Sasa nimemwelewa Mh Lowassa!!

Ni hayo maamuzi magumu ndio ambayo tunadhani yangeweza kuleta suluhu katika yote...Tumsikilize Mhe. Jaji Warioba katika kipindi cha dakika 45 ITV atalonga nini manake katika dondoo tu inaonekana nae analaumu utawala uliopo kwa kudhani bado upo katika kipindi cha kufanya kampeni badala ya kutekeleza mikakati ya kuwaletea wananchi maendeleo...
 
Kufanya jambo jema, ila kwa nia mbovu hakulihalalishi ulilolifanya. Ndicho alichokifanya huyu baba yako Lowassa: Kutumia matatizo ya Watanzania kujipatia manufaa. Hawezi kuja leo akadai alitumwa na mkuu wake! Alikuwa wapi siku zote? Ananuka ufisadi, hafai hata kwa udiwani.
 
Kumsafisha Lowassa haihitaji hata dodoki, si mda mrefu mr. White atang'ara ile mbaya. Watanzania tuna vipaji vya kusahau. 2015 Lowassa ndani ya ikulu.
 
Mkuu wa kaya katufikisha hapa tulipo na sasa hatma ya magamba si mikononi mwake tena bali wale tunaoambiwa ni mafisadi papa ndani ya magamba
 
Ni hayo maamuzi magumu ndio ambayo tunadhani yangeweza kuleta suluhu katika yote...Tumsikilize Mhe. Jaji Warioba katika kipindi cha dakika 45 ITV atalonga nini manake katika dondoo tu inaonekana nae analaumu utawala uliopo kwa kudhani bado upo katika kipindi cha kufanya kampeni badala ya kutekeleza mikakati ya kuwaletea wananchi maendeleo...

Maamuzi magumu ili utekeleze ujambazi, ni bora kutokufanya kabisa. Kamwambia hujawakuta
 
Kumsafisha Lowassa haihitaji hata dodoki, si mda mrefu mr. White atang'ara ile mbaya. Watanzania tuna vipaji vya kusahau. 2015 Lowassa ndani ya ikulu.

Kumsafisha huyu Mmeru labda ukiue chama kabisa, waanze upya. Ananuka uvundo wa ufisadi
 
Mkuu ulichoongea ni sawa kabisa na ndiyo ukweli wenyewe huo.Ila tatizo ni kwamba Lowassa amechafuka sana na hawezi kusafishika hata
kwa dodoki la chuma.....but the guy is so good

We have said this, time and again that the guy is good for nothing.

Kama unasema hasafishiki, una maana ni mchafu na hiyo inaondoa hicho mnachoita "so good". Ametufikisha hapa tulipo. Kutokana na woga uliojengwa baada ya yeye kuvuruga, maamuzi yote yalikwama na muda mrefu ukawa wa malumbano ya uhalali wa Dowans na Richmond ambazo amezizalisha yeye.

Ukweli ni kwamba uamuzi wa kujiuzulu kwake ilikuwa ni mbinu ya kukimbia kujibu tuhuma maana alikuwa ameshikwa mahali ambapo asingeweza kujinusuru au kujikwamua bila kumaliza heshima yake ndogo aliyokuwa nayo. Walimshika pabaya na bila kutarajia. Yote kwa yote, kuwa na mchwa kwenye nyumba, wakimaliza akiba ya chakula ni tatizo kubwa ambalo haliwezi kuvumilika hata kama mchwa huyo kuna wakati hujenga kichuguu ambacho ni makazi ya nguchiro.
 
Unajua sijui!Ila kuna wanadam wako tofauti na wengine!Hii nchi bwana unaweza kuzimia ukiyajua yaliyomo humu!
 
mkuu umenena vema, LOWASSA alikuwa anachapa kazi si mchezo eg alihangaika ili kupata artificial rain, alipita hata sehemu mbovu kama LUMAGE huko Makete kuangalia chanzo cha UMEME wanachotumia wao nk Ndiyo maana watu wanasema 2015 the BEST present from CCM is EDWARD LOWASSA kimsingi huyu MBUNGE ni mchapa kazi ila basi tu

kwanini awe raisi lowassa tupo milioni 40 bana!
 
Lowassa amefanya maovu mengi na hawezi kusafishika. Ondoa yote, alifanya mkataba wa kutengeza mvua Thailand nani anakumbuka? Pesa nyingi ilitumika, achana kuhangaisha watanzania wavumilivu. Lowassa angekuwa China angehukumiwa cortmarsal kwa kupigwa risasi coz ni mtu HATARI sana, kwanza kaleta kiongozi wa nchi ambaye ni legelege (JK) kupitia mtandao, pili yeye binafsi ni mwizi kwa kufanya mikataba hewa kama RichMonduli hata kwenye chama chao cha magamba inasemekana alifanya mikataba tata (kitegauchumi). Kumleta Lowassa ni kuhatarisha utulivu wa nchi, hata akipitishwa na magamba hata lindika kabisa.
 
...Tumsikilize Mhe. Jaji Warioba katika kipindi cha dakika 45 ITV atalonga nini manake katika dondoo tu inaonekana nae analaumu utawala uliopo kwa kudhani bado upo katika kipindi cha kufanya kampeni badala ya kutekeleza mikakati ya kuwaletea wananchi maendeleo...
Mkuu Ngoshwe,
Warioba alishazibwa mdomo kwa kashfa ya Mwananchi Gold. Akithubutu kuchonga tu kesho utasikia ametinga Kisutu. Hakuna aliye msafi huko
 
Alaah, mwisho wa uchaguzi ni mwanzo wa uchaguzi mwingine!! nasikia harufu ya kampeni.
 
That time nakumbuka mkuu siku moja nilikua na appointment na Mkurugenzi mmoja wa Halmashauri nilimkuta ofisini akitetemeka na aliahirisha appointment yangu kisa next week kulikua na ziara ya Lowasa wilayani mwake.
hahaha, unaona, watu walikuwa wanachapa kazi kinguvu, kama hawataki kuchapa kazi walikuwa wanalazimishwa...sasa ona mwendo wa kibagamoyo tulionao sasa na huyu ******...hamna lolote. kama tatizo lilikuwa ni lowasa, mbona hadi leo hii wakati issue ya richmond imeshapotea na haihusiani na kinachoendelea sasaivi, umeme umekuwa tabu kuliko hata kipindi cha lowasa, kwani kipindi kile cha lowasa tulikuwa kwenye wakati mgumu kama tulivyo sasaivi? this is a worse staff aisee kwasasa, watu mara ngereja, mara kikwete etc....tujifunze kutokwenda mbaali kwa jambo kawaida kama ilivyokuwa kwenye richmond....lowasa kwa urais 2015 oyeeeeee. na atapita.
 
Nia si klumtetea Lowasa wala Mtu yeyeote ambae anatuhumiwa kwa kuchangia kurejesha nyuma maendeleo ya nchi hii. Ila kwa hali ilivyo sasa hata kama huwezi kushawishika unaweza kuona jinsi ilivyotofauti kuwa na Kiongozi wa mfano wa Lowasa katika mfumo wa utawala wetu...ni mangapi tumekuwa tukielezwa kwa nadharia na hakuna vitendo?
Lowasa pamoja na ufisadi wake lakini aliweza kuthibutu katika mambo mengi magumu:

(i) alidiriki kulitafutia ufumbuzi tatizo la umeme hafi likamchafua kisiasa:
(ii) alibuni mipango mbadala ya kuzuia foleni jiji la Dar ikiwemo njia tatu na kutambua barabara za pembeni ya mjini ambazo sasa zimeshindwa kuendeklezwa;
(iii) alisimamia mpango wa ujenzi wa shule za kata na zahanati japo hazikuwa na mtizamo wa muda mrefu ikiwemo kuandaa wauguzi na waalimu;
(iii) Ndie aliesaidia kwa kiasi kikubwa kuleta ufumbuzi wa tatizo la maji kwa baadhi ya miji japo hali bado inasuasua;
(iv) aliwezesha mpango wa ruzuku za pembejeo kwa wakulima japo uzalishaji katika sekta ya kilimo haukjakaa vizuri;
(v) aliweza kuchukua maamuzi magumu ya papo hapo ikliwemo kuwafukuza watendaji wabovu pasipo kujali ni nani mwenye dhamana ya kuwachukulia hatua za nidhamu (juzi mmesikia wenyewe Mwenzake akitamba i hadharani "kama yeye angekuwa Rais angemfukuza kazi Jairo) lakini baadae tunatangaziwa amesimamishwa ili kuchunguzwa kwanza....na wanaomchunguza ni wale wale wanaoendelea kutuhumiwa kuhusika katika kashfa nyingine ikiwemo kushindwa kushauri ipasavyo kwenye suala la Richmond...
katika hayo yote hapo juu sijaona hata moja lilofanikiwa zaidi ya kuongezeka kwa gharama za umeme ( sababu kuu ikiwa ni ufisadi/fursa ya kufanya biashara), kuongeza kwa ajali barabarani, Kuongezeka kwa rushwa na wizi ( kwenye suala la ruzuku kwenye pembejeo). Kutoa maamuzi ya kukurupuka na hatima yake serikali kushindwa kesi za madai. hayo yote uliyoorodhesha hapo ni mambo ya kitaalam na si ya kisiasa na tanzania kuna wataalamu wengi sana wa nishati, ujenzi nk> tatizo la wanasiasa ni kutaka kutatua matatizo huku wakiangalia kama watapata fursa ya kufanya biashara au ufisadi kwenye kila tatizo letu. Kwenye suala la uraisi nadhani kila mtanzania ana haki ya kikatiba kugombea nafasi yeyote... Ila kwa EL itabidi ajibu swali aliloulizwa na Mwalimu JKN....mali zote kazipata wapi????
 
That time nakumbuka mkuu siku moja nilikua na appointment na Mkurugenzi mmoja wa Halmashauri nilimkuta ofisini akitetemeka na aliahirisha appointment yangu kisa next week kulikua na ziara ya Lowasa wilayani mwake.
Kumtetemekea mtu si kwamba ndio ishara ya kwamba huyo mtu anafanyakazi sana. nadhani alitetemeka kwa sababu hakujua atakuja na maamuzi gani (ya kukurupuka bila utafiti wa kutosha ) Hata chizi akiwa anakuja ofisini kwako lazima utatemeka pia
 
Tunashukru mkuu kwa makala yako iliyojaa mafundisho na maelezo yenye elimu kwa wananchi
 
Lowassa anafaa kuchunge ng'ombe na usanii Uongozi hawezi jamani na Watanzania siku wakikosea wampa uongozi wa juu Mungu apishe mbali ni dicteta zaidi ya Gadaffi na wengine. Ni mtu wa visasi na uongozi mbaya wa kutimua watu kazi kwenye mikutano ya hadhara.
 
Nikweli kabisa tatizo halikuwa la Mh. lowasa wakati ule, bali lilikuwa ni la kimfumo yaani taratibu zetu katika zoezi zima la manunuzi/mikataba hususani katika mazingira ya zarura kwa mujibu wa sheria zetu za manunuzi. na hili ni zahiri Lowasa alijitahidi sana kufanya maamuzi kwa kuangalia umuhimu wa umeme kwa uchumi wa nchi na wananchi. na kubwa zaidi tatizo hilo lilikuwa ndiyo haswa limetokea tofauti na ilivyosasa pamoja na kulijua tatizo bado nia ya dhati ya kushughulikia imekua sifuri hasa ukilinganisha na makisio mabovu yasiyokidhi haja, ambayo tumshuhudia mswada wake ukiondoshwa bungeni ili wakajipange upya.
 
Mkulu kaumia sana kuchafuka kwa jairo, ulikuwa mkono wake wa kuume toka akiwa katibu wake pale ikulu, huyu jamaa alikuwa ukitofautiana nae ni sawa na kugombana na mkuu wa kayamwenyewe. Nadili zote za mzee, huyu ndie alikuwa anasimamia. Kabla hii haija bumbuluka, alituchangisha mill. 20 kila idara na sekta ya nm. Kwa kisingizio cha semina ya wabunge, lakini semina ile haikugharimu hata 100m. Million 450 ziko wapi?
 
Back
Top Bottom