Mzee Mwafrika
JF-Expert Member
- Sep 25, 2007
- 203
- 99
.
nakupa pole sana mzee mwafroka.
nani kakudanganya hapa kuna watu wanaweza kujadili falsafa? hapa watu wanataka mambo ya kwenye mikeka ya vibarazzani. we anzisha hapa thread ya mambo ya "wapwa", "tusker baridi" na "mabikira" uone jeshi la wachangiaji litakavyofumuka.
juzi nguli alianzisha thread ambayo haikuwa na content bali kichwa cha habari tu kisemacho"eti mtu wa kwanza kufanya ngono na mwanamke ana access siku zote hata kama mwamnamke yule kaolewa" alikusanya uwanja mzima wa wana JF na sijui amepewa thanks ngapi?
haya ndo wana JF wanataka. sana sana ukitoka nje kidogo, ujadili mambo ya zito.
hiyo metafizikia uliyogusia hapo juu unadhani wangapi wanaweza hata kukuambia ni mnyama gani????
hakuna great thinkers hapa!!!!!!!!!
mkuu nimekubali!
unajua mi nimeishawaelewa hawa wanaochangia hapa JF. kuna wengine wameishajuana na wanachangiana kuungana mkono hata kwa mambo ya kipuuzi kabisa. kuna wengine wanatoka kwenye kujadili suala la msingi wanaanza kuchati masuala yao binafsi nje ya mada, hivyo wanwachanganya watu makini wanaofuatilia hoja inavyojadiliwa.
Mimi binafsi napenda sana mambo yanayojenga na kuimarisha maarifa, ningependa sana kufuatilia mjadala wa thread yako mpaka mwisho. Mimi binafsi sijajikita sana katika falsafa, lakini ninaweza kubaini mtazamo Fulani unafuata falsafa gani. hivyo utaona kama tungekuwa na great thinkers wa kweli, sie wengine tungefaidika sana kwa kufuatilia michango hapa jamvini
inasikitisha sana
revolution inahitajika nchini, hasa hasa kuhusu swala la elimu. hapa nipo naandika proposal ya kuja TZ kuhamasisha public understanding of Science and the world around them,. kaeni chonjo wadau wa TBC
Mzee Mwafrika,
Umeshamsoma Bertrand Russell katika "The Problems of Philosophy"?
http://www.ditext.com/russell/russell.html
inabidi watu kuhamasishwa kwanza in masses, kabla ya kuanza kufanya sayansi ya maana yenye kuleta innovation ktk biomedicine, environmental microbiology, biotech etc. huwezi fanya sayansi TZ bila kuwa na personell wa kutosha na wenye motisha. Vijana wengi wenye vipaji wameenda kusoma Accounting, Finance, na Journalism huku kozi za sayansi na uhandisi haziko kwenye "fashen"
Bado mkuu ila nimeshafuatilia kidogo baadhi ya kazi zake na hasa maisha yake!yah one of the best katika karne iliyopita!nitachimba zaidi na nitarudi hapa tena.Nilikuwa napitia Arguments of God's existance katika mitandao mbali mbali,mtu wangu kuna watu wamezaliwa kufikiri na kama ufikiri basi umekufa!
Hii miradi yenu ya kuhamasisha wananchi kwa kutafuna hela za wafadhili wa miradi ndiyo inayoilostisha nchi hii. Hivi Newton, Archimedes, Einstein na wengineo walisubiri fedha za wafadhili wa kuwahamasisha? Science happens when it is done and not just spoken about. Kama unataka sayansi njoo uifanye!
Asante Mzee Mwafrika, tangu ulipojoin JF mwaka 2007Falsafa ni nini?
Falsafa ni mapenzi ya hekima:ni safari ya kuitafuta hekima.Karibuni sana akina Bruley,mwanakijijji,companero na wengine wote tupikane
Mimi nimejikita hasa kwenye Metafizikia maana napenda kujua zaidi masuala kuhusu imani na uwepo wa Mungu.karibuni wote!!
Mbona hizi hata hapa tumezichambua sana.Ulipata wasaa wa kuzipitia?
Mfano mmoja tu huu hapa chini
https://www.jamiiforums.com/habari-...hy-i-am-not-a-christian-bertrand-russell.html
Asante Mzee Mwafrika, tangu ulipojoin JF mwaka 2007
Na hiyo idadi ya posti zako, ndio unakuja leo kuwakaribisha kina Mzee Mwakijiji, Blueray, Campanero
Na wengineo kuja kujadili falsafa?.
Kweli nondo zote zinazopita JF huzioni, au kwa vile sio za metafizia, hakuona mambo ya freemasons humu!. Hukuona mambo ya Yoga humu?. Hukuona mambo ya Psychic humu?. Mind of Matter?. Life After life?. Metafizikia gani unayotafuta wewe?.
Somo zuri sana! hili linafanya watu wapende kutafakari mambo nakuwa wabunifu! Japokuwa hii post ni ya muda mrefu takribani miaka 10 sasa lakini bado inamashiko makubwa sana kwa vijana kusoma na kuielewaFalsafa ni nini?
Ni vigumu sana kupata maana halisi ya neno "falsafa".Falsafa sio wazo:falsafa sio maono:falsafa sio njia ya kufikiri:falsafa ni tofauti ya hivi vyote.
Falsafa ni mapenzi ya hekima:ni safari ya kuitafuta hekima.Katika safari hii yakupasa kutafakari kila kitu na kuvijaribu kupitia mazungumzo na majibizano(discussion):Falsafa haitaki uwakili wa kile unachokiamini bali utetezi wa kweli.
Yawezekana umeianza hii safari pasipo kufahamu:Umeshawahi kujiuliza haya maswali(au yafanayo na haya)?
kama ndio basi kuna uwezekano umeshaianza safari hii!
- Je kuna uwepo wa Mungu?nini maana ya maisha?-dini
- Kuna uwezekano wa kusimama kwa muda?-sayansi
- Je demokrasia ni mfumo mzuri wa kuendesha serikali?-Siasa
- sheria zipi zafaa kuongoza jamii fulani? n.k
Hii ni thread maalumu kwa wanafalsafa wachanga;wakongwe na wale wenye wapenzi ya hekima kujifunza na kupeana mawazo mapya pamoja na kubadilishana nondoz zinazohusiana na falsafa.Karibuni sana akina Bruley,mwanakijijji,companero na wengine wote tupikane.
Mimi nimejikita hasa kwenye Metafizikia maana napenda kujua zaidi masuala kuhusu imani na uwepo wa Mungu.karibuni wote!!