Ndanda to Lomwe
Member
- Aug 7, 2008
- 31
- 1
Spika wa bunge amewasili mjini Urambo majira ya alasiri akitokea Tabora ambako alitua na ngege ya pricision iliyotokea Dar.Mjini Tabora alipokelewa na wanafamilia.
Baada ya mapumziko ya muda alianza safari ya kuelekea Urambo,kama kilomita 20 kutoka Urambo ndipo yalipoanza maandamano ya kumpokea ambayo yalikuwa yakisimamishwa na wananchi wakitaka hata wasikie sauti yake,naye hakutaka kuwakatisha tamaa,alilazimika kuhutubia mikutano 3 leo akiwa katika vijiji vilivyopo njiani kuelekea Urambo,amewaambia wanachi wasiwe na wasiwasi kwa yaliyotokea DODOMA,yeye hatabadilika hata kidogo na ataendelea na mapambano juu ya ufisadi na hakuna wa kumtisha.
Baada ya hapo akaendelea na hutuba kwa kuzungumzia juu ya maendeleo na mafanikio katika kipindi chake cha Ubunge na kuwajulisha wananchi kuwa sasa barabara ya Urambo - Tabora iaanza kuwekwa lami.
Baada ya mapumziko ya muda alianza safari ya kuelekea Urambo,kama kilomita 20 kutoka Urambo ndipo yalipoanza maandamano ya kumpokea ambayo yalikuwa yakisimamishwa na wananchi wakitaka hata wasikie sauti yake,naye hakutaka kuwakatisha tamaa,alilazimika kuhutubia mikutano 3 leo akiwa katika vijiji vilivyopo njiani kuelekea Urambo,amewaambia wanachi wasiwe na wasiwasi kwa yaliyotokea DODOMA,yeye hatabadilika hata kidogo na ataendelea na mapambano juu ya ufisadi na hakuna wa kumtisha.
Baada ya hapo akaendelea na hutuba kwa kuzungumzia juu ya maendeleo na mafanikio katika kipindi chake cha Ubunge na kuwajulisha wananchi kuwa sasa barabara ya Urambo - Tabora iaanza kuwekwa lami.
Last edited: