Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,815
- 4,565
Wawakilishi wa Mchezaji Pape Ousmane Sakho hawaridhishwi na kukosekana kwa muda wa kucheza kwa Mteja wao ndani ya Simba, wakiamini Msenegal huyo anastahili muda zaidi wa kucheza.
Kutokana na hilo kwa mujibu wa taarifa nilizopata ni kuwa kuna baadhi ya ofa watazifikisha Msimbazi kumhusu Mteja wao ambazo zitakuwa na maslahi kwa Simba kiuchumi ili POS aweze kuondoka kusaka changamoto mpya.
Sakho alisaini kandarasi ya miaka mitatu na Wekundu wa Msimbazi, akiwa ametumikia miaka miwili huku kipengele cha mkataba kikimtaka alipe mshahara wa miezi mitatu tu ili avunje mkataba wake, tayari ameshaandika barua.
Wanaamini Kijana anastahili muda wa kucheza zaidi, ijapo mpaka sasa bado hakuna ofa mezani kwa Simba huku zikitarajiwa mwishoni mwa msimu.
Mchezaji mwingine aliyeomba kuondoka Simba ni Mzambia Mosses Phiri, ambapo wanakuwa ni wachezaji watatu mpaka Sasa hivi baada ya Awali Joash Onyango kuandika barua ya kuondoka klabuni hapo.
Kutokana na hilo kwa mujibu wa taarifa nilizopata ni kuwa kuna baadhi ya ofa watazifikisha Msimbazi kumhusu Mteja wao ambazo zitakuwa na maslahi kwa Simba kiuchumi ili POS aweze kuondoka kusaka changamoto mpya.
Sakho alisaini kandarasi ya miaka mitatu na Wekundu wa Msimbazi, akiwa ametumikia miaka miwili huku kipengele cha mkataba kikimtaka alipe mshahara wa miezi mitatu tu ili avunje mkataba wake, tayari ameshaandika barua.
Wanaamini Kijana anastahili muda wa kucheza zaidi, ijapo mpaka sasa bado hakuna ofa mezani kwa Simba huku zikitarajiwa mwishoni mwa msimu.
Mchezaji mwingine aliyeomba kuondoka Simba ni Mzambia Mosses Phiri, ambapo wanakuwa ni wachezaji watatu mpaka Sasa hivi baada ya Awali Joash Onyango kuandika barua ya kuondoka klabuni hapo.