Baada ya CDM kuonyesha ukomavu wa kisiasa wa kuwafukuza wanachama wake pasi na kuogopa umaarufu wake,na kukiacha chama cha CCM kikitoa maagizo yasiyoambatana na vitendo (matishio au tishia nyau) Imedhihirika kuwa hiki chama chatakiwa kukabidhiwa dola na kinaweza fanya maamuzi magumu yanayo hitajiwa na wananchi. Watu wanaiba mali ya umma wanachekewa tu, mikataba mibovu inaingiwa na inakuwa ya siri sisi twacheka tu, tembo wanauwawa sisi tunaangalia tu, eti wauza unga tunawafahamu lakini kwa vile ni wenzetu tuna waangalia tu!Umeme unapanda sisi tuko na stori za Zitto tu. Katiba mpya kwa sasa si ajenda kwetu ila makala za CDM tu. Sasa nimetambua kumbe hakuna maisha bila CHADEMA hii nimedhihiri kuwa inasemwa sana kwa vile ndio uhai wa wananchi. SASA MIMI NA FAMILIA YANGUMAMBO YAKO CHADEMA.Nahitaji kadi.