Education Mentor
JF-Expert Member
- Oct 26, 2016
- 396
- 687
SAIKOLOJIA: KUPAMBANA KUSHINDANA CHUKI
Katika somo la leo najaribu kuangazia Saikolojia ya kuhusu chuki ambao katika Ulimwengu wa leo uliotaharuki kwa visasi na ukatili kutokana na tatizo hilo.
Lakini kuhusu chuki si kwamba tu imekuwepo katika ulimwengu huu tu ni jambo ambalo limekuwepo kwa karne na karne nyingi, lakini shida inakuja sababu hatujui namna ya kupambana na chuki au kuelewa kwanini chuki zinakuwepo au unajikuta unaingia katika mazingira ya kuchukia au kuchukiwa.
Chuki mara nyingi anazaliwa na Hasira inayochochewa na fitina au taarifa zinazochochewa vibaya. Na Chuki ndio baba wa vita na machafuko Ulimwenguni kote kuanzia katika familia, koo, jamii, kabila, taifa na hadi mataifa.
Sababu chuki anabebwa kirahisi na kutumika kama propaganda ili kuunganisha jamii kuwa na adui mmoja katika dhana ya Utaifa (Nationalism), mifumo ya kimaisha mfano ubepari na ujamaa na hata katika dini pia.
BASI TUANZE NA TAFSIRI MUHIMU KWANZA JE, CHUKI NI KITU GANI?
Tafsiri
Chuki ni hali ya kutokuwepo upendo hali ya kuwa na roho mbaya hali ya kuwa na kinyongo.
Tunaona misamiati mitatu muhimu inatokea katika tafsiri ambayo ni kukosekana upendo, roho mbaya na kinyongo.
Kisaikolojia
Chuki ni hisia za ndani za kutokutaka, kuvutiwa au kupenda
Jambo au kitu chuki kinaweza tofautiana kwa kiwango tofautitofauti na muelekeo wa tabia za uadui ambapo upelekea uharifu, mauaji au hata vita.
Kwanini basi kuna Chuki? sababu kuna wakati unaweza jiuliza kwanini nachukiwa na pengine ukatafuta suluhu pasipo kupata majibu ya kuridhisha.
Aina za chuki
Chuki katika dunia ya leo zinagawanywa katika makundi kama yafuatayo chuki za kisiasa, Kidini, kijinsia na zile za rangi (Racism)
Chuki hubeba sifa nyingi lakini baadhi ni hizi
Mfano kama mbeba chuki ana matatizo kama vile Schizophrenia au Bipolar disorder na mengine mengi yanaweza kumpelekea kuwa na chuki pasipo mantiki.
Lakini katika suala la fikra inaweza kuwa shida ya kimazingira tu labda kiburi mfano labda ndugu mmoja anaona jamii flani au jinsia flani ni duni au washamba basi hawapaswi kuwa na fursa au nafasi katika jamii.
Hata kama masirahi hayo ni halali au batili kwahiyo wakati wote unaweza kujikuta unatumbikua katika chuki bila kufahamu labda pengine umekuwa sehemu ya kupambana na rushwa au uharifu Fulani.
Husuda mara nyingi sana ndizo zina zaa Majungu na fitina hasa kama kuna ushindani wowote makazini na kwenye jamii.
Kutokana husuda huanza na wivu unaoegemea upande hasi. Hivyo ni muhimu sana kujifunza kufurahia mafanikio ya wengine na pia yakikupa motisha.
UFANYE NINI UNAPOKUMBANA NA TATIZO LA CHUKI KATIKA JAMII AU MAKAZINI
Katika somo la leo najaribu kuangazia Saikolojia ya kuhusu chuki ambao katika Ulimwengu wa leo uliotaharuki kwa visasi na ukatili kutokana na tatizo hilo.
Lakini kuhusu chuki si kwamba tu imekuwepo katika ulimwengu huu tu ni jambo ambalo limekuwepo kwa karne na karne nyingi, lakini shida inakuja sababu hatujui namna ya kupambana na chuki au kuelewa kwanini chuki zinakuwepo au unajikuta unaingia katika mazingira ya kuchukia au kuchukiwa.
Chuki mara nyingi anazaliwa na Hasira inayochochewa na fitina au taarifa zinazochochewa vibaya. Na Chuki ndio baba wa vita na machafuko Ulimwenguni kote kuanzia katika familia, koo, jamii, kabila, taifa na hadi mataifa.
Sababu chuki anabebwa kirahisi na kutumika kama propaganda ili kuunganisha jamii kuwa na adui mmoja katika dhana ya Utaifa (Nationalism), mifumo ya kimaisha mfano ubepari na ujamaa na hata katika dini pia.
BASI TUANZE NA TAFSIRI MUHIMU KWANZA JE, CHUKI NI KITU GANI?
Tafsiri
Chuki ni hali ya kutokuwepo upendo hali ya kuwa na roho mbaya hali ya kuwa na kinyongo.
Tunaona misamiati mitatu muhimu inatokea katika tafsiri ambayo ni kukosekana upendo, roho mbaya na kinyongo.
Kisaikolojia
Chuki ni hisia za ndani za kutokutaka, kuvutiwa au kupenda
Jambo au kitu chuki kinaweza tofautiana kwa kiwango tofautitofauti na muelekeo wa tabia za uadui ambapo upelekea uharifu, mauaji au hata vita.
Kwanini basi kuna Chuki? sababu kuna wakati unaweza jiuliza kwanini nachukiwa na pengine ukatafuta suluhu pasipo kupata majibu ya kuridhisha.
Aina za chuki
Chuki katika dunia ya leo zinagawanywa katika makundi kama yafuatayo chuki za kisiasa, Kidini, kijinsia na zile za rangi (Racism)
Chuki hubeba sifa nyingi lakini baadhi ni hizi
- Chuki husambaa haraka sana kuliko hasira
- Chuki ni chombo kinachotumika kutengeneza na kusambaza propaganda
- Chuki huwa inatoa ujasiri wa kitambo tu
- Chuki ni hasira iliyojengwa muda mrefu hata kukomaa kutokana na taarifa za aina ya fitina
BASI FAHAMU MAZINGIRA YANAYOWEZA SABABISHA CHUKI? - Fikira potofu
Mfano kama mbeba chuki ana matatizo kama vile Schizophrenia au Bipolar disorder na mengine mengi yanaweza kumpelekea kuwa na chuki pasipo mantiki.
Lakini katika suala la fikra inaweza kuwa shida ya kimazingira tu labda kiburi mfano labda ndugu mmoja anaona jamii flani au jinsia flani ni duni au washamba basi hawapaswi kuwa na fursa au nafasi katika jamii.
- Kujifunza
- Sumbua Tendea Vibaya au Tesa jamii au kundi flani
- Misiguano ya kimasilahi
Hata kama masirahi hayo ni halali au batili kwahiyo wakati wote unaweza kujikuta unatumbikua katika chuki bila kufahamu labda pengine umekuwa sehemu ya kupambana na rushwa au uharifu Fulani.
- Husuda
Husuda mara nyingi sana ndizo zina zaa Majungu na fitina hasa kama kuna ushindani wowote makazini na kwenye jamii.
Kutokana husuda huanza na wivu unaoegemea upande hasi. Hivyo ni muhimu sana kujifunza kufurahia mafanikio ya wengine na pia yakikupa motisha.
UFANYE NINI UNAPOKUMBANA NA TATIZO LA CHUKI KATIKA JAMII AU MAKAZINI
- Muhimu fahamu kwamba sio wakati wote unaweza fahamu kwa nini unachukiwa?. Hivyo muhimu kuchukua hatua za kiusalama hasa pale vitisho vinapokuwa vinachukua hatua.
- Pata washauri wazuri sababu wakati mwingine kuna vitu tunafanya tunakosea hivyo kwa hali ya kibinadamu inakuwa sio rahisi kufahamu. Hivyo ni muhimu kuondoa kiburi na kukubali kuweza shauriwa au shaurika.
- Wakati mwingine hii utokea kazini hasa pale unapokuwa labda pengine una juhudi katika kujituma kwa kazi sana (do gooders) hii pia zipo tafiti zinazodhibitisha huwa ni vichochezi vya chuki makazini au mashuleni.
- Wakati mwingine katika ushindani wa namna yoyote kati ya mtu na mtu au watu na vikundi hasa unapojitokeza kutoa msaada upande mmoja kwa kufahamu au kutofahamu.
- Wakati mwingine ni muhimu sana kujifunza kukaa kimya sababu kuongea ongea napo pia huchochea kujenga chuki.