JF Member
JF-Expert Member
- Dec 14, 2014
- 7,393
- 9,665
Siasa ni msingi wa mambo mengi hapa diniani. Siasa iko kila sehemu, kanisani, makazini, na hata kwenye kumbi za starehe.
Siasa ni Imani, mtu akiishi kwenye mlengo furani wa siasa na akakolea ni ngumu sana kumuondoa huko.
Awamu ya Tano ilikuwa na Aina yake ya Siasa, mlengo wake wa siasa, na hii ikawa kama Imani kwa watu walio hudumu katika awamu Ile. Na wananchi wengi pia wakazoe mtindo ule wa siasa, hasa we aliokuwa wanyonge:
Siasa hizo zilikuwa na mambo yafuatayo;
1. Siasa za hapa kazi tu: yaani watu walikuwa wakiamka wakilala wanawaza kazi tu. Mambo ya starehe hapana na yalikuwa machache mno. Na hata mambo ya Siasa kila Mara yakapigwa marufuku, mambo ya show off yakapungua. Watu wakajenga Imani ya hapa kazi tu
2. Siasa za kujitegemea. Hii iliwajengea watanzania matamanio ya kutaka kujitegemea, na wengi waliamini wanaweza kujitegemea bila kuomba omba kwa Wazungu.
3. Siasa za kuwajali wanyonge. Wanyonge walitembea kifua mbele.
4. n.k..hizo ni mifano tu Aina ya Siasa ambazo awamu ya Tano ilijenga Imani.
Bàada ya kiongozi mkuu kuaga Dunia, watu wengi Sana walilia na kuhudhinika. Lakini wangine waliamini anaeingia ataendelea na Aina Ile ya utawala/siasa.
Wakashangaa amewaacha na kujiunga na wale waliokuwa kinyume na kiongozi wao (Kigogo2014 Group).
Hii inawatesa wengi Sana hasa walio na imani ya utawala wa awamu ya Tano. Wengi wanaenda mbali na kusema Mama ndie alikuwa anavujisha siri za awamu ya Tano ( kwa kigogo 2014). Na wengine Wana muita msariti.
Sasa basi, vita imeanza kupamba moto. Na hii vita inapiganwa kwa style hii.
1. Watu wa awamu ya Sita wameshikilia mitandao. Kama kawaida Yao hata awamu ya Tano walikuwa vile vile. Na wanawapeleka hasa awamu ya Tano.
2. Watu wa amawamu ya Sita wameshika majukwaa ya kisiasa na kiutawala. Hivyo Wana nguvu na visemeo wanavyo.
3. Watu wa amawamu ya Tano, wanashikilia majeshi yetu. Kwa maana kwamba majeshi yetu bado yanaishi kwa Imani ya awamu ya Tano. Hayajaelewa vizuri Imani ya awamu ya sita. Si mnajua majeshi yetu yameundwa kwa mtindo wa hapa kazi tu tangu uhuru?
4. Watu wa awamu ya Tano wameshikilia vizuri Sana siasa za chini kwa chini hasa kwa wanyonge. Ukiongea na watu watano wale wa nchini, nne haiwaelewi hii awamu. Wengi watakwambia ni awamu ya wapigaji. Ndio maana hata mawaziri wakitumia ndege utasikia wapigaji wanapenda Raha.
Vita hii vinaipa nguvu awamu ya Tano kushinda uchaguzi iwapo uchaguzi ungefanyika Leo. Kwa maana ya walio wapiga kura ni wale wanao iunga mkono awamu ya Tano.
Awamu ya Tano haijapata mtu wa kujitoa hadharani na kutetea, Imani Yao. Hivyo wanaitwa washamba.
Awamu ya sita, inajulikana kama awamu ya wahuni. Awamu ya msoga. Wengi wanawaita wezi.
Awamu ya Tano , wanajulikana kama sukuma gang, hii inawapunguzia mashabiki wasio wasukuma. Ila inawapa nguvu wasukuma kuendelea kuipigania awamu ya Tano kimyakimya.
Itaendelea
Siasa ni Imani, mtu akiishi kwenye mlengo furani wa siasa na akakolea ni ngumu sana kumuondoa huko.
Awamu ya Tano ilikuwa na Aina yake ya Siasa, mlengo wake wa siasa, na hii ikawa kama Imani kwa watu walio hudumu katika awamu Ile. Na wananchi wengi pia wakazoe mtindo ule wa siasa, hasa we aliokuwa wanyonge:
Siasa hizo zilikuwa na mambo yafuatayo;
1. Siasa za hapa kazi tu: yaani watu walikuwa wakiamka wakilala wanawaza kazi tu. Mambo ya starehe hapana na yalikuwa machache mno. Na hata mambo ya Siasa kila Mara yakapigwa marufuku, mambo ya show off yakapungua. Watu wakajenga Imani ya hapa kazi tu
2. Siasa za kujitegemea. Hii iliwajengea watanzania matamanio ya kutaka kujitegemea, na wengi waliamini wanaweza kujitegemea bila kuomba omba kwa Wazungu.
3. Siasa za kuwajali wanyonge. Wanyonge walitembea kifua mbele.
4. n.k..hizo ni mifano tu Aina ya Siasa ambazo awamu ya Tano ilijenga Imani.
Bàada ya kiongozi mkuu kuaga Dunia, watu wengi Sana walilia na kuhudhinika. Lakini wangine waliamini anaeingia ataendelea na Aina Ile ya utawala/siasa.
Wakashangaa amewaacha na kujiunga na wale waliokuwa kinyume na kiongozi wao (Kigogo2014 Group).
Hii inawatesa wengi Sana hasa walio na imani ya utawala wa awamu ya Tano. Wengi wanaenda mbali na kusema Mama ndie alikuwa anavujisha siri za awamu ya Tano ( kwa kigogo 2014). Na wengine Wana muita msariti.
Sasa basi, vita imeanza kupamba moto. Na hii vita inapiganwa kwa style hii.
1. Watu wa awamu ya Sita wameshikilia mitandao. Kama kawaida Yao hata awamu ya Tano walikuwa vile vile. Na wanawapeleka hasa awamu ya Tano.
2. Watu wa amawamu ya Sita wameshika majukwaa ya kisiasa na kiutawala. Hivyo Wana nguvu na visemeo wanavyo.
3. Watu wa amawamu ya Tano, wanashikilia majeshi yetu. Kwa maana kwamba majeshi yetu bado yanaishi kwa Imani ya awamu ya Tano. Hayajaelewa vizuri Imani ya awamu ya sita. Si mnajua majeshi yetu yameundwa kwa mtindo wa hapa kazi tu tangu uhuru?
4. Watu wa awamu ya Tano wameshikilia vizuri Sana siasa za chini kwa chini hasa kwa wanyonge. Ukiongea na watu watano wale wa nchini, nne haiwaelewi hii awamu. Wengi watakwambia ni awamu ya wapigaji. Ndio maana hata mawaziri wakitumia ndege utasikia wapigaji wanapenda Raha.
Vita hii vinaipa nguvu awamu ya Tano kushinda uchaguzi iwapo uchaguzi ungefanyika Leo. Kwa maana ya walio wapiga kura ni wale wanao iunga mkono awamu ya Tano.
Awamu ya Tano haijapata mtu wa kujitoa hadharani na kutetea, Imani Yao. Hivyo wanaitwa washamba.
Awamu ya sita, inajulikana kama awamu ya wahuni. Awamu ya msoga. Wengi wanawaita wezi.
Awamu ya Tano , wanajulikana kama sukuma gang, hii inawapunguzia mashabiki wasio wasukuma. Ila inawapa nguvu wasukuma kuendelea kuipigania awamu ya Tano kimyakimya.
Itaendelea