Sasa nimeelewa hoja/shida ya wana-UKAWA

Sasa nimeelewa hoja/shida ya wana-UKAWA

Kwa hiyo ni nini kinafwata hilo siyo muhimu? ila cha muhimu tu (kwa mujibu wa Lowasa/UKAWA) CCM iondoke kama nimekuelewa vizuri ndivyo ulivyomaanisha?

Mkubwa hiyo sio tu kwa mujibu wa Lowasa, hiyo ni shauku ya watu wengi! Chochote kinachofuata kitawezekana tu baada ya kuutoa mfumo uliopo sasa, ni suala la vipaumbele tu na mkakati kwamba kwa sasa cha muhimu na cha kwanza ni kuondoa kwanza mfumo uliopo.
 
Sijawahi kuona ccm wanaweweseka kama mwaka huu.
 
Mkubwa hiyo sio tu kwa mujibu wa Lowasa, hiyo ni shauku ya watu wengi! Chochote kinachofuata kitawezekana tu baada ya kuutoa mfumo uliopo sasa, ni suala la vipaumbele tu na mkakati kwamba kwa sasa cha muhimu na cha kwanza ni kuondoa kwanza mfumo uliopo.


Sasa Je kama muhimu ni kuondoa CCM tu, Na tuseme Lowasa akawa raisi wa JMT halafu ghafla akageuka kuwa Museveni (raisi wa Uganda) akafuta Upinzani na kuweka Udikteta kwa kufuta vyama vingi, akatumia Katiba iliyopo inayompa madaraka makubwa na kujimillikisha gesi na rasilimali zote yeye na wenzake tunawezaje kuirudisha tena nchi yetu ktk kwake?

Nasema hivi kwa maana mpaka sasa hivi hakuna chochote kinachoonyesha ni nini Lowasa anasimamia, ni ipi itikadi ya Lowasa/UKAWA hivyo ni kama kamari kuna kupata na kukosa ndivyo unavyotaka kusema?
Lakini kama ni hivyo huwezi kucheza kamari na Nchi hapa tunaongelea Nchi na siyo Kampuni au familia bali ni nchi yenye Watu milioni 45 sasa kutaka tu kubalisha Uongozi kwa kutegemea kamari kwangu mimi ni hiyo haitoshi!
 
Sasa Je kama muhimu ni kuondoa CCM tu, Na tuseme Lowasa akawa raisi wa JMT halafu ghafla akageuka kuwa Museveni (raisi wa Uganda) akafuta Upinzani na kuweka Udikteta kwa kufuta vyama vingi, akatumia Katiba iliyopo inayompa madaraka makubwa na kujimillikisha gesi na rasilimali zote yeye na wenzake tunawezaje kuirudisha tena nchi yetu ktk kwake?

Nasema hivi kwa maana mpaka sasa hivi hakuna chochote kinachoonyesha ni nini Lowasa anasimamia, ni ipi itikadi ya Lowasa/UKAWA hivyo ni kama kamari kuna kupata na kukosa ndivyo unavyotaka kusema?
Lakini kama ni hivyo huwezi kucheza kamari na Nchi hapa tunaongelea Nchi na siyo Kampuni au familia bali ni nchi yenye Watu milioni 45 sasa kutaka tu kubalisha Uongozi kwa kutegemea kamari kwangu mimi ni hiyo haitoshi!

Kwanza napenda nikupongeze kwamba leo umekuja na maswali muhimu ambayo yalitakiwa tujiulize sio tu kwa ukawa bali kwa ujumla wake kwamba ni kitu gani tunakitaka kwa serikali ijayo tunayotarajia kuiweka madarakani 25 October.

Pili hayo yote unayosema mgombea wa ukawa akiingia madarakani anaweza kuyafanya, mengi tayari yanafanywa na mfumo ulipopo madarakani kwa kisingizio cha demokrasia. Na hii itatuma ujumbe kwamba kumbe dhamira na nguvu ya wananchi ndio itakayoshinda milele. Hivyo basi, hata kama rais yeyote atakengeuka na yeye ataondolewa tu na wananchi kwa njia yeyote.

CCM imekua na mtaji na mazingira mazuri sana kuwafanya wananchi waikubali na kuikumbatia, matokeo yake wamekua kinyume na kufanya mengi ya yale unayoyaogopa ya kufuja na kukandamiza wananchi, ufisadi na mambo yafananayo na hayo. Hii imepelekea wananchi wasitake kabisa kitu chochote kuhusu CCM.

Na hili hata CCM wanalitambua na wanajua kabisa uchaguzi wa mwaka huu unamaanisha vita.
Mwisho kabisa, kwa hali ilivyo, hata kama ikitokea CCM ikashinda, utendaji wake hautakua kama zamani hiyo ni mojawapo ya faida za hizi harakati za mabadiliko.

Kwani kama wangetimiza wajibu wao nani ana tatizo nao? Ndio maana tumefikia mahali watu wanaona kwa huu mfumo uliopo kuendelea kushika hatam, mabadiliko yeyote hayawezekani. Na hicho ndio kimeleta shauku na dhamira ya dhati ya kuundoa kwanza madarakani.
 
Haswaaaaaaa!!!!ikafie mbali!!!
baada ya kupata shida sana kwa muda sasa kuwaelewa wafuasi wa ukawa/lowasa mwishowe nimekuja kuwaelewa ni kwamba wao wanachokitaka chama cha mapinduzi kiondoke madarakani na kinaondokaje na nani anakuja baada ya ccm kuondoka hilo kwao siyo muhimu ila cha muhimu tu ccm iondoke!

Kitu kilichokuwa kinanipa shida kuelewa ni kwamba ni kwanini maswali magumu hawataki kuyajibu? Maswali kama je, kama ccm ndiyo mbaya iweje tena muwe tayari kuwaamini watu wale wale waliokuwa ccm na wengine bado wapo wajibadilishe jina nakujiita ukawa badala ya ccm halafu mseme mnataka kuindoa ccm madarakani hamuoni kwamba mtakuwa mmefanya kazi bure?

Jibu la hili swali ni kwamba tutajua mbele kwa mbele cha muhimu ccm iondoke!

Sasa baada ya majibu kama haya basi nimeamua kuwaelewa na kutambua kwamba wana ukawa wana intelejensia ndogo na hamna kitu mtu utafanya kuwashawishi vinginevyo kwa maana hata hawako tayari kwa majadiliano yenye maswali mgumu!

Kwao haijalishi nani anakuja lkn cha muhimu ccm iondoke!
 
Back
Top Bottom