contemporary medical knowledge of the Islamic world, It became the standard textbook for teaching in European universities into the early modern period, The Canon of Medicine remained a medical authority for centuries. It set the standards for medicine in medieval Europe and the Islamic world and was used as a standard medical textbook through the 18th century in Europe
Sasa twende kwenye Quran unayoita ngojera kama kuna uvumbuzi kulinganisha na upupu wa vatikani kuhusu yuda kamtomba huyu na kumzaa yule, au pumba za mazingaombwe ya kutoa mikate na samaki iliyofichwa kwenye magunia
In Surah Ar-Rahman, it states “He released the two seas, meeting [side by side], Between them is a barrier [so] neither of them transgresses” (Quran, 55:19-20).
- Science has discovered that in places where two different seas meet, there is a barrier that divides them which helps both the seas maintain their own temperature, salinity, as well as density
- The scientific understanding of the separation of seas and oceans—meaning the physical, hydrological, or geological barriers that keep different bodies of water from fully mixing—has been discovered and refined over several centuries, with key milestones occurring in the 16th, 18th, and 20th centuries.
Ni kweli ni Mungu wa Baruch De Spinoza, yule anaejidhihirsha kupitia gunduzi za kisayansi na mazingira asilia, na wala SIYO yule wa imani potofu/kishirikina (superstitious beliefs) za wakristo, wayahudi, na waisilamuKabla hatujaisifu sayansi tumpe Kwanza sifa zake aliyemuumba BINADAMU alafu hyo binadamu ndo akagundua SAYANSI.
Wakati Sayansi ya leo imejua kuna nguvu ya asili isiyoonekana na inayoundwa na maada ya isiyooneka na kwa kutokujua wakaamua kuita Dark Enegy na Dark Matter, na huu utafiti ndio unawasukuma kusema kuna uwezekano wa kuwa na mfumo mwingine wa maisha wenye viumbe huko anga za mbali, na pia kutoa baadhi ya ushahidi wa huo kwa matukio yasiyoelezeka, hapo ndio neno Aliens linapokuja kwenye picha kamili.So did Mohamed flew to heaven with a winged horse?
Mungu wa waislam alikuwepo kitambo hata hii Dunia haikuwepoNi kweli ni Mungu wa Baruch De Spinoza, yule anaejidhihirsha kupitia gunduzi za kisayansi na mazingira asilia, na wala SIYO yule wa imani potofu/kishirikina (superstitious beliefs) za wakristo, wayahudi, na waisilamu
Ishu ya dark matter na dark energy haihusiani kabisa na stori za imani potofu za kidini (superstitious beliefs) za waislamu, wakristo, na wayahudi.Wakati Sayansi ya leo imejua kuna nguvu ya asili isiyoonekana na inayoundwa na maada ya isiyooneka na kwa kutokujua wakaamua kuita Dark Enegy na Dark Matter, na huu utafiti ndio unawasukuma kusema kuna uwezekano wa kuwa na mfumo mwingine wa maisha wenye viumbe huko anga za mbali, na pia kutoa baadhi ya ushahidi wa huo kwa matukio yasiyoelezeka, hapo ndio neno Aliens linapokuja kwenye picha kamili.