Safari ya Lissu kuelekea Nairobi ilikuwa ni mateso na vilio, Spika Ndugai usitoneshe vidonda

Nimesikitika sana,sikutegemea mjomba wangu Ndugai aongee vile leo alivyoongea!!

Pia hakuna kitu kimeniuma sana kama nilivyosikia Ndugai alikuwa kwenye ile kamati ya bunge iliyokwenda nyamongo kisha kupindisha ukweli eti maji ya mto hayakuwa na sumu lakini wananchi walipowataka wabunge wa kamati ile waguse maji wabunge wote waligoma. Halafu leo hii Ndugai anasimama na kujifanya mzalendo eti anapigania raslimali za taifa huku akisahau Lissu ndio aliyekuwa akiwatetea wananchi wa nyamongo dhidi ya sumu ile kwenye mto. Halafu ukimsikia anavyozunguza kwa kejeli na ulevi wa madaraka huku akiwananga wapinzani kwamba ndio kipimo cha kutokuwa dhaifu. Yaani hajui hata udhaifu uko kwenye nini.
 
Kuna watu humu nimeona nao wanachangia kwa upotoshaji,akiwemo mtu anaitwa Tume ya Katiba juu ya namna Lissu alivyotoka Tanzania kwenda Nairobi.

Kwanza naomba ku-declare kuwa nilishiriki "indirectly" kuona namna gani usafiri wa kwenda Nairobi unapatikana,japo nilikuwa mbali na nyumbani,lakini niliwasiliana na wadau ili kuona huyu mtu anapata usafiri kufika eneo la matibabu baada ya kusikia uhitaji mkubwa ni kufika Nairobi usiku uleule.

Suala la kwanza lilioafikiwa na Bunge ilikuwa ni kumleta Dsm-Muhimbili,ndege iliyokodiwa ilikuwa ni ya kampuni ya Safari Air Link na si ya NHIF kama anavyosema huyo Ndugai,ambayo ni MEDEVAC,ilikuwa ni Caravan usajili wa 5H-EWA,mali ya Peter Fox(mmiliki wa kampuni ya Safari Air Link),bahati mbaya ikatokea mabadiliko ya kwenda Nairobi,na ile ndege ikawa na rubani mmoja na haiwezi kwenda Nairobi usiku ikiwa na rubani mmoja ambaye hakuwa na masaa ya kuruka usiku.TCAA walikuwa tayari kutoa kibali cha ndege kuruka usiku hata kama ina injini moja kwa sharti la kuwa na marubani wawili,Ukawa ni mtihani mwingine wa kuanza kutafuta ndege nyingine usiku uleule.

Ndege nyingine ya Safari Air Link aina ya Citation(Jet Engines) siku hiyo ilikuwa imeenda Pemba ya Mozambique kama si Zambia,Fox akawa hana option,sbb pia hiyo ndege isingeweza kubeba abiria wengi ambao CHADEMA walikusudia wasafiri na Lissu.

Ndege kubwa ya kuwatosha mgojwa,daktari pamoja na wasindikizaji akiwemo mkewe, ikawa ni hiyo Citation ya Flight Link,5H-ETG.Ambayo ilipaswa kutoka Dsm kuja Dodoma usiku uleule,ili inyanyuke kwenda Nairobi.

Jambo hili likawezekana,lakini ilipaswa pesa iwe juu ya meza kwa mlipo ya dola,Dodoma hakukuwa na Mbunge wala waziri mwenye dhamana ya dola,Turky wa Mpendae akachukua dhamana hiyo ya mali kauli,sababu mmiliki wa kampuni ya Flight-Link(Mhindi) wana ushirika naye.Ndege ilinyanyuka Dsm-Dodoma na baadae Nairobi

Siri ya safari ile wakiwa angani,naamini ipo siku Mbowe na Msigwa wataiandikia kitabu(A Day to Remember in a Dark Political Arena),Ilikuwa ni safari ngumu iliyojaa machozi na uchungu mkubwa,walisafiri kwa shida sana,kitanda kilikuwa kinacheza na pia dripu ilibidi Dokta asafiri akiwa ameishika mkononi kaining'iniza juu sababu ya "height" ya ndege,ilikuwa ni safari ya mateso na experience mbaya sana kwa kina Msigwa na Mbowe pamoja na mke wa Lissu.Mungu aliyemponya Danieli katikati ya Simba wenye njaa,alitenda miujiza.

Sijaelewa huu upotoshaji wa huyu Ndugai ameutoa wapi,kwamba kuna ndege ilikodiwa toka Nairobi?Hiyo ndege ni ipi?kwamba aliomba itumie "airspace" ya Tanzania kinyume na sheria za nchi?Kwani sheria za nchi zinavunjwaje kwa ndege iliyoomba kibali kutua Tanzania na ikaruhusiwa?

Huu uwongo ni wa nini?hiyo ndege mliyokodi toka Kenya ni ipi?Maana kila mtu hata siyekuwa Dodoma aliona ndege iliyoondoka na Lissu ni 5H-ETG mali ya kampuni ya FlightLink.

Hii ni kampuni ya Tanzania,ndio maana usajili wa ndege umeanza na "5H",ndege zote zilizosajiliwa Tanzania huanza na "5H",zile za Kenya huanza na "5Y" na majirani Uganda ni "5X"...Wewe Ndugai hiyo ndege ya Kenya mliyoiombea kibali cha kutumia "airspace" yetu tena kinyume cha sheria ni ipi?Na sheria zipi mlizovunja?

Sasa unaona mtu anakuja humu anasema eti Lissu alitoka na ndege Dodoma hadi Dsm then ndio akaenda Nairobi.Huu uwongo mnauzalisha toka wapi??Wacheni upumbavu katika uhai na maisha ya watu sbb ya siasa!!Eboooo!!!!

Nimemsikiliza Ndugai hapa Jf kwenye video,ameongea kwa uchungu na huzuni,sababu maneno ya Lema yamemuingia sana,amefikia hatua ya kusema kama CHADEMA wanataka kumpeleka Lissu India,bunge lipo tayari endapo Waziri atakubali.Maneno ya Lema yamegusa mfupa,Job anajua aliondoka na hali gani hapa nyumbani kwenda India,amekaa miezi kibao akiugua.

Kila aliyekuwa anasimama bungeni,kabla ya kuchangia,alimuombea Spika afya njema na arudi mzima nyumbani.Watu walisali...Kuna siku Bulaya aliongoza sala ya kuomba afya ya spika katika Canteen ya Bunge.

Malumbano yanayoanzishwa na Spika ndani ya bunge juu ya afya ya Lissu ni afya kwa ubinadamu na utu.Kuanzia lile la kutofautiana idadi ya risasi na Kubenea mpaka kamati ya maadili,na lile kusema Turky ndio kachangia.Turky ni muislam safi,sadaka isiyo na mawaa na yenye dhawabu haitangazwi.

Palipo na tendo jema,Mungu hufungua riziki...Kuitangaza sadaka ya Turky bungeni na kumuondolea neema kubwa na ndogondogo mja wake.Mh.Spika,tumia busara kufunga malumbano ya afya ya Lissu Bungeni,wakati upo India,watu walijibiidisha kukuombea na si kujadili na kulumbana juu ya afya yako na matibabu yako.FUNGA MJADALA WA KUSIMANGANA BUNGENI KUHUSU AFYA NA HALI YA TUNDU LISSU...HUU SI UBINADAMU.

Kuna kijana sijui ni msemaji wa chama naye katoka kabisa na "Press Release" kupongeza hali ya Mbunge Turky,kutoa "mali kauli" ya safari ya ndege.Jamani mnaharibu sadaka za wenzenu.Turky mwenyewe amenukuliwa akisema;
" Mbowe akaniomba kwa kuwa nafahamiana nao (wenye ndege) niwadhamini wamuwahishe Lissu halafu wao watalipa. Na ndicho nilichofanya (kuwadhamini kwa mali kauli) na pesa hiyo imelipwa jana. Tunamshukuru Mungu nia njema hufungua milango yake” .Watu mnaharibu sadaka za watu bila kujua,nia njema ya Turky ipo katika hayo maneno yake ya mwisho yenye "bold".

Msaidieni Lissu kama nyie mlivyosaidiwa kwa kofia za ubunge na uspika wenu,wacheni masimango,tendeni kama vile mlivyotendewa,wengine mlikwenda India miguu haingii hata katika viatu,mlivaa suti na sandozi.Mungu amewaponya...Lipeni wema juu ya wema!!Mnaleta "urasimu" wa taratibu za matibabu nje ya nchi kwa mwili wa binadamu ulipigwa na kulowa rasasi zaidi ya 10?Ebooo!!HIZO PESA ZA MAMA ZENU?

We Live Once,but Legacy Lives forever!!
View attachment 588456
Juu ni ndege ya kampuni ya FlightLink(Tanzania) iliyompeleka Lissu Nairobi

View attachment 588458
Hii ni ndege ya Safari Air Link iliyokusudiwa kumleta Dsm ikashindikana
Safi sana Mkuu Barafu! Heshima mbele, endelea kunyoosha mambo. chukua KUMI zangu!!
 
Barafu, Mungu awabariki nyote ambao mlitoa michango ya namna mbalimbali kumfanya mpendwa wetu Lisu aweze kupata matibabu. Hatuna maneno mazuri ya kusema. Hamkutenda kwaajili ya Lisu bali kwaajili yetu sote tuliopatwa na simanzi kubwa katika tukio hili.

Mungu wetu tunaomba usikie maombi yetu, ni maombi yetu sisi wenye huzuni, siyo maombi ya Tundu Lisu. Kama ulimfufua Lazaro, kama uliwaponya viwete, vipofu na wengine wengi, kwa nini isiwezekane kwa Lisu? Tunajua katika wewe Mungu wetu hakuna usiloliweza, ukitaka, mpendwa wetu anaweza kusimama wakati wowote.

Wewe ulisema, 'Ombeni mtapewa', tunajua wewe ni mwaminifu katika ahadi zako. Tunaomba kwaajili ya uhai na afya ya Mpendwa wetu Tundu Lisu.

Tena ulisema, 'Tafuteni mtapata', tunakutafuta wewe uliye asili ya yote, umjalie uzima na afya ndugu yetu Tundu Lisu, aliyepo kitandani, si kwa mapenzi yako bali kwa mapenzi ya ibilisi.

Bwana wetu ulituambia, 'gongeni mtafunguliwa', tunagonga kwenye nyumba ya mamlaka yako ili mkono wako wenye nguvu ukamguse na kumnyanyua ndugu yetu Tundu Lisu.

Ni mapenzi yetu, ndugu yetu arejee katika hali yake lakini kwa mapenzi yako katika haya mateso anayoyapitia, unaweza kumvusha, hata akatoka akawa bora zaidi kama ilivyokuwa kwa Ayubu. Mapenzi yako yatimizwe, sasa na hata milele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
barafu

Katika nchi inayofuata sheria, Ndugai alitakiwa kufungwa jela baada ya kumshambulia mtu kwa bakora katika kampeni.

Hakufaa kuwa hata mbunge,licha ya Spika. Alitakiwa kuwa jela.

Ila hapo Tanzania, chama kama CCM hakijui scandal ni nini, mtu kama Ndugai aliyetakiwa kwenda jela, sio tu kapewa nafasi kugombea ubunge,kapewa Uspika pia.

Mimi sishangai akiwa mzushi mzushi, mjivuni jivuni, limbukeni limbukeni, na muongo muongo.Vitendo vyake vya nyuma havinipi shaka kwamba anaweza kuwa hivi.
 
Nakumbuka Ndugai alivyotoka India, Mbowe alienda kumsalimia kabla ya viongozi wengine wa Ccm kwenda kumsalimia.
Utu ni kitu cha thamani sana, tatizo ulevi wa madaraka ndio unafanya watu wengine waonekane kama sio binadamu na hawafai kuishi.
Mungu ni mwema ndio maana mpaka sasa TL yuko hai na iko siku atasimama na kutaja jinsi Mwenyenzi Mungu alivyomuokoa kwenye dimbwi ka mauti.
 
Bahati nzuri tu ni kwamba Mungu anajitofautisha na mwanadamu katika masafa ya kufikiri na kutenda. Mara zote yeye anaanzia sisi tunapoishia. Vinginevyo tungeweza kuongea mangine kabisa muda huu.Kwa jinsi watu walivyomuombea Ndugai kwa sauti na ukimya halafu baada ya kupona eti amerudia jeuri zake nina imani Mungu angekuwa mwanadamu angefuta uponyaji aliomufanyia.

Kuna watu wanadharau sana Facility ya kuungama dhambi kwa Mamlaka ya Kanisa lakini Yesu alipoweka nafasi yeye kama hiyo alijua mambo kama haya ya akina Ndugai.Ndugai yangetokea.Alijua akili kama za akina Ndugai zipo duniani. Huyu Ndugai angekuwa ni mtu anatambua na anao uelewa mpana juu ya Sakramenti ya Upatanisho lazima angeenda kuungama hiyo dhambi. Bahati mbaya sana dhambi zake "anaungamia" kwenye kiti chake cha uspika.

Ndugai, uzima ulevya na ugonjwa ulegeza. Huna madaraka ya kutambia wenzio isipokuwa kama usilingalipewa na huyo akaaye Juu. Usingalivaa mavazi ya Kifalme kama Spika kama Yeye aliye mwanzo na mwisho Wa Ufalme asingalikupatia ufalme huo.
 
Malumbano wanaoanzisha ni chadema wenyewe..wakijibiwa wanaona wanaonewa..ndugai alielezea taifa wingi wa risasi alizopigwa lisu kwenye gari..kubenea akasema ndugai muongo..wakati kitendo tu cha kutaja wingi kule wa risasi ilibidi mumpongeze..maana angeweza pia kukaa kimya..kamsema zito bungeni..zito akagusia lisu..wakati lisu hausiki..Lema nae anamshutumu kuhusu lissu..
Sasa vitu mnaanzisha wenyewe..mkijibiwa mnasema malumbano..basi kaeni kimya uguzeni mgonjwa wenu..ila msidhani shughuli zitasimama kwa sababu ya ugonjwa au kifo cha lisu..hata vikao vya Acacia na timu ya magufuli havijasimama
Sheiza, kama unaakili timamu utafuta huu uchafu uliouweka hapa na kumuomba radhi kila aliyeusoma! Tanzania ni ya watanzania na sio kikundi kidogo unachokishabikia, Ndugai na wote wanaodhani wanahati miliki ya uhai wanajidanganya. Hata hao waliopanga na kutekeleza shambulio dhidi ya Lisu dhamila zitawatesa mpaka wafe! Hawata kaa waonje raha na amani mioyoni mwao milele. Wewe unayeshangilia hapa kwa ujinga wako hutakaa ulione hilo kwani hawatakuambia mateso wanayo yapata.
 
Malumbano wanaoanzisha ni chadema wenyewe..wakijibiwa wanaona wanaonewa..ndugai alielezea taifa wingi wa risasi alizopigwa lisu kwenye gari..kubenea akasema ndugai muongo..wakati kitendo tu cha kutaja wingi kule wa risasi ilibidi mumpongeze..maana angeweza pia kukaa kimya..kamsema zito bungeni..zito akagusia lisu..wakati lisu hausiki..Lema nae anamshutumu kuhusu lissu..
Sasa vitu mnaanzisha wenyewe..mkijibiwa mnasema malumbano..basi kaeni kimya uguzeni mgonjwa wenu..ila msidhani shughuli zitasimama kwa sababu ya ugonjwa au kifo cha lisu..hata vikao vya Acacia na timu ya magufuli havijasimama

Ndiyo maana ya uhuru wa kutoa maoni...

Angalia na soma tena na tena ulichokiandika, uone ambavyo huna tofauti na Job Ndugai na Spika wa bunge....

Lakini unaheshimiwa na tunaheshimu maoni yako....

Asante kwa kuja, na karibu tena wakati mwingine kutoa maoni yako...!!
 
Malumbano wanaoanzisha ni chadema wenyewe..wakijibiwa wanaona wanaonewa..ndugai alielezea taifa wingi wa risasi alizopigwa lisu kwenye gari..kubenea akasema ndugai muongo..wakati kitendo tu cha kutaja wingi kule wa risasi ilibidi mumpongeze..maana angeweza pia kukaa kimya..kamsema zito bungeni..zito akagusia lisu..wakati lisu hausiki..Lema nae anamshutumu kuhusu lissu..
Sasa vitu mnaanzisha wenyewe..mkijibiwa mnasema malumbano..basi kaeni kimya uguzeni mgonjwa wenu..ila msidhani shughuli zitasimama kwa sababu ya ugonjwa au kifo cha lisu..hata vikao vya Acacia na timu ya magufuli havijasimama
J shonza hand writing, hongera naona kwa sasa una ulinzi kama DAB
 
Back
Top Bottom