Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,909
- 945
Mbunge wa jimbo la Urambo mkoani Tabora, Margaret Sitta ameiomba Serikali kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu hususani wale wanaoishi maeneo ya vijijini kwa kuwa wanakumbana na kadhia ya kutembea umbali mrefu na adha ya mvua waendapo kufundisha.
Akichangia hoja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bungeni jijini Dodoma amesema kwa kuwa mara nyingi Wananchi wakiungana na Serikali inakuwa jambo jepesi kupatikana kwa shule, suala la Walimu kukaa mbali na shule nalo litazamwe kwani ni muhimu nao kuishi karibu na shule hizo.
Mbunge huyo wa Urambo ametolea mfano kwenye uanziashwaji wa shule shikizi kwa kusema huwa zinapatikana mahali ambapo ni sehemu hapakuwa na shule kwa umbali mrefu sana na vijiji vilipo, hivyo Wananchi wakishirikiana na Serikali shule huanzishwq na wanafunzi wanaanza kusoma japokuwa walimu hawajulikani wataishi wapi ili wahudumie Wanafunzi hao.
Akichangia hoja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bungeni jijini Dodoma amesema kwa kuwa mara nyingi Wananchi wakiungana na Serikali inakuwa jambo jepesi kupatikana kwa shule, suala la Walimu kukaa mbali na shule nalo litazamwe kwani ni muhimu nao kuishi karibu na shule hizo.
Mbunge huyo wa Urambo ametolea mfano kwenye uanziashwaji wa shule shikizi kwa kusema huwa zinapatikana mahali ambapo ni sehemu hapakuwa na shule kwa umbali mrefu sana na vijiji vilipo, hivyo Wananchi wakishirikiana na Serikali shule huanzishwq na wanafunzi wanaanza kusoma japokuwa walimu hawajulikani wataishi wapi ili wahudumie Wanafunzi hao.