Sadaka ya ajabu kuliko zote

Sadaka ya ajabu kuliko zote

Tumefika mahari ulimwengu usio onekana ( spiritual world ) uheshimiwe na utumiwe sana maana huo ndiyo utatufanya tuyumbe ktk maisha haya au la,ila kupanga ni kuchagua.
 
SADAKA YA AJABU KULIKO ZOTE:-
(Unatakiwa kuitoa hata kama kanisa lako hawaifundishi ama kuisisitiza).

Kuna sadaka inaitwa Fungu la kumi (Zaka/Tithe) ambayo unatakiwa kutoa asilimia 10 ya mapato yako yote. Sadaka hii umaajabu wake uko hapa:- usipoitoa kwa HIARI itakutoka kwa LAZIMA.

KIMSINGI....

Hii sadaka unapoitoa inafanya kazi kubwa mbili:-

1). Inalinda na kuhifadhi usalama wa mambo yako yote:- (biashara yako, afya yako, ndoa yako, watoto wako, afya za wanaokutegemea, akiba zako, fedha zako, usalama wa mali zako, ajira yako, mshahara wako n.k)

2). Inafungua madirisha ya baraka:- (yaani unakuwa na ideas nyingi useful, unakuwa na uwezo wa kubuni na kutekeleza, unakuwa na nguvu ya pekee kufanya kazi, unakuwa na maono, unakuwa na kibali kwa kila ulifanyalo, unakuwa na spidi kubwa kimaendeleo, n.k). [MALAKI 3:8-12]

CHA AJABU....

Kwa kuwa kazi ya sadaka hii ni kukulinda, usipoitoa kwa hiari tena kiukamilifu, maana yake ni kwamba ule ulinzi unakuwa haupo. Ndio utashangaa umeuchuna kutoa hilo fungu la kumi let say elfu themanini (katika laki nane unayolipwa), halafu unapigiwa simu kwamba mzazi anaumwa kijijini na unakwenda kutumia laki mbili!

Ama ndio ile unagoma kutoa fungu la kumi then unashangaa kila mshahara ukitoka ama kila ukishika fedha, matatizo yanaongozana msururu, kufumba na kufumbua unakuta hela zimeisha bila hata kujielewa elewa! Kama una tatizo katika ndoa yako, kabla hujaomba ama kuombewa hebu kagua ikiwa unatoaga fungu la kumi kiuaminifu.

Huwezi kuacha kutoa fungu la kumi kwa uaminifu halafu uchumi wako ukabaki salama. Huwezi ukaacha kutoa fungu ka kumi halafu uwe na garantii ya kwamba ndoa yako itakuwa ni, "heat free marriage", "stress free marriage", ama "Haeaven on Earth" marriage. Haiwezekani!

Na kama huwa hutoi fungu la kumi na unadhani kuwa uko salama, huenda hujajua kwamba kutotoa kwako ndio kunasababisha mambo yako yawe magumu kifedha ama yawe yanaenda kwa jasho jingi sana. Kama unatoa fungu la kumi kiuaminifu hutakiwi kuwemo katika orodha ya wanaopambana na joto la fedha kuwa ngumu mtaani. Nakuona unajitetea moyoni kutokana na kutotoa kwako. Pleaseee hebu jaribu kuitoa hii sadaka kwa uaminifu ujionee inavyothibitisha kile anachosema Mungu kuhusu sadaka hii.

HALAFU...

Huo unaoufanya ni utoto ujue! Yaani Mungu anakupa milioni moja unakuwa mchoyo kumpa laki moja?!!?!!? Hivi unajua kwamba Mungu hafanyagi madili makubwa/ya maana na watoto? Unajichelewesha na kujiangamiza ujue?

Hakuna maombi wala matamko ya kinabii yatakayokufanikisha kiuchumi, kindoa, kiuzazi, kikazi ikiwa hautoi fungu la kumi kwa bidii, kwa furaha na uaminifu. Hata kama unatafuta mtoto, mume, ajira (n.k) unapoendelea na maombi ama kuombewa tafadhali zingatia sana fungu la kumi. Sadaka zote unazotoa zinaanza kuwa na maana ukishakuwa umemalizana na Mungu katika kipengele cha fungu la kumi.

Na kama hutoagi fungu la kumi wala hata usijichoshe kumuomba Mungu kwamba akubariki kiuchumi. Tena uelewe kwamba suala sio kiwango, suala ni moyo. Kama unaona ni ngumu kutoa fungu la kumi katika laki moja unayopata sasa, usifikiri ukishika milioni utaweza kutoa, kinachokuzuia sasa na laki moja ndicho kitakuzuia mbeleni na milioni kumi.

USISAHAU...

Mimi sikuelezi habari nilizozisoma ama kujifunza tu, hapana! Ninakueleza uzoefu halisia kutoka katika maisha yangu. Ninarekodi ya majanga na misala iliyonipata kwa kupuuza fungu la kumi ama kutotoa kwa uaminifu na ninazifahamu baraka za kuzingatia fungu la kumi kwa uaminifu. Nilishaweka agano na Mungu ya kwamba sitakaa nicheze na habari ya fungu la kumi, maana kibano chake sio cha hapa! Kama unabisha, shauri yako, endelea kuhanya hanya hivo hivo!

[HASHTAG]#SmartMind[/HASHTAG]
Sadaka toa mwenyewe kwa kuamua mwenyewe kwa jambo unalolipenda mwenyewe.

Kamaunapenda pombe, kuwanywesha rafiki zako pombe kwa kuwa moyo wakounafurahi ni sadaka kubwa kulikokusaidia masikini halafu roho yakoikasononeka.

Hayo mambo mengine ya asilimia kumi Mungu kasemani uongo tu, Mungu huyo hayupo.

Angekuwepo angechapa noti zake mwenyewe asihitaji sadaka ya mtu.
 
SADAKA YA AJABU KULIKO ZOTE:-
(Unatakiwa kuitoa hata kama kanisa lako hawaifundishi ama kuisisitiza).

Kuna sadaka inaitwa Fungu la kumi (Zaka/Tithe) ambayo unatakiwa kutoa asilimia 10 ya mapato yako yote. Sadaka hii umaajabu wake uko hapa:- usipoitoa kwa HIARI itakutoka kwa LAZIMA.

KIMSINGI....

Hii sadaka unapoitoa inafanya kazi kubwa mbili:-

1). Inalinda na kuhifadhi usalama wa mambo yako yote:- (biashara yako, afya yako, ndoa yako, watoto wako, afya za wanaokutegemea, akiba zako, fedha zako, usalama wa mali zako, ajira yako, mshahara wako n.k)

2). Inafungua madirisha ya baraka:- (yaani unakuwa na ideas nyingi useful, unakuwa na uwezo wa kubuni na kutekeleza, unakuwa na nguvu ya pekee kufanya kazi, unakuwa na maono, unakuwa na kibali kwa kila ulifanyalo, unakuwa na spidi kubwa kimaendeleo, n.k). [MALAKI 3:8-12]

CHA AJABU....

Kwa kuwa kazi ya sadaka hii ni kukulinda, usipoitoa kwa hiari tena kiukamilifu, maana yake ni kwamba ule ulinzi unakuwa haupo. Ndio utashangaa umeuchuna kutoa hilo fungu la kumi let say elfu themanini (katika laki nane unayolipwa), halafu unapigiwa simu kwamba mzazi anaumwa kijijini na unakwenda kutumia laki mbili!

Ama ndio ile unagoma kutoa fungu la kumi then unashangaa kila mshahara ukitoka ama kila ukishika fedha, matatizo yanaongozana msururu, kufumba na kufumbua unakuta hela zimeisha bila hata kujielewa elewa! Kama una tatizo katika ndoa yako, kabla hujaomba ama kuombewa hebu kagua ikiwa unatoaga fungu la kumi kiuaminifu.

Huwezi kuacha kutoa fungu la kumi kwa uaminifu halafu uchumi wako ukabaki salama. Huwezi ukaacha kutoa fungu ka kumi halafu uwe na garantii ya kwamba ndoa yako itakuwa ni, "heat free marriage", "stress free marriage", ama "Haeaven on Earth" marriage. Haiwezekani!

Na kama huwa hutoi fungu la kumi na unadhani kuwa uko salama, huenda hujajua kwamba kutotoa kwako ndio kunasababisha mambo yako yawe magumu kifedha ama yawe yanaenda kwa jasho jingi sana. Kama unatoa fungu la kumi kiuaminifu hutakiwi kuwemo katika orodha ya wanaopambana na joto la fedha kuwa ngumu mtaani. Nakuona unajitetea moyoni kutokana na kutotoa kwako. Pleaseee hebu jaribu kuitoa hii sadaka kwa uaminifu ujionee inavyothibitisha kile anachosema Mungu kuhusu sadaka hii.

HALAFU...

Huo unaoufanya ni utoto ujue! Yaani Mungu anakupa milioni moja unakuwa mchoyo kumpa laki moja?!!?!!? Hivi unajua kwamba Mungu hafanyagi madili makubwa/ya maana na watoto? Unajichelewesha na kujiangamiza ujue?

Hakuna maombi wala matamko ya kinabii yatakayokufanikisha kiuchumi, kindoa, kiuzazi, kikazi ikiwa hautoi fungu la kumi kwa bidii, kwa furaha na uaminifu. Hata kama unatafuta mtoto, mume, ajira (n.k) unapoendelea na maombi ama kuombewa tafadhali zingatia sana fungu la kumi. Sadaka zote unazotoa zinaanza kuwa na maana ukishakuwa umemalizana na Mungu katika kipengele cha fungu la kumi.

Na kama hutoagi fungu la kumi wala hata usijichoshe kumuomba Mungu kwamba akubariki kiuchumi. Tena uelewe kwamba suala sio kiwango, suala ni moyo. Kama unaona ni ngumu kutoa fungu la kumi katika laki moja unayopata sasa, usifikiri ukishika milioni utaweza kutoa, kinachokuzuia sasa na laki moja ndicho kitakuzuia mbeleni na milioni kumi.

USISAHAU...

Mimi sikuelezi habari nilizozisoma ama kujifunza tu, hapana! Ninakueleza uzoefu halisia kutoka katika maisha yangu. Ninarekodi ya majanga na misala iliyonipata kwa kupuuza fungu la kumi ama kutotoa kwa uaminifu na ninazifahamu baraka za kuzingatia fungu la kumi kwa uaminifu. Nilishaweka agano na Mungu ya kwamba sitakaa nicheze na habari ya fungu la kumi, maana kibano chake sio cha hapa! Kama unabisha, shauri yako, endelea kuhanya hanya hivo hivo!

[HASHTAG]#SmartMind[/HASHTAG]
MAkanisA waliyoleta wazungu yamewafanya mmekuwa wajinga
 
Ni kweli KABISA ila siyo kila penye msaraba unapeleka sadaka hutafanikiwa kwa kiwango kilicho kusudiwa na MUNGU BABA,soma kumbukumbu 12:5 na kumbukumbu 18:18-26
Tumia Agano Jipya kushawishi utoaji zaka.

Pia Mtoa mada. Maana wengi wanatumia Agano la kale ila tukiwaambia nguruwe haramu wanakimbilia agano jipya.
 
In short kama hutoi fungu la kumi huendi mbinguni, mbingu ni kwaajili ya watakatifu na sio kwaajili ya wezi soma Malaki 3:8-12.mbingu ni kwaajili ya wanaolitii neno la Mungu
Justify kwa kutumia agano Jipya.
 
Inaonekana "biashara" inakwenda mrama.
Nasikia na misamaha ya kodi kwa taasisi za dini imepunguzwa.
Nadhani hii no mbinu mbadala ya kupiga pesa za waumini.
Wanasiasa nao hawachangii mpaka itakapofika 2019
 
Ni kama unanunua ulinzi wako
Yaani unalipwa kwa KK security au makampuni mengine ya ulinzi.
Unataka utuaminishe kuwa nipe nikupe and virse versa
Sijaelewa hapa umeandika nini.
 
tatizo hilo fungu la kumi linaenda kuliwa na wengine....
Sadaka haikupasi ufikilie nani anakula iyo pesa wewe toa kwa moyo wote...nahatakama anakula si ndio kamba yake ina mruhusu..kama atakula bila mapenzi ya Mungu laana haita muacha salama
 
in a masonic world we call it rituals. kuna siri nyingi sana za ulimwengu ambazo si kila mtu anazijua, na ikitokea ukajua baadhi tu ya siri hizi unaweza kufanya mambo mengi na ya aajabu sana kwani unakuwa unafahamu principles za ulimwengu.

kati ya principle muhimu sana ni pamoja na kafara/sadaka. na in a masonic world kafara/ sadaka ni kati ya rituals zinazozingatiwa kwa umakini zaidi. fumbo la sadaka/kafara si jambo geni hata kwenye vitabu vya dini. na unaweza kuona katika kitabu cha mwanzo ambapo Cain na abel walitoa sadaka za mazao na mifugo.

kafara ili iwe na mafanikio lazma ikuume, na kafara kubwa zaidi ni ile ya damu hasa ya mtu wako wa karibu. tunaona katika biblia, Ibrahim alijaribisa imani kwa kuombwa kumtoa kafara mwanae wa pekee Isaka, au kwa wakristu, Mungu alitoa kafara ya damu ya mwanae Yesu kristu ili kushinda vita dhidi ya dhambi.

hizi zote hazitokei kama coincidence, bali kuna siri nzito ya ulimwengu iliyo nyuma ya kafara. dini zetu zimedodosa taratibu chache katika maswala ya kafara, na imerahisisha zaidi hata utaratibu wa kutoa kafara hizi kwa kuzipa thamani ya pesa. hivi sasa hutatakiwa kumtoa mwanao, ila utatoa pesa itakayokuuma kiasi. ....
 
Kutoa fungi la kumi ni sawa,, lakini tatizo ni huko zinakoenda,, ya ani mi nitoe fungu la kumi halafu"nabii" apeleke guest,, never ever
Sio lazima umpelekee yeye, ipeleke kwa watoto yatima au wajane au wagonjwa wasiojiweza Mungu atakubariki sana.
 
Nakubaliana nawewe mtoa Mada

Hilo ni la kweli kabisa.
 
Back
Top Bottom