Samia scholarship itumiwe kwa dhati kulivusha taifa

Samia scholarship itumiwe kwa dhati kulivusha taifa

mkwelitu

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2026
Posts
551
Reaction score
791
Katika taarifa ya kipindi cha Nipashe leo asubuhi hii, toka radio one, imeripotiwa Serikali itafafadhili vijana 1050 watakaosoma masomo ya science ndani na nje ya Nchi.

Taarifa hiyo imeeleza vijana 1000 watasoma ndani ya Nchi masomo mbalimbali ya sayansi na 50 nje ya Nchi.

Kwanza naipongeza Serikali kuja na mkakati huu, ikiwa tu utakuwa makini, usio na upendeleo wa kisiasa, kidini au kifamilia.

Naelewa tumechelewa sana tangu Mwl Nyerere aliposomesha bure tangu chekechea hadi PhD lakini baadae Serikali ya mwinyi ikaweka malipo kwa elimu ya Secondary hadi chuo kikuu.

Hatujachelewa ikiwa tuna utashi wa kweli.
 
Apa ndani kuna mambo gani ya kisayansi yaliyopo na je kuna mwanasayansi gani mu AFRIKA na mtanzania? (tuanzie apo kwanza)
 
Wamebadilisha jina la mikopo kuwa samia scholarship. Samia Extended scholarship pekee ndio scholarship inayotolewa SUZA na NM AIST
 
Wamebadilisha jina la mikopo kuwa samia scholarship. Samia Extended scholarship pekee ndio scholarship inayotolewa SUZA na NM AIST
Kumbe ???

Hata hivyo bado ni njema, ila tu wasiingize siasa zao kwenye taaluma na elimu kuharibu.
 
Katika taarifa ya kipindi cha Nipashe leo asubuhi hii, toka radio one, imeripotiwa Serikali itafafadhili vijana 1050 watakaosoma masomo ya science ndani na nje ya Nchi.

Taarifa hiyo imeeleza vijana 1000 watasoma ndani ya Nchi masomo mbalimbali ya sayansi na 50 nje ya Nchi.

Kwanza naipongeza Serikali kuja na mkakati huu, ikiwa tu utakuwa makini, usio na upendeleo wa kisiasa, kidini au kifamilia.

Naelewa tumechelewa sana tangu Mwl Nyerere aliposomesha bure tangu chekechea hadi PhD lakini baadae Serikali ya mwinyi ikaweka malipo kwa elimu ya Secondary hadi chuo kikuu.

Hatujachelewa ikiwa tuna utashi wa kweli.
Mwambieni mama yenu aache kujikomba komba kwa wananchi, what is samia scholarship! Kwani pesa ni zake? Kwa nini pesa, isiwekwe Bodi ya mikopo, Mambo ya kipuuzi sana haya, kama anataka kujisafisha, aende yeye,thabit, gilshoni kwenye talk to Al Jazeera,au BBC, wakahojiwe na manguli sio kujificha uwani
 
Mwambieni mama yenu aache kujikomba komba kwa wananchi, what is samia scholarship! Kwani pesa ni zake? Kwa nini pesa, isiwekwe Bodi ya mikopo, Mambo ya kipuuzi sana haya, kama anataka kujisafisha, aende yeye,thabit, gilshoni kwenye talk to Al Jazeera,au BBC, wakahojiwe na manguli sio kujificha uwani
Iwekwe kwenye board ya mikopo au ibakie Samia scholarship, hoja yangu kwa Serikali ni kutochanganya elimu, technology na mambo yao ya siasa.
 
Kumbe ???

Hata hivyo bado ni njema, ila tu wasiingize siasa zao kwenye taaluma na elimu kuharibu.
Watu wanawaza vitu vya ajabu wanaita scholarship alafu mhitimu akimaliza chuo anailipa kama mkopo. Ibakie kama mkopo ili watu wafahamu ukweli, scholarship hupaswi kurudisha ulichotumia.
 
Watu wanawaza vitu vya ajabu wanaita scholarship alafu mhitimu akimaliza chuo anailipa kama mkopo. Ibakie kama mkopo ili watu wafahamu ukweli, scholarship hupaswi kurudisha ulichotumia.
Ikiwa ni mkopo, usemacho uko sahihi.
 
Back
Top Bottom