ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wakati ule alipochukua uamuzi mgumu wa kujiuzulu, alisema, " ETI KISA NI UWAZIRI MKUU" ni kama vile alikuwa mtu aliyekuwa ameshinikizwa na mtu fulani kujiuzulu ili kupisha kelele za watanzania baada ya kubaini nae alihusika katika kashfa ya Richmond.......lakini wakati ule nilidhani Lowasa alikuwa hajui analofanya kwa kukubali kwake kuwajibika hadharani akasema, ...."najiuzulu".
Wengi tulidhani baada ya kujiuzulu Mhe. Lowasa mambo ya Nishati ya Umeme katika nchi hii yata kaa vizuri kwani ni kipindi kile kile ambapo tulitangaziwa mikakati kibao Bungeni na Kwenye hotuba ya Mhe. Rais ile ambayo sasa hatuisikii ya kila mwezi kuwa tatizo la umeme litakuwa historia...
Kumbe sasa kwa fikra za wazi mnaweza kubaini tatizo halikuwa na wala sio Lowasa..., Lowasa alijitahidi kadiri ya uwezo wake kutimiza maagizo ya mkuu..haya tunayaona sasa ni yale yale yaliyomtokea Lowasa, yamemgusa Mhe. Waziri Mkuu mwingine Pinda, sasa kwa staili nyingine ya posho za kuwahonga wapitisha bajeti kwa kutaka wafunike kombe ili bajeti ya nishati ipite mabo yaendelee kama kawaida.., Awali Mhe. Waziri Mkuu alionyesha kughazabika eti haya mambo ya "posho za kulainisha maamuzi" hayapo Serikalini.
Safari hii kupitia Mtendaji Mkuu wa Wizara ile ile ya Nishati Bw. David Jairo..huyu ambae alikuwa ni Mtumishi muadilifu, mtaalamu wa Sheria, ambaye alipata kufanya kazi kwa karibu sana na Mkuu wa nchi kule IKULU akiwa ni msaidizi wa Mkuu wa Nchi chini ya Katibu Mkuu Kiongozi wa sasa (aliyetoka Wizara ya Mambo ya Nje na Mkuu wa Nchini) ambaye ametangaza kuanza hatua za kumwajibisha Jairo ili hali nafasi yake ya Ukatibu Mkuu Nishati inatangazwa kupangiwa mtumishi mwingine (Eliakim Maswi).
Hapo napo tena ni funika kombe mwaharamu apite kama ilivyokuwa kwa wale watendaji waliotajwa kuhusika na kashfa ya Richmond...(Jairo atapangiwa kazi nyingine) http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=31495
.Eti Jairo sasa anaonekana kikwazo cha upatikanaji wa UMEME, kama ilivyokuwa kwa Mhe. Lowasa, Je, ni wapi Jairo alipata ujasiri na kiburi cha wa kuandika yale aliyoandika kuziagiza taasisi anazozisimamia kama haikuwa mazoea au hakupata maagizo yoyote toka kwa mtu fulani wa juu yake?
(Waziri wake, Waziri Mkuu na Mkuu wa Nchi hawakujua haya ambayo yaliandikwa, kutumwa na kuhifadhiwa kwenye majalada ya umma kwa lengo la kuomba fedha amazo zinaingia kwenye akanuti ya taasisi nyingine ya umma kwa lengo la kuhonga watendaji)? .....Mhe, Msabaha wakati ule nae aliponzwa kwa kuandika madokezo ya kuagiza wa chini yake...lakini alipokuwa akichomoka akitoa kauli ambayo iliashiria kuwa nae aliagizwa na mkubwa wake wa kazi kufanya yale aliyofanya na wakati ule tukasema ni "Lowasa tu huyo...'
Lakini kauli za kujiuzulu kwa Lowasa nazo zilionyesha kana kwamba nae aliagizwa kufanya vile na mtu mwingine wa juu yake ...ni nani? hatukujua! (LOwasa akachafuka)!...... Sasa tumefumba macho kabisa, hatuna mjadala tena juu ya kulipa sdeni la Mrithi wa RICHMOND yaani DOWAS hasa baada ya Wakuu wa Dunia hii (Marekani) kuingilia kati kwa staili ya Symbion Power, ...........tunamjadili Jairo.....
Hatujui kumbe hapa tulipo, tunachohitaji ni umeme, umeme kwa gharama zotote zile (hayo ndio maamuzi magumu ambayo Lowasa aliyasimamia na yakamfanya aonekane hafai). Tulidhani Lowasa ndio kikwazo cha maendeleo ya nchi hii, eti kumbe hata baada ya kujiuzulu kwake bado matatatizo ni yale yale tena sasa ni mazito zaidi..tumeona bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini imeashindwa kupita kwa kile kinachodaiwa kukosa mikakati ya kuondoa tatizo la Umeme na wakati huo Katibu wake Mkuu kung'olewa kwa kashfa ya kutaka kuiwezesha bajeti hiyo ipite kimya kimya...eti sasa si Waziri Msabaha, Karamagi wala Lowasa wameshiriki katika hili sakata....