Sato na Sangara kutoka China

Sato na Sangara kutoka China

Spina

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
704
Reaction score
163
Kuna sato na sangara hai na waliogandishwa wanauzwa mwananyamala na Wachina. Bei yake ni poa kuliko Sato na Sangara tika Mwanza. Hao samaki ni zao la vifaranga waliochukuliwa Lake victoria kijanja na kuoteshwa kwenye bwawa kubwa huko Gwanzhu. Sera za Serikali yetu zinatoa fursa kwa wachina/wageni na kudidimiza wavuvi na viwanda vya ndani. Jadili kwa hoja. Hatua thabiti zichukuliwe haswa kuhakikisha Wachina hawa wamefuata taratibu na wanalipa kodi kuwaingiza tz.
 
Sioni tatizo kwa wachina kuuza sato na sangara kwa bei nafuu,maana inamsaidia mtanzania wa kawaida kupata hao samaki kwa beo rahisi,sio wote wana afford kununua sato kilo kwa 10,000 na sangara kwa 8,000 kama wanauza chini ya hapo sio mbaya.
 
Wauze tu ilimradi wasiwe na madhara maana wachina akili zao hazina msimamo kabisaa
 
Hii ingewezekana ata hapa Tanzania ila sheria sinazohusiana na uvuvi na ziwa Victoria ndo kikwazo.Samaki wa kufuga baada ya miezi mitatu anauzika ni ajira ngapi zingetengenezwa?
 
Mambo mengine serikali haihusiki bali ni ubinafsi wetu saisi wananchi. Huo uvuvi haramu kwa nyavu na baruti ndo unachangia sekta ya uvuvi kuyumba.

Soko ni huria hivyo km huwezi kujipanga kushindana utakuwa mtazamaji, sisi walaji kwetu cha msingi usalama hata km zingetoka misri.
 
kama hawana madhara acha wauze tu kwa bei ya chini tena walete wengi kama walivyomwaga vibua, maana hawa victoria ni kama tunasuza mdomo tu.
 
Wauze tu ilimradi wasiwe na madhara maana wachina akili zao hazina msimamo kabisaa

Samaki hao sina hakika sana kama ni salama kwa afya zetu,hao vibua kuna mchina niko nae ofisin alishanikataza kuwatumia,nilipotaka kuhoji sana aligoma na jibu likabaki hilohilo 'si SAWA!!!
 
ndo yale yale, Baba anajali marafiki na majirani kuliko wanae
 
Siku tatu zilizopita nilienda soko la samaki la Kivukoni,Dar es salaam kwa bahati nzuri nilikuwa na expert wa masuala ya samaki.Kuna samaki wengi alinikataza nisiwanunue akaniambia hao wanatoka China na wamewekewa madawa ya kuwazuia wasiharibike kwa kweli nilistushwa sana na taarifa ile ikanibidi niende eneo ambalo wavuvi huwa wanashusha samaki waliotoka kuvuliwa muda huo huo ndo nikawanunua.
 
Samaki hao sina hakika sana kama ni salama kwa afya zetu,hao vibua kuna mchina niko nae ofisin alishanikataza kuwatumia,nilipotaka kuhoji sana aligoma na jibu likabaki hilohilo 'si SAWA!!!

Hapo sasa kazi kwetu ukweli tunaujua anayetaka anunue asiyetaka aache. Tusiponunua watakosa soko biashara itakufa
 
Kwel mkuu the mountain lion,wale si kwamba wanawekwa kwenye barafu la hasha kuna dawa wanapuliziwa wana uweko wa kukaa hata mwaka,na kuthibitisha hilo jaribu kununua hao vibua hata akae siku nzima juan hayeyuki!!swali je ni barafu gan hyo???
 
Siku tatu zilizopita nilienda soko la samaki la Kivukoni,Dar es salaam kwa bahati nzuri nilikuwa na expert wa masuala ya samaki.Kuna samaki wengi alinikataza nisiwanunue akaniambia hao wanatoka China na wamewekewa madawa ya kuwazuia wasiharibike kwa kweli nilistushwa sana na taarifa ile ikanibidi niende eneo ambalo wavuvi huwa wanashusha samaki waliotoka kuvuliwa muda huo huo ndo nikawanunua.

Wamejaa mtaani hao samaki na kwenye vibanda vya Chips...Wanakaa hata mwaka bila kuharibika...Sijui kama ni salama kwa Afya za walaji
 
Kuna sato na sangara hai na waliogandishwa wanauzwa mwananyamala na Wachina. Bei yake ni poa kuliko Sato na Sangara tika Mwanza. Hao samaki ni zao la vifaranga waliochukuliwa Lake victoria kijanja na kuoteshwa kwenye bwawa kubwa huko Gwanzhu. Sera za Serikali yetu zinatoa fursa kwa wachina/wageni na kudidimiza wavuvi na viwanda vya ndani. Jadili kwa hoja. Hatua thabiti zichukuliwe haswa kuhakikisha Wachina hawa wamefuata taratibu na wanalipa kodi kuwaingiza tz.
umaskini ni ki2 kikibaya sana. Nchi imegeuzwa jalala na watu wachache wachoyo na walafi. Badala ya kusimamia ipasavyo uvuvi nchini wanaudidimiza. Nasikia pia kuna kuku wengi wa nyama kutoka Brazil.
 
​wachina bwana, naomba hao samaki wawe samaki wazuri mana unaweza kuta wametengeneza hao
 
Sioni tatizo kwa wachina kuuza sato na sangara kwa bei nafuu,maana inamsaidia mtanzania wa kawaida kupata hao samaki kwa beo rahisi,sio wote wana afford kununua sato kilo kwa 10,000 na sangara kwa 8,000 kama wanauza chini ya hapo sio mbaya.

Absolutely true
 
samaki wanaweza kuwa artificial hao, kumbuka mwaka juzi yaliletwa mayai ya kuku artificial toka china!
 
Back
Top Bottom