Kimilidzo
JF-Expert Member
- Jan 3, 2011
- 1,346
- 613
Sisi wakazi wa vijijini tulikuwa tumemiss sana sauti ya Rais wetu wa moyoni, ambaye akituamuru tuingie mtaani kama Misri na Algeria tunaenda mara moja bila kupinga, Dr Slaa (PhD). Hatimaye jana kupitia luninga ya ITV tumeisikia kutoka mahakamani Arusha. Watu walizizima kwa furaha pale kilabuni tulipokuwa tunaangalia luninga kwa kulipia kutokana na ukosefu wa umeme. Sauti ya Rais wa mioyoni mwetu imekonga nyoyo zetu na tunatamani kesi iwe inasikilizwa kila siku ili tuwe tunamsikia mara kwa mara. Sauti ambayo inaweza kumtoa nyoka pangoni. Tumefarijika kusikia kuwa Rais atatutembelea kwa maandamano kuanzia keshokutwa na atafika hadi wilayani. tunasema Karibu sana Rais wetu mpendwa Dr Slaa (PhD) na Dowans ya JK hailipwi ng'ooooooo