We Know Next
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 814
- 380
Huko nyuma nilisha wahi kusema, siku ambayo watanzania walalahoi watakapoamua kuingia barabarani, sijui watawala hawa watakimbilia wapi kujificha. Sasa wakati umefika, na wakati wenyewe ni leo Jumatatu tarehe 30/1/2012. Siku ambayo Serikali iliyochaguliwa na Wananchi wake wenyewe, imewageuka na kuamua kufanya mauaji ya halaiki kwa kuwanyima huduma muhimu ya afya.
Nafahamu, Madaktari leo hawawezi kurudi kazini, na nafahamu Manesi na wahudumu wengine wa afya kuanzia kesho watoa matamko yanayofanana na hili la Madaktari, Madaktari Bingwa nao, muda si mrefu watatoa tamko linalofanana na hili la madaktari, na kitakachofuata hapo ni kilio na kusaga meno. Kwa sababu watakao athirika ni watanzania wote wa kawaida bila kujali itikadi zao au kazi zao, tutasikia na chama cha waongoza ndege nao wanagoma, Dawasco nao watagoma, Tanesco nao watagoma, kwasababu hakuna atakayepona kwa hili.
Kwa vile Madaktari wameonyesha njia, tuwaunge mkono watanzania wote wenye mapenzi na nchi hii, na kupigana na serikali dharimu. Hatuna silaha, kama wao walivyo na majeshi, lakini umoja wetu ni silaha tosha. Napendekeza kwa kupitia kamati maalum ya madaktari, wafungue account huru, ambayo sisi wapenda mabadiliko tutawachangia na pesa hizo zitawasaidia kujikimu ktk kipindi hiki kigumu. Tunafahamu hawa wenzetu wana familia na ndugu wanaowahusu na kuwategemea. na kwavile vita hii si ya kwao peke yao, hatuna budi kusaidia kwa hali na mali kuendeleza mapambano. Nina uhakika watu wengi watajitoa kuchangia account hiyo ya Madaktari, na wao wakipata pesa hizo watajua namna ya kuzigawanya. Shime MaDoctor wa ukweli, Shime JF na Watanzani wapenda mabadiliko, muda wa kulalamika umeisha, tufanye kwa vitendo. Dr. Ulimboka, tuwekee hiyo account details leo hii hii, au kama kuna njia nyingine ya mbadala tujuze. Tupo pamoja.
Nafahamu, Madaktari leo hawawezi kurudi kazini, na nafahamu Manesi na wahudumu wengine wa afya kuanzia kesho watoa matamko yanayofanana na hili la Madaktari, Madaktari Bingwa nao, muda si mrefu watatoa tamko linalofanana na hili la madaktari, na kitakachofuata hapo ni kilio na kusaga meno. Kwa sababu watakao athirika ni watanzania wote wa kawaida bila kujali itikadi zao au kazi zao, tutasikia na chama cha waongoza ndege nao wanagoma, Dawasco nao watagoma, Tanesco nao watagoma, kwasababu hakuna atakayepona kwa hili.
Kwa vile Madaktari wameonyesha njia, tuwaunge mkono watanzania wote wenye mapenzi na nchi hii, na kupigana na serikali dharimu. Hatuna silaha, kama wao walivyo na majeshi, lakini umoja wetu ni silaha tosha. Napendekeza kwa kupitia kamati maalum ya madaktari, wafungue account huru, ambayo sisi wapenda mabadiliko tutawachangia na pesa hizo zitawasaidia kujikimu ktk kipindi hiki kigumu. Tunafahamu hawa wenzetu wana familia na ndugu wanaowahusu na kuwategemea. na kwavile vita hii si ya kwao peke yao, hatuna budi kusaidia kwa hali na mali kuendeleza mapambano. Nina uhakika watu wengi watajitoa kuchangia account hiyo ya Madaktari, na wao wakipata pesa hizo watajua namna ya kuzigawanya. Shime MaDoctor wa ukweli, Shime JF na Watanzani wapenda mabadiliko, muda wa kulalamika umeisha, tufanye kwa vitendo. Dr. Ulimboka, tuwekee hiyo account details leo hii hii, au kama kuna njia nyingine ya mbadala tujuze. Tupo pamoja.