Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Akitoa neno la ufunguzi wa majadiliano hayo, Naibu Katibu Mtendaji wa SADC anayeshughulikia ushirikiano wa Kikanda, Bi. Angeles N'Tumba alisema kikao hicho ambacho ni cha kwanza kufanyika, kitajadili miongozo ambayo SADC na Marekani wataitumia katika ushirikiano wao ambao umelenga maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na amani na usalama, afya, uchumi na usimamizi wa rasilimali kama vile nishati na madini.
Ameongoza kuwa Marekani ipo tayari kushirikiana na SADC kutatua changamoto zinazoikabili kanda hiyo hususan zile zinazorejesha nyuma utekelezaji wa miradi ya maendeleo na amani na usalama.
Inaelezwa kuwa jukwaa hilo la majadiliano ni kielelezo cha dhamira ya dhati na ya pamoja kati ya SADC na Marekani katika kukuza na kuimarisha ushirikiano endelevu, mtangamano wa kikanda na kuibua fursa za kiuchumi kwa manufaa ya pande zote.