Elections 2010 Sasa Najiunga Na Chama Cha Siasa Rasmi

.....Hata mie bado nipo nipo tu, si mwanachama wa chama chochote cha siasa.......nilikuwa shabiki maandazi yaani nilikuwa nafuata upepo tu kama bendera.Hapa kweli watu mmeonyesha mwamko lakini jamani hebu muwe serious kufungua matawi mengi ya chadema hata huko vijijini hapo ndipo mtatambulika.

Nadhani hili si jukumu la Dr Slaa, Mnyika, Tundu Lisu Kitila, Baregu au Marando pekee, ni jukumu letu sote, chukua kadi ya chama, nunua bendera na sogeza chama mtaani kwako.

Ukombozi uanze sasa

Mimi ni mwanachama wa CHADEMA tangu 2004 lakini sasa natangaza rasmi kuingia kwenye siasa za majukwaani, nitagombea ubunge uchaguzi ujao
 
Uzoefu na uchungu nilioupata kupitia uchaguzi huu umenifanya niamue kuingia kilingeni, labda upinzani unakosa maandalizi majimboni, unakosa wagombea wenye uwezo na unakosa mkakati wa kisayansi kushinda

Tumeiacha kazi ya kupigania taifa hili kwa akina Tundu lisu, well tumechangia mawazo, muda na pesa lakini tumesahau kuwa tunapaswa kuingia kilingeni na kupambana na Dhuluma kwa taifa hili.

Nilichojifunza toka kwa wananchi ni kwamba, Ukijiandaa na ukijipanga unaweza kushinda na kila ushindi wa CHADEMA ni pigo kwa CCM, jamani tuamke, Twende majimboni tuanze kujiandaa 2015.

Kuna baadhi ya wagombea wa CHADEMA hawafanani na Chama hasa wale wanaotoka CCM, Heshima kwa SHIBUDA lakini wengi toka CCM hawasaidii CHADEMA. Tunahitaji kutengeneza wagomea wetu, vijana wasomi na wenye uelewa maana wapo wasomi wa aina ya Willium Malecela. Hapana nasungumzia watu kama Mnyika, Mdee, nk....

Lets go out, lets create a network now, lets start fundrising, lets take them out. tutumie uzoefu wa akina Mnyika, Mdee, Zito Kabwe (Hata kama simfahamu vizuri siku hizi tofauti na zamani) Kafulila David, Regia (hata kama Kaibiwa) Tundu Lisu nk kukomboa taifa hili
 
sikuwa na chama chochote bali kura yangu nimekuwa nikiwapa Chadema nami natangaza kujiunga rasmi na Chadema ili tukafungue matawi zaidi na kutoa elimu ya uraia hasa kwa ndugu zetu vijijini. Nitaangalia hatua zipatazo kufuatwa ili kuwa mwanachama. Chadema Juuuuuuuuuuuuuuu!:fencing::lalala::fencing::smile-big:
 
du na mimi natangaza rasmi kujiunga na chadema, ndio chama pekee kinachoweza kurudisha tumaini lililopotea la watanzania. tushirikiane ktk hili jamani. PEOPLEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEES
 
.....Hata mie bado nipo nipo tu, si mwanachama wa chama chochote cha siasa.......nilikuwa shabiki maandazi yaani nilikuwa nafuata upepo tu kama bendera.Hapa kweli watu mmeonyesha mwamko lakini jamani hebu muwe serious kufungua matawi mengi ya chadema hata huko vijijini hapo ndipo mtatambulika.
Preta huu ni ukweli kabisaaaaaaa. Hili limekuwa ni wazo langu wakati mchakato wa uchaguzi ulipokuwa ukiendelea. Nafikiri sasa nitawajibika kuchukua likizo na kuzamia vijijini ili kufungua matawi mengi kuliko ilivyofikirika. I need partners who are ready to support me.
Nitawasiliana na ofisi za mkoa nikapate kadi na bendera na kuzamia vijijini. Najua mwezi mmoja unaweza kunitosha kufungu hundreds of branches in my area. Mwaka 2015 uchaguzi utakuwa tofauti sana. Nyerere wakati anaanzisha Tanu haikuwa rahisi. Alitembea sana.
Shime wana Chadema uchungu wa nchi yetu utusukume kufanya zaidi 2015 tutakuwa tunatisha. We need solidarity.
 
hata mimi ccm nilikuwa naichukia toka kipindi cha mageuzi nikawa mwana nccr baada ya kutuvuruga nikaacha na kurudi ccm lakini sasa kutokana hali hii nimeichana kadi ya ccm.Hapa nilipo nataka kadi ya chadema sijui nitapataje sasa hivi nipo belgium masomo
Tembelea Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa maelezo zaidi na mawasiliano ya jinsi unavyoweza kuwa mwanachama. Ukishindwa ni PM
 
Mimi nina kadi ya CCM toka 1986. Niliipata mkoani Iringa. Sijawahi ilipia. Ni mwanachama mfu, kama Dr. Azaveli.

Sasa nataka kuwa active member wa Chadema.
Nimetoa baadhi ya maelekezo ya jinsi ya kuwa wanachama. ukishindwa ni PM nikusaidie.
 
Mwaka 2015 hakuna hata mtu atakayepita bila kupingwa lazima kuwa na wagombea wazuri na wanaofahamika katika kila jimbo. kazi ya kuelimisha wananchi na kueleza sera na mipango ya chama lazima ianze leo na si kesho. Nami, kwa rehema ya Mwenyezi Mungu, nitakuwa katika kinyang'anyiro hicho nadhani hilo jimbo la Kinondoni litanifaa. Kitaeleweka

Ushapata maumivu ukiwa jukwaani... Sasa jaribu maumivu ukiwa ndani ya uwanja! Teh teh teh!!!!
 
Nami pia! Nilidhani ktk maisha yangu sitakuwa mwanachama wa chama chochote, lakini natangaza rasmi kuwa sasa natafuta utaratibu wa kujiunga na CHADEMA!

Sasa unafikiri ukichukua kadi ndiyo kura yako itahesabika mara mbili ama vipi?
 
Good luck... Ukishindwa huko sikuzote mlango wa ccm upo wazi.. Hatuna kinyongo..
 
WATANZANIA NA HASA CHADEMA TWENDENI VIJIJINI ILI TUWEZE KIOKOMBOA HII NCHI KWA UHAKIKA ZAIDI MAANA HUKO NDIO KUNA WATU WENYE DAMU YA AJABU.NAUNGA MKONO HOJA:WATANZANIA TUAMKE WAKATI NDIO HUU:bowl::smile-big:
 
Back
Top Bottom