Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,016
- 9,885
Salama Jabiri "Ecejay"
Nilimfahamia kwenye kipindi cha Planet Bongo ambacho kiliurithi moto wa Hip Hop Base HOP kutoka kwa mwana Hip Hop, Saigon ambaye alikifanya kwa namna ya tofauti, kisha Salama akakiacha kwenye mikono ya Abdallah Khamis Ambua " Dulla Planet" ambaye naye akakibadilisha na kukifanya kwa namna yake mpaka kupewa wiki nzima (Jumatatu mpaka Ijumaa).
Akiwa hapohapo East Africa TV, alipita kwenye kipindi kiitwacho Friday Night Live (FNL) ambacho kilitupa ladha za watangazaji wengine kama Ssebo, Jimmy Kabwe (JK), Sam Misago, na wengineo.
Akatemana na utangazaji na kuendelea na mishe nyingine lakini baadaye akakaa chimbo na AY na Josh na kuibuka na kipindi maarufu cha Mahojiano kilichoitwa Mkasi.
Akaibuka na segment ya kuzungumzia kabumbu na baada ya hapo akaibuka na Salama na.
Salama alisifika sana kwa ukosoaji wa videos na nakumbuka mwaka 2006 alimchana QJ kwenye ngoma yake ya Sifai kuwa alivaa tisheti ya mikono mifupi na kuonesha kiwiko ambacho kilipauka.
Videos nyingi zilipitiwa na alikumbana na misukosuko MINGI. Bila shaka, ukiniambia nikutajie mtu ambaye amekuza thamani ya videos za Muziki wetu basi nitasema ni Salama.
Nilikuwa nikisikia tu kuwa kuna "mmama" wa kizungu ambaye Salama anamgeza kuanzia uvaaji na mtindo wake mzima wa maisha wa kujiweka kama mwanaume. Nikajua ni kamba tu, nilipomwona Ellen Degeneres kwenye kipindi chake kiitwacho The hellen Show ndipo nilipoamini kwamba kila mtu ana anayefanana naye kwenye dunia hii.
Salama amesikika kwenye intro ya wimbo wa Jay Moe unaoitwa Tutakukumbuka, wimbo ambao Moe aliuandika baada ya kifo cha Mutie Rodney Abraham Mengi.
Salama alisikika kwenye intro ya Agost 13 ya Fid Q na nilimsikia Fid akisema kwamba Majani alimzingua sana kwamba inakuwaje anawapeleka watu ambao ni "Miyeyusho" studioni lakini Fid akasisitiza kuwa angefanya kitu poa, Majani akakata kamba na Salama akafanya alichokifanya.
Salama aliwahi kushindanishwa na Fatma Hassan "Fetylicious, DJ Fetty" wa Clouds FM lakini wawili hao hawakuwahi kulumbana na zaidi ni " wana" Ila kiukweli wawili hawa walielekeana kwa vingi; jinsia, maumbo, vionjo vyao vya kipekee wakiwa hewani, maswali chokozi na chonganishi na uchangamfu wakiwa nyuma ya mic. Nilitamani sana kuwasikia wakitangaza pamoja.
Akimhoji Adam Mchomvu, Salama alisema alifuatwa na Ruge ili ahamie Clouds lakini alipotaja dau alilolitaka, wakashindwana.
KALI ZA KUSISIMUA KUHUSU SALAMA
1. Kutekwa na Kikosi (Pina) kwa sababu ya kuponda video yao, halafu akanyolewa nywele na kushindwa kutokea kwenye kipindi. Je ilikuwa kweli hii?
2. Kuwa na mtoto na kumficha Sauzi. Je ni kweli hii??
3. Salama ni shabiki wa timu "nyekundu" hivyo umeshajua kwa wale pacha wa Kariakoo, anashabikia timu gani.
4. Salama alidaiwa kuwa aliwahi kutoka na Fid. Wengine walidai Salama alimtoa Fid nishai kwa ule mwonekano wake wa zamani na ndiye aliyechochea Fid kubadilika, lakini pia Salama alimponda Ngosha kuwa alivaa mguo wa kulalia kwenye video ya Hapo vipi ya Prof. Jay, Je ni kweli? Lakini Nikki Mbishi ana line inayosema, "Mkasi haukukata rasta za kubanda " Kuna uhusiano na nilichokiuliza.
5. SALAMA aliiponda Bongo Star Search kwa kila kitu. Madam Ritha Paulsen akapata habari hiyo na kukutana na Salama akiwa amefura kama mbogo.
Walipokutana, Salama akabaki na msimamo wake na kumpa ramani nzima Ritha ya namna ambavyo BSS ilitakiwa kuwa.
Ritha akafurahi na kumpa shavu Salama na kuanzia hapo Salama amekuwa jaji wa mashindano hayo ya kuibua vipaji mpaka leo.
Usiogope kukosoa kwa kuogopa kukosea, usiogope kukosoa unapoona upo sahihi, unaweza kuinuka kwa ukosoaji wako.
Napenda Kiswahili chenye marashi ya Zenji, napenda Kiingereza chake, napenda " kauli kubwa" anazozitoa akivurigwa, napenda vile anavyoonesha hisia zake halisi pasipo kujali utajisikiaje. Napenda vile alivyo.
Napenda namna alivyoulinda mwonekano wake na kuonekana "Forever Young"
Nampenda Salama.
Una kipi cha kusema kuhusu Salama?
Nilimfahamia kwenye kipindi cha Planet Bongo ambacho kiliurithi moto wa Hip Hop Base HOP kutoka kwa mwana Hip Hop, Saigon ambaye alikifanya kwa namna ya tofauti, kisha Salama akakiacha kwenye mikono ya Abdallah Khamis Ambua " Dulla Planet" ambaye naye akakibadilisha na kukifanya kwa namna yake mpaka kupewa wiki nzima (Jumatatu mpaka Ijumaa).
Akiwa hapohapo East Africa TV, alipita kwenye kipindi kiitwacho Friday Night Live (FNL) ambacho kilitupa ladha za watangazaji wengine kama Ssebo, Jimmy Kabwe (JK), Sam Misago, na wengineo.
Akatemana na utangazaji na kuendelea na mishe nyingine lakini baadaye akakaa chimbo na AY na Josh na kuibuka na kipindi maarufu cha Mahojiano kilichoitwa Mkasi.
Akaibuka na segment ya kuzungumzia kabumbu na baada ya hapo akaibuka na Salama na.
Salama alisifika sana kwa ukosoaji wa videos na nakumbuka mwaka 2006 alimchana QJ kwenye ngoma yake ya Sifai kuwa alivaa tisheti ya mikono mifupi na kuonesha kiwiko ambacho kilipauka.
Videos nyingi zilipitiwa na alikumbana na misukosuko MINGI. Bila shaka, ukiniambia nikutajie mtu ambaye amekuza thamani ya videos za Muziki wetu basi nitasema ni Salama.
Nilikuwa nikisikia tu kuwa kuna "mmama" wa kizungu ambaye Salama anamgeza kuanzia uvaaji na mtindo wake mzima wa maisha wa kujiweka kama mwanaume. Nikajua ni kamba tu, nilipomwona Ellen Degeneres kwenye kipindi chake kiitwacho The hellen Show ndipo nilipoamini kwamba kila mtu ana anayefanana naye kwenye dunia hii.
Salama amesikika kwenye intro ya wimbo wa Jay Moe unaoitwa Tutakukumbuka, wimbo ambao Moe aliuandika baada ya kifo cha Mutie Rodney Abraham Mengi.
Salama alisikika kwenye intro ya Agost 13 ya Fid Q na nilimsikia Fid akisema kwamba Majani alimzingua sana kwamba inakuwaje anawapeleka watu ambao ni "Miyeyusho" studioni lakini Fid akasisitiza kuwa angefanya kitu poa, Majani akakata kamba na Salama akafanya alichokifanya.
Salama aliwahi kushindanishwa na Fatma Hassan "Fetylicious, DJ Fetty" wa Clouds FM lakini wawili hao hawakuwahi kulumbana na zaidi ni " wana" Ila kiukweli wawili hawa walielekeana kwa vingi; jinsia, maumbo, vionjo vyao vya kipekee wakiwa hewani, maswali chokozi na chonganishi na uchangamfu wakiwa nyuma ya mic. Nilitamani sana kuwasikia wakitangaza pamoja.
Akimhoji Adam Mchomvu, Salama alisema alifuatwa na Ruge ili ahamie Clouds lakini alipotaja dau alilolitaka, wakashindwana.
KALI ZA KUSISIMUA KUHUSU SALAMA
1. Kutekwa na Kikosi (Pina) kwa sababu ya kuponda video yao, halafu akanyolewa nywele na kushindwa kutokea kwenye kipindi. Je ilikuwa kweli hii?
2. Kuwa na mtoto na kumficha Sauzi. Je ni kweli hii??
3. Salama ni shabiki wa timu "nyekundu" hivyo umeshajua kwa wale pacha wa Kariakoo, anashabikia timu gani.
4. Salama alidaiwa kuwa aliwahi kutoka na Fid. Wengine walidai Salama alimtoa Fid nishai kwa ule mwonekano wake wa zamani na ndiye aliyechochea Fid kubadilika, lakini pia Salama alimponda Ngosha kuwa alivaa mguo wa kulalia kwenye video ya Hapo vipi ya Prof. Jay, Je ni kweli? Lakini Nikki Mbishi ana line inayosema, "Mkasi haukukata rasta za kubanda " Kuna uhusiano na nilichokiuliza.
5. SALAMA aliiponda Bongo Star Search kwa kila kitu. Madam Ritha Paulsen akapata habari hiyo na kukutana na Salama akiwa amefura kama mbogo.
Walipokutana, Salama akabaki na msimamo wake na kumpa ramani nzima Ritha ya namna ambavyo BSS ilitakiwa kuwa.
Ritha akafurahi na kumpa shavu Salama na kuanzia hapo Salama amekuwa jaji wa mashindano hayo ya kuibua vipaji mpaka leo.
Usiogope kukosoa kwa kuogopa kukosea, usiogope kukosoa unapoona upo sahihi, unaweza kuinuka kwa ukosoaji wako.
Napenda Kiswahili chenye marashi ya Zenji, napenda Kiingereza chake, napenda " kauli kubwa" anazozitoa akivurigwa, napenda vile anavyoonesha hisia zake halisi pasipo kujali utajisikiaje. Napenda vile alivyo.
Napenda namna alivyoulinda mwonekano wake na kuonekana "Forever Young"
Nampenda Salama.
Una kipi cha kusema kuhusu Salama?