SAKATA la Bombadier: Tundu Lissu ni mmoja wa samaki wadogo. Atutajie zile kubwa

Wabongo bwana, eti MTU akihoji utendaji wa serikali na maamuzi yake ya kukurupuka, na kujaribu kuonyesha hasara nchi hii imeipata, zaidi akiwatanabahisha wanasheria watende kwa weledi katika uingiaji wa mikataba na kuishauri serikali ipasavyo inapotaka kuvunja mkataba, badala ya kuhanikizwa na wanasiasa.


Leo MTU huyo anaitwa si mzalendo. Je uzalendo ni kupiga vigelegele kwa kila serikali inachokifanya, pasi na kuishauri, kukosoa au kuonya? Wengi tunakumbuka mikataba ya madini inayopigiwa kelele kwa sasa huko nyuma ulipokuwa ukihoji majibu yake yalikuwa kama haya. Ooh! Wavivu wa kufikiri, ooh wawekezaji wanatumia mitaji mikubwa tuwalinde.

Ooh tunajenga mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji na tusipofanya hivyo wataenda nchi zingine, hivyo Rais wetu ( BWM) anahitaji kuungwa mkono na mguu sasa yako wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
wabongo ni maiti tu ndio maana watu wanavumyiwa nyumba zao na hawaseme kitu
 
Hakuna hasiyejua kuwa tulinunua Bombadiee Q400 Dash 8, ofcoz suala lilikuwa wazi na kila mtu alikuwa anajua ndege imeshalipiwa tunasubiria zije tu. Hivyo ata hao wadeni wetu walikuwa na information zote ndio maana wakaikamata kirahisi, usimsingizie mtu yeyote yule
Haya. Asiyejua maana HAAMBIWI maana.
 
Labda ni baada ya tambo za mkulu kuwa cash ipo tele mpaka ndege analipa bila kuhitaji.
Nao wakaona ni wakati muhafaka kudai kilichochao.
Si hivyo mkuu. Ni ngoma inayochezwa ili Maono ya Magufuli yasitimilike.Na inachezwa chini chini. WHY NOW after miaka17. Hebu jiulize.
 
Uhuru sio kuwaondoa wazungu tu!

Bado taifa hili halina uhuru wa kuihoji serikali, kuikosoa, na hata kuishauri.

Nchi yenye uhuru Raisi hawezi kuingilia maamuzi ya bunge, kutojali maumivu ya watu wake kwa mfano serikali iko kimya kupotea kwa ben saanane, kutekwa kwa roma, na hata kutishiwa basola kwa nape.

Lakini pia watu wenye kinga ya mahakama serikali inabomoa nyumba zao, so sijui ni uhuru gani watakaojiringia wananchi hao.

Nahisi utakuwa umepata logic.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa. Ila katika kukosoa serikali kosoa kwa heshima na toa suluhisho au maoni mbadala.
Tuone NANI ATAKUSHITAKI.Kuingilia Bunge sijasikia bali kumwomba Spika tu hilo nimesikia. Na Bunge LINAJITEGEMEA.
Na Haliwezi kuingiliwa na rais. Unless kama WAKATI ALIPOLIOMBA BUNGE LICHUNGUZE na LIREKEBISHE SHERIA za MADINI.

Maana Rais HAWEZI Kuzibadilisha yeye binafsi kiholela. Basi hazitakuwa na MASHIKO na NGUVU KISHERIA. Kumbuka Bunge hutunga sheria Serikali Hutumia sheria hizo na kuzi enforce.

MAHAKAMA nayo haingiliwi ISIPOKUWA inapotaka KU SLOW down MAENDELEO ya nchi kwa Manufaa ya wachache.
Kama RELI ya KISASA inataka kujengwa je IPITIE CHUMBANI mwa mtu aliye ndani ya MITA husika asizoruhusiwa mtu kujenga nyumba?
 
Tumeshikiliwa mali zetu na Uganda??? Au nimeona vibaya, tunadaiwa nini na Uganda. Hii nchi ina madeni kila kona
 
Nafikir ipo haja ya kujua nn maana ya SHEREHE/KUSHEREKEA, tuwekee kapicha tuone TL alivosherekea
Wakati Lugha ya mtu inapomsaliti. Na si TL pekee ila ni pamoja na hao Watanzania wachache wasioitakia mema nchi hii.
 
Bora ubaki huko huko manake wameshakuharibu,anaetangaza watu wafe kwa njaa ni Magu. Lisu ni mwanasiasa lazima apinge sera za CCM mawazo tofauti si dhambi. Acheni wengine wafikiri tofauti na mabwana zenu.

Watanzania wengi wamefurahi sababu sizonje mbaguzi na ana roho mbaya, polisi n nyie vibaraka wake hamtaweza kumsafisha wanaomwambia abadilike ndio watamsafisha.

Ni vile hauko bongo kitambo kama kweli ila huyu jamaa tunamuombea mabaya sababu anatutesa kw ushamba wake na hashauriki. Yeye mwenyewe sio mfia nchi zaidi ya kwao na jamaa zake.


Uzalendo ni kufia nchi yako. Huwezi ukafurahia nchi yako inyimwe misaada watu wafe kwa kukosa chakula na madawa kisa unampinga mpinzani wako wa kisiasa. Huo ni ushenzi namba wani.

Na kwenye hili la ndege kukamatwa, Lissu amefurahia sana hasa kwenye ile hotuba yake. Na kwa kuangalia timing, motive, circumstances ni wazi Lissu na wenziwe wana mkono katika hili.

Heri lawama kuliko fedheha. It is about time serikali iwaangushie rungu la dola. Hivi vya kuogopa kuonekana serikali inafunga wapinzani at this point viwekwe pembeni. Kuna baadhi ya wapinzani hawana adabu na wana take advantage serikali kuogopa lawama.

Wanamuita Magufuli dikteta. Dikteta hakamati mtu mara saba kwa kosa hilo hilo. Anakamata mara moja tu anaekamatwa hatoki tena. Na akitoka hata siasa yenyewe hataki tena.

Hapo kusiwe na dhamana wala bail na atakayejipendekeza awekwe ndani vile vile.

Wengine hata uraia tulishapoteza lakini bado tuna uchungu na homeland. Magufuli anakusanya kodi, anapinga rushwa, ana vision ya maendeleo. Hawa wapinzani wangekuwa positive wakashirikiana nae bado wangepata umaarufu kisiasa, wangependeza kwa wananchi na nchi ingesonga mbali.

Niko Marekani zaidi ya miaka ishirini. Kungekuwa na upinzani wa kipumbavu kama huu wa Tanzania Marekani ingeshaparaganyika siku nyingi.

Upinzani mahali pake ni bungeni. Serikali inapingwa bungeni. Tena uchaguzi wa wabunge kuna mid term election. Huu hausubiri uchaguzi mkuu wa rais.

Wabunge, magavana na maraisi wa upinzani wanashindana kwa kuwafanyia mema wananchi na nchi yao. Sio kwa kuifanyia ushenzi nchi.
 
Usiangalie tulipoangukia, angalia tulipojikwaa.
Umghadhibikie aliyesababisha deni maana ndipo "mimba" ilipotungia..

Huyo si mwingine bali ni Joni pombe
AWAMU ZILIZOPITA ndo ZIMETULETEA haya. Hela ngapi ilitumika MASAFARI ya nje ya nchi bila TIJA kwa taifa?
Mzee ameingia
AMEBANA mianya.
RELI za kisasa zinataka kujengwa,
NDEGE nazo AMENUNUA nk.
Kwani hawa walikuwaga wanatumiaje hela?
Ndo walotuingiza katika TAABU hii ya KUDAIWA.
Wakatuachia madeni.
 
Mimi ninasimama pekee yangu kwa msaada wa Mungu pekee. Sina egemeo lingine mkubwa !!

Unless hii "nimejua umeegemea wapi ", uwe na maana kuwa namtetea Tundu Lissu...

If that what you mean..... then you are absolutely right !

Hii ni kwa sbb, mimi nawapenda sana mwanasiasa wa sampuli ya Tundu Lissu....

Specific kwa TL, ni kuwa thé guy ni jasiri na mwerevu, msomi anayeutumia usomi wake kwa usahihi kabisa sana na kwa hakika (hata km utabisha), jamaa ni mzelendo haswaa wa taifa lake....

Ni kwa sbb, mzalendo wa kweli, si mnafiki, mu wazi na msema kweli kwa maana ya ukweli wenyewe. Akikosea hukiri makosa yake, hana majivuno (arrogance), hajikwezi kama alivyo Magufuli Rais wako na vivyo hivyo haoni haya kuwakosoa wengine na vivyo hivyo kuwapongeza/kuwatambua....

Mimi naegemea kwa mtu wa namna hii, mwenye sifa hizi, baaaasi.....
Ni siku gani TL alikosea AKAKIRI?
Na ni WAPI Magufuli AMEJIKWEZA?
Naomba jibu la hayo mawili
 
Wewe ni mpuuzi mkubwa badala ya kuongelea hasara tuliyopata unaongelea upumbavu mtupu tena wa mgonjwa wa akili! Lissu ndie alivunja mkataba? ndie aliyedai? eti mzalendo una uzalendo gani wewe hata chembe ya uzalendo hujui na definition ya uzalendo kwako ni msamiati!
Ahsante mwalimu. Probably definition ya UZALENDO nitaifahamu. Akili yangu iko timamu
Ndo maana siadiki na JAZBA kama ulivyoandika wewe. EXAMINE yourself na uji evaluate kuhusu MATAMSHI yako.
Hapo utajua mimi na wewe tuko tofauti sana.
 
Back
Top Bottom