Bujibuji Simba Nyamaume
Platinum Member
- Feb 4, 2009
- 78,169
- 166,130
MTU mmoja anayedaiwa kuwa ni mchawi alidondoka kwenye nyumba moja eneo la Mbezi Luis jijini Dar es Salaam akiwa safarini kwa njia ya ungo akielekea Shelisheli kwenye mkutano wa wachawi.
Taarifa za awali zilieleza kwamba mtu huyo alijieleza kwamba alitokea mkoani Mwanza akiwa na wenzake sita wakielekea kwenye mkutano nje ya nchi , lakini bahati mbaya yeye alidondoka katika jiji la Dar es Salaam.
Pmaoja na bahati mbaya yake ya kudondoka, lakini pia alikubwa na kipigo kikali kutoka kwa wakazi wa eneo la Mbezi asubuhi ya jana na kusababisha kifo chake.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, marehemu ambaye jina lake halikujulikana alidai alidondoka na ungo wake katika eneo hilo alipokuwa safarini.
Huyu mtu ana umri wa kati ya miaka 28 na 35, alikuwa hana nguo, bali alijifunga kipande kidogo cha nguo kukinga sehemu za siri na alikuwa amejipaka masizi usoni na sehemu zingine za mwili, alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Naye mwenye nyumba alipodondoka marehemu , Mwajabu Shabani alisema aliamka jana saa 12 asubuhi na kwamba alipofungua mlango wa kutoka nje, ghafla alimuona mtu huyu akiwa amekalia ungo na kujiinamia.
Nilishtuka kuona mtu wa namna hiyo, katika hali ya kiwewe na kutaka msaada kwa watu, wakaja na kuanza kumhoji huku vurugu mshangao vikizidi kuongezeka na kusababisha mlango wa nyumba yangu kuvunjwa, alisema mama huyo.
Alisema katika mahojiano hayo mtu huyo alidai kuwa alitoka Mwanza akiwa na wenzake sita wakiwa safari kuelekea Shelisheli kwenye mkutano ambapo wenzake wamemwacha.
Mwandishi alishuhudia ungo aliokuwa akitumia mtu huyo kusafiria ambao ulikuwa ukichomwa na baadhi ya watu waliokuwa katika eneo hilo , lakini haukuungua .
Ungo huo ukawa kivutio kwani hata baada ya kuweka mfuta ya taa moto haukuwaka.
Pamoja na ungo huo kulikuwa na vitu vingine kama, pembe ya ngombe iliyokuwa imefungwa na matambara.
Jitihada ya kumpata mwenyekiti wa mtaa aliyejulikana kwa jina moja la Kayanda hazikufanikiwa na ilisemekana alikuwepo kwenye eneo la tukio ila aliondoka baada ya kupingwa na kukimbia kutokana juhudi zake za kuwazuia watu wasimpige mtu huyo.
Mwandishi aliona vurugu zilivyozidi na aliamua kwenda kituo cha polisi Mbezi kwa Yusuf, lakini alipishana na polisi waliokuwa wakielekea kwenye tukio ingawa walikuta tayari mtu huyo alishauawa.
Polisi waliuchukua mwili wa mtu huyo ingawa waliauacha ungo wake na vitu vingine huku watu wakiendelea kuushangaa ungo huo uliokuwa hauungui moto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga alipoulizwa juu ya tukio hilo, alisema bado hajapata habari hizo.
Ndiyo kwanza nazisikia habari hizi kwako, hata asubuhi nilipoambiwa matukio yaliyotokea katika mkoa wangu, hilo sikuambiwa, lakini nitafuatilia tukio hilo, alisema Kamanda Kalinga
Taarifa za awali zilieleza kwamba mtu huyo alijieleza kwamba alitokea mkoani Mwanza akiwa na wenzake sita wakielekea kwenye mkutano nje ya nchi , lakini bahati mbaya yeye alidondoka katika jiji la Dar es Salaam.
Pmaoja na bahati mbaya yake ya kudondoka, lakini pia alikubwa na kipigo kikali kutoka kwa wakazi wa eneo la Mbezi asubuhi ya jana na kusababisha kifo chake.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, marehemu ambaye jina lake halikujulikana alidai alidondoka na ungo wake katika eneo hilo alipokuwa safarini.
Huyu mtu ana umri wa kati ya miaka 28 na 35, alikuwa hana nguo, bali alijifunga kipande kidogo cha nguo kukinga sehemu za siri na alikuwa amejipaka masizi usoni na sehemu zingine za mwili, alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Naye mwenye nyumba alipodondoka marehemu , Mwajabu Shabani alisema aliamka jana saa 12 asubuhi na kwamba alipofungua mlango wa kutoka nje, ghafla alimuona mtu huyu akiwa amekalia ungo na kujiinamia.
Nilishtuka kuona mtu wa namna hiyo, katika hali ya kiwewe na kutaka msaada kwa watu, wakaja na kuanza kumhoji huku vurugu mshangao vikizidi kuongezeka na kusababisha mlango wa nyumba yangu kuvunjwa, alisema mama huyo.
Alisema katika mahojiano hayo mtu huyo alidai kuwa alitoka Mwanza akiwa na wenzake sita wakiwa safari kuelekea Shelisheli kwenye mkutano ambapo wenzake wamemwacha.
Mwandishi alishuhudia ungo aliokuwa akitumia mtu huyo kusafiria ambao ulikuwa ukichomwa na baadhi ya watu waliokuwa katika eneo hilo , lakini haukuungua .
Ungo huo ukawa kivutio kwani hata baada ya kuweka mfuta ya taa moto haukuwaka.
Pamoja na ungo huo kulikuwa na vitu vingine kama, pembe ya ngombe iliyokuwa imefungwa na matambara.
Jitihada ya kumpata mwenyekiti wa mtaa aliyejulikana kwa jina moja la Kayanda hazikufanikiwa na ilisemekana alikuwepo kwenye eneo la tukio ila aliondoka baada ya kupingwa na kukimbia kutokana juhudi zake za kuwazuia watu wasimpige mtu huyo.
Mwandishi aliona vurugu zilivyozidi na aliamua kwenda kituo cha polisi Mbezi kwa Yusuf, lakini alipishana na polisi waliokuwa wakielekea kwenye tukio ingawa walikuta tayari mtu huyo alishauawa.
Polisi waliuchukua mwili wa mtu huyo ingawa waliauacha ungo wake na vitu vingine huku watu wakiendelea kuushangaa ungo huo uliokuwa hauungui moto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga alipoulizwa juu ya tukio hilo, alisema bado hajapata habari hizo.
Ndiyo kwanza nazisikia habari hizi kwako, hata asubuhi nilipoambiwa matukio yaliyotokea katika mkoa wangu, hilo sikuambiwa, lakini nitafuatilia tukio hilo, alisema Kamanda Kalinga