Kaka bei hio bei! Mimi mbongo sio mtalii kaka, mbona bei kali sana?!1.6M mkongo
Ficha umasikini wako na uswahili wakoKabati la milango miwili laki6??
Linakuja na sambusa za nyama ndani?
Ebu tuongee faragha, ni Inbox Please..Bei ya mbao imesimama kaka, naweza kukuambia mkongo halafu nikaweka mtondolo baadae ukaniona mimi tapeli..
Achana nayeTatizo sio sambusa za nyama, unataka kitu kizuri cha kupendeza nyumbani kwako![]()
Sio yeye uyoNilishayaona, lakin nlivoona post yako ya sambusa n nyama kuhusiana n kabat tulizoziona... Then nkajaribu kucompare io avatar n post uloitoa nkapata jibu kuwa haviendan kbsa.... Ndo nkakuuliza io avatar kam ni real ww
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani umelazimishwa kununua?We mleta mada itakua ulidanganywa kuhusu jamiiforums, uliambiwa members wote ni millionaires ndo maana unakuja na bei za ajabu ajabu.
We maisha ya kibongo ninunue kitanda laki 9? Au hujui bidhaa zako unamlenga mteja gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu zuri sasa state itakuwa AQUEOUS au SOLID?MBFH20
Sent from my Phillips Savvy using JamiiForums Mobile App.
Tukienda na Ukweli
Watanzania wengi hasa hawa wajisiriamali wanapenda over price bidhaa zao...
Wachonga SAMANI wengi wao design zao ni mbovu, finishing ni mbaya sana
Makabati mengi 98pc yamewekwa plywood kwa nyuma ambazo ni rahisi kuvunjika....
Vioo vimekuwa attached na vimsumari vidogo vile
Door handles nyingi huvunjika mapema kuliko.....
Kama ni kochi basi tegemea kukalia mbao kwenye sehemu ya kuegemea utaegemea mbao,
Kama ni ngozi basi jua itapauka mapema sana
Wengi wanaigana
Vitanda design yao ni hiyo hiyo mara nyingi vingi wameachanisha mbao kama hicho hapo juu.
Ukija kwenye kitanda cha chuma nacho ni kerooo vyuma kupata kutu ni upesi sana,
kwenye vitanda zile chaga zenu mmmmmh
Kwenye meza ya chakula wanapaka vanish nyingi unakuta kitu kinangaaa ile kishamba shamba
Jaribuni kwenda shule mjifunze design nzuri na finishing nzuri.
Wachina wanauza sana sababu wamepunguza bei vitu vyao, hivyo na nyinyi tengenezeni vitu ili muuzie watu wengi na sio kuuza bei ghali afu unajikuta wapata mteja 1 tu
Pia tembeleeni watu wengine muone finishing zao zilivyo nzuri
Umewahi kutazama vitu ninavyotengeneza au unaongelea mafundi kwa ujumla, ungewahi kuona hata kitu kimoja tuu nilichotengeneza ningeweza kukuelewa, finishing yangu ukiiona utasema ni ya hao unaowatukuza(wachina), tembea uone sio unaongea tuu. Njoo nikuoneshe bidhaa zangu sibahatishi najiamini na kama upo Dar ntakulipia nauli uje ofisini kwangu
Mafundi sijui mna tatizo gani mtu akiwakosoa mnaona ni tatizo kubwa sana kukosolewa
Kama huwezi kufanya production inayoendana na market jua kabisa ni sawa unakua muimba hip hop Bongo ilihali mashabiki wako hawanunui mziki wako zaidi ya kukusifia kwenye vijiwe vyao vya bangi.Kosoa kama kuna ukweli, unafikiri ubora wa kazi unatokana na maneno? Nikuchaji pesa nyingi kwa quality mbovu? Ukiambiwa kitanda 1M unang'aka ukiambiwa laki tatu unusu unakubali, nani akutengenezee kitanda kizuri kwa laki 3.5 yako, nakulipulia tuu utajua mwenyewe mbele ya safari.. Tengeneza kitu kizuri mteja mwenyewe ukimtajia bei anakua haamini kama umetengeneza wewe au umeagiza.. Anyway, karibu tutembelee siku moja utayaamini maneno yangu
Kama huwezi kufanya production inayoendana na market jua kabisa ni sawa unakua muimba hip hop Bongo ilihali mashabiki wako hawanunui mziki wako zaidi ya kukusifia kwenye vijiwe vyao vya bangi.
Usiwe mkali mkuu, wachina hawashindwi kutengeneza vitu expensive kama vyako, wala hawashindwi kutengeneza vitu vizuri kama unavyodai wewe, tatizo ni kwamba who buys your products?
Je product yako inaendana na market?
Fanya sensa ndogo tu, watu wangapi mtaani kwako wanamudu kununua kitanda cha laki 9? Uwe mkweli tu, kama unafanya biashara kujifurahisha its fine endelea.
Mwisho wa siku naomba uweke picha ya kabati la vyombo kubwa lenye kuanzia milango mitatu na useme ni bei gani kama namudu ntakupigia tufanye biashara.
Acha porojo weka bei ya nilichokuulizaSijaanza leo hii biashara, ingekuwa hivyo unavyosema ningerudi kijijini muda mrefu sana, najiamini na ndio maana hata wateja wangu ni watu wa kawaida sana ila wanapenda vitu vizuri