Makamanda CDM Wote acheni kujadili hawa vibaraka wa CCM-ACT, kikubwa tupange mikakati ya ushindi. Kuendelea kuwajadili hawa wasaliti ni kupoteza wakati bure.
Rai yangu; Elimu ni muhimu kwa wanachi, kila kamanda awe mjumbe kwa jirani yake katika kumng'oa mkoloni mweusi huyu CCM na vibaraka wake.
MUNGU nibariki Mimi pamoja na familia yangu.
Wenye vyeti vya CCM tunaruhusiwa kuchoma na kuja huko au hatutakiwi?
Ni sawa na ngoma ivumayo sana...! Tangu lini ngozi ya kitimoto ikawamba ngoma? Shy land wee ni mshkaji wangu sana tu hapa JF lakini kwa hili nina maoni tofauti
Kwanza ni dhambi kabisa tena ni kejeli kubwa kwa Zito kujilinganisha na Nyerere R.I.P, Mwalimu hakujijenga binafsi na alipigania ukombozi wa kweli wa taifa hili, mwalimu hakuwa na tamaa ya Mali na alikuwa na maono
Zito ni mbinafsi, hii ni hulka yake hashauriki na haambiliki, yeye anajiona ni bora zaidi na popote alipo na chochote anachofanya hupenda kuwa juu/ kujikweza
Zito si mnyenyeku na akifanya hivyo hufanya kwa manufaa binafsi
Zito si mtu wa kutaka changamoto, kitu ambacho kitamgharimu hata huko ACT,
Kwasasa yupo HONEYMOON!kila kitu ni shangwe tu. Fungate hili likiisha akatulia ofisini ajenge chama ndipo hapo tutakaposhuhudia maajabu! Ni suala la muda tuu..!!!
Wanaharakati na watanzania wote ambao tunapenda maendeleo na demokrasia ya kweli tulioachana na chama cha ubaguzi na uchu wa madaraka.
Naomba tukutane hapa ili tuweze kushauriana namna yakuendelea na propaganda na ajenda zetu zuri za kimaendeleo katika jamii, lengo kubwa ni kukieneza chama chetu kipya cha ACT ili kiweze kujipambanua wazi kwa wanainchi katika harakati zake za kuwatetea wananchi ambao tangu wapate uhuru wamekosa fursa yakuvitumia maliasili za nchi yao kama ipasavyo.
Karibuni wote ili tuendeleze mikakati ya kulikomboa taifa letu, na hapa hapa tutapata fursa ya kutambuana wanaharakati wote tuliomo humu jamvini.
Karibuni sana.
Shy land hatuwezi kufanana wala kukubaliana kwenye kila kitu, lakini pia ni mapema mno kuweza kujua ACT kitakuwa chama cha aina gani hasa ukiangalia historia ya kuanzishwa kwakeKwa hiyo hata wewe ndugu yangu mshana jr pamoja na uwezo wako mkubwa wa kufikiri bado unaubia na chama cha ukabila.
chama kimoja kimeanzishwa kwa ajili ya kugawanya upinzani na hiyo ni ajenda yake kuu ili kufanikisha kuendelea na majoka wa makengeza na wao wakiwa wanufaika. Hiyo vita ni dhahiri
Shy land hatuwezi kufanana wala kukubaliana kwenye kila kitu, lakini pia ni mapema mno kuweza kujua ACT kitakuwa chama cha aina gani hasa ukiangalia historia ya kuanzishwa kwake
Labda tusubiri mwakani tar kama ya Leo tuone!!! Iweke kwenye kumbukumbu zako nami nitafanya hivyo
ACT ni ujinga na kujitoa uewela. Eti uzalendo, nani mzalendo, uzalendo hauji kwa kuuandika kwenye katiba au kuutamka bali matendo. ZZK ni kama Augustn Mrema na hoja zake za kukamata dhahabu airport eti huo ni uzalendo, uzalendo ni dhana pana sana.
Ni sawa na ngoma ivumayo sana...! Tangu lini ngozi ya kitimoto ikawamba ngoma? Shy land wee ni mshkaji wangu sana tu hapa JF lakini kwa hili nina maoni tofauti
Kwanza ni dhambi kabisa tena ni kejeli kubwa kwa Zito kujilinganisha na Nyerere R.I.P, Mwalimu hakujijenga binafsi na alipigania ukombozi wa kweli wa taifa hili, mwalimu hakuwa na tamaa ya Mali na alikuwa na maono
Zito ni mbinafsi, hii ni hulka yake hashauriki na haambiliki, yeye anajiona ni bora zaidi na popote alipo na chochote anachofanya hupenda kuwa juu/ kujikweza
Zito si mnyenyeku na akifanya hivyo hufanya kwa manufaa binafsi
Zito si mtu wa kutaka changamoto, kitu ambacho kitamgharimu hata huko ACT, akitokea mwanachama atakayepingana na misimamo yake ndipo hapo rangi zake halisi Zitakapoonekana
Kwasasa yupo HONEYMOON!kila kitu ni shangwe tu. Fungate hili likiisha akatulia ofisini ajenge chama ndipo hapo tutakaposhuhudia maajabu! Ni suala la muda tuu..!!!
Mpwa naomba nikuulize swali
Je baada ya zito kukutwa na hatia akafukuzwa chama ALITAKIWA KUFANYA NINI?
Mpwa naomba nikuulize swali
Je baada ya zito kukutwa na hatia akafukuzwa chama ALITAKIWA KUFANYA NINI?
Simple answer
Jr kakuambia si mnyenyekevu so hawez kunyenyekea anapokosa jhakubali changamoto ndio maana anabaki ktk wingu la fikra zake tu
Si muungwana maana muungwana ni vitendo hayo ya leo huko act tuliyajua kabla hata alipoulizwa alikuwa akikataa but leo anaongoza jahaz linalotegemea upepo bila weledi
Wakat akiwa kwenye kampen zake za ubunge mwaka 2010 aliwaambia ndio mwisho wake kugombea ubunge atakapo kuja tena atakuwa anaomba kura za urais. Hata kama chadema isingeandaa hatua za kinidhamu zilizochukuliwa awali kabla hajenda mahakaman angetafuta namna tu aondoke chadema ili agombee urais wake huo wa mkoa wa kigoma.
Kweli vikao vya zito na kizoka pamoja na wasira vimefanikiwa, hata zile pesa za crdb mtaa wa azikiwe ulizochukua kweli zimekufanya ukageuka adui ktk mioyo ya wtz makini but shujaa Kwa wapuuz wanaokupaka mafuta Kwa mgongo wa chupa kama samson