Simba: Tuko mbioni kuilipa fedha Teungueth ya Senegal kwa ajili ya Sakho ili kujiepusha na kadhia ya kufungiwa kusajili

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,115
Muda mfupi baada ya kutangazwa kwa uamuzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kuifungua Simba SC kusajili mpaka itakapolipa madai ya klabu ya Teungueth ya Senegal kuhusu Mchezaji Pape Ousmane Sakho, klabu ya Simba imesema ilimuuza Mchezaji Sakho kwa klabu ya Quevilly Roven Metropole ya Ufaransa mwezi August 2023 na kwamba makubaliano ya malipo ni ya awamu mbili.

“Malipo ya awamu ya kwanza (50%) yalilipwa tarehe 2 October 2023 , Klabu ya Simba ilikuwa inasubiri awamu ya pili ili kuilipa asilimia 15% ya mauzo kwa klabu ya Teungueth ya Senegal”

“Klabu ya Simba inakiri kuwa kulikuwa hakuna mawasiliano na klabu ya Teungueth ya Senegal yaliyopelekea kadhia hii, hata hivyo, Klabu ya Simba inapenda kujulisha umma kuwa iko mbioni kukamilisha malipo hayo hivi punde, klabu ya Simba itaendelea kuheshimu sheria, kanuni na kanuni na taratibu za mpira wa miguu kama ambavyo imekua ikifanya”

20231123_162417.jpg

Pia soma: Simba Sport Club yafungiwa kusajili kisa Pape Ousmane Sakho
 
Kwann baada ya kuumuza na kulipwa 50% na nyie msingelipa nusu ya hela ya watu? Na ndio kwanza mkakata mawasiliano

Janja janja nyingi shida yenu.
Masela walitaka waitafune hela halafu mzigo wamwachie kanji bhai...
 
Simba iko mbioni kulipa ili kujiepusha na kadhia ya kufungiwa.View attachment 2822539

Pia soma: Simba Sport Club yafungiwa kusajili kisa Pape Ousmane Sakho
Wakuu, kwa barua hiyo, linazuka swali lingine. Kwa hapa JF, sina shaka ni sehemu ambayo wapo watu wenye vichwa vyao, ambao hakipiti kitu rahisi hivi hivi bila kuumiza kichwa hata kidogo.

Ombi langu, kwa anaye fahamu, hivi kupeleka mashtaka huko , mpaka kuanza kuyasikiliza, kujitetea kwa aliyeshtakiwa, inaweza kuchukua muda gani?

Nimeuliza hivyo, kwa sababu, Simba wanatuambia walilipwa fedha nusu tarehe 2/10/2023. Hivyo, toka walipwe mpaka leo 23/11/2023, zimepita siku 52. Na tunaambiwa hukumu, walipewa siku 45 toka hukumu, wawe wamelipa.

Kimahesabu hapo, ukitoa hizo siku 45 kurudi nyuma toka leo, zinabaki siku 7. Kwa hiyo, inaonyesha hukumu ilitoka siku 7 tu toka wapewe hiyo 50%?
 
Wakuu, kwa barua hiyo, linazuka swali lingine. Kwa hapa JF, sina shaka ni sehemu ambayo wapo watu wenye vichwa vyao, ambao hakipiti kitu rahisi hivi hivi bila kuumiza kichwa hata kidogo.

Ombi langu, kwa anaye fahamu, hivi kupeleka mashtaka huko , mpaka kuanza kuyasikiliza, kujitetea kwa aliyeshtakiwa, inaweza kuchukua muda gani?

Nimeuliza hivyo, kwa sababu, Simba wanatuambia walilipwa fedha nusu tarehe 2/10/2023. Hivyo, toka walipwe mpaka leo 23/11/2023, zimepita siku 52. Na tunaambiwa hukumu, walipewa siku 45 toka hukumu, wawe wamelipa.

Kimahesabu hapo, ukitoa hizo siku 45 kurudi nyuma toka leo, zinabaki siku 7. Kwa hiyo, inaonyesha hukumu ilitoka siku 7 tu toka wapewe hiyo 50%?
Janja janja ni kawaida yao, mwaka 2021 walipigwa ban pia na FIFA


Mwamedi ni msanii sana
 
Wakuu, kwa barua hiyo, linazuka swali lingine. Kwa hapa JF, sina shaka ni sehemu ambayo wapo watu wenye vichwa vyao, ambao hakipiti kitu rahisi hivi hivi bila kuumiza kichwa hata kidogo.

Ombi langu, kwa anaye fahamu, hivi kupeleka mashtaka huko , mpaka kuanza kuyasikiliza, kujitetea kwa aliyeshtakiwa, inaweza kuchukua muda gani?

Nimeuliza hivyo, kwa sababu, Simba wanatuambia walilipwa fedha nusu tarehe 2/10/2023. Hivyo, toka walipwe mpaka leo 23/11/2023, zimepita siku 52. Na tunaambiwa hukumu, walipewa siku 45 toka hukumu, wawe wamelipa.

Kimahesabu hapo, ukitoa hizo siku 45 kurudi nyuma toka leo, zinabaki siku 7. Kwa hiyo, inaonyesha hukumu ilitoka siku 7 tu toka wapewe hiyo 50%?
Kwahiyo unataka kusemaje?
 
"Kukopa harusi kulipa matanga".

Watanzania mpaka wameminywa p ndiyo wanajuwa kulipa. Shenzi taipu.
 
Ukisikia uswahili ndio huu. Wameshapoke 50% walitakiwa wailipe hiyo club papo hapo hata 7.5% wakipolea installment ya pili wamalizie, ndio namna biashara inafanyila siyo utapeli utapeli
 
Kwahiyo unataka kusemaje?
Nataka kusema kuwa,je hiyo kesi ilianza kabla ya kutolewa hiyo fedha nusu? Na kama ilikuwa walipe hiyo fedha watakayo lipwa wao, kwa nini washindwe hili shauri? Kwa mujibu wa barua yao, sikuona kama walistahili kushindwa na kupewa adhabu. Wasiwasi wangu, hatujaambiwa ukweli .

Haiwezekani, hukumu itoke siku saba toka walipwe. Utajiuliza, walishtakiwa lini? Inawezekana walilipwa siku nyingi sio hiyo 2/10/2023
 
Timu yangu watu wanagawana fito hadi wanakaushia madeni, Simba hamna uongozi pale
 
Back
Top Bottom