Saa chache kabla mtu hajafa

Wakulonga

JF-Expert Member
Oct 29, 2012
762
772
Kwa mujibu wa uislam mtu anapokaribia kufariki huonyeshwa matendo yote alofanya katika maisha yake. Kisha huonyeshwa mafikio yake eidha motoni au peponi. Sasa wanasayansi wa leo wame prove hilo

Je,wajua kinachopita akilini mwako unapokaribia kufa?-Utafiti​

Saa 7 zilizopita
Picha ya ubongo

CHANZO CHA PICHA, FRONTIERS IN AGING NEUROSCIENCE

Data mpya kutoka kwenye "ajali" ya kisayansi imependekeza kwamba wakati unapoaga dunia ,maisha yanaweza kujirejelea machoni mwako.

Timu ya wanasayansi ilipanga kupima mawimbi ya ubongo ya mgonjwa mwenye umri wa miaka 87 ambaye alikuwa na kifafa. Lakini wakati wa kurekodi mfumo wa neva, alipata mshtuko mbaya wa moyo - akitoa rekodi isiyotarajiwa ya ubongo unaokufa.

Ilifichua kuwa katika sekunde 30 kabla na baada, mawimbi ya ubongo ya mwanaume huyo yalifuata mifumo ile ile ya kuota au kukumbuka kumbukumbu.

Shughuli za ubongo za aina hii zinaweza kuonesha kwamba "kumbukumbu ya maisha" ya mwisho inaweza kutokea katika dakika za mwisho za mtu, timu iliandika katika utafiti wao, uliochapishwa katika jarida la Frontiers in Aging Neuroscience mnamo Jumanne.

Picha ya ubongo

CHANZO CHA PICHA, FRONTIERS IN AGING NEUROSCIENCE

Dk Ajmal Zemmar, mwandishi mwenza wa utafiti huo, alisema kwamba kile timu, wakati huo iliyokuwa Vancouver, Canada, ilipata kwa bahati mbaya, ilikuwa rekodi ya kwanza kabisa ya ubongo unaokufa.

Aliiambia BBC: "Hii ilikuwa bahati tu, hatukupanga kufanya jaribio hili au kurekodi ishara hizi."

Kwa hivyo tutapata taswira ya wakati tukiwa na wapendwa wetu na kumbukumbu nyingine zenye furaha? Dk Zemmar alisema haiwezekani kuelezea.

"Kama ingekuwa ulimwengu wa kifalsafa, ningebashiri kwamba ikiwa ubongo ungetoa kumbukumbu, pengine ungependa kukukumbusha mambo mazuri, badala ya mambo mabaya," alisema.

"Lakini nini cha kukumbukwa kitakuwa tofauti kwa kila mtu."

Dk Zemmar, ambaye sasa ni daktari bingwa wa upasuaji wa mishipa ya fahamu katika Chuo Kikuu cha Louisville, alisema katika sekunde 30 kabla ya moyo wa mgonjwa kuacha kutoa damu kwenye ubongo, mawimbi ya ubongo wake yalifuata mifumo ile ile tunapofanya kazi zenye uhitaji wa juu wa utambuzi, kama vile kuzingatia, kuota au kuzingatia. kukumbuka kumbukumbu.

Iliendelea sekunde 30 baada ya moyo wa mgonjwa kuacha kupiga - hatua ambayo mgonjwa hutangazwa kuwa amekufa.

"Huu unaweza kuwa ukumbusho wa mwisho wa kumbukumbu ambazo tumepitia maishani, na hujirudia kupitia ubongo wetu katika sekunde za mwisho kabla hatujafa."

Utafiti huo pia unaibua maswali kuhusu ni lini hasa, maisha yanaisha - wakati moyo unapoacha kupiga, au ubongo unapoacha kufanya kazi.

Dk Zemmar na timu yake wametahadharisha kuwa hitimisho pana haliwezi kupatikana kutokana na utafiti mmoja. Ukweli kwamba mgonjwa alikuwa na kifafa, akiwa na damu na ubongo uliovimba, hufanya mambo kuwa magumu zaidi.

"Sikuwahi kujisikia vizuri kuripoti kesi moja," Dk Zemmar alisema. Na kwa miaka kadhaa baada ya kurekodiwa kwa mara ya kwanza mnamo 2016, alitafuta kesi kama hizo kusaidia kuimarisha uchanganuzi lakini hakufanikiwa.

Kitanda cha hospitali

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Lakini utafiti wa 2013 - uliofanywa kwa panya wenye afya nzuri - unaweza kutoa fununu.

Katika uchambuzi huo, watafiti wa Marekani waliripoti viwango vya juu vya mawimbi ya ubongo wakati wa kifo hadi sekunde 30 baada ya mioyo ya panya kuacha kupiga - sawa na matokeo yaliyopatikana kwa mgonjwa wa kifafa wa Dk Zemmar.

Kufanana kati ya tafiti ni kwa "kushangaza," Dk Zemmar alisema.

Sasa wanatumai kuchapishwa kwa kisa hiki kimoja cha kibinadamu kunaweza kufungua mlango kwa masomo mengine katika dakika za mwisho za maisha.

"Nadhani kuna jambo la ajabu na la kiroho kuhusu tukio hili la karibu kufa," Dk Zemmar alisema. "Na matokeo kama haya - ni wakati ambao wanasayansi wanaishi."
 
Jambo la msingi kwa muono wangu jaribu kuishi kwa Upendo na kula bata na familiya yako yaani Mke,Mme, watoto na watu wenye uhitaji wa kweli,au kama wewe siyo muumini wa ndoa jipende mwenyewe napendelea kusaidia watu wenye uhitaji wa kweli ..hii itakuwa kumbukumbu bora zaidi katika maisha yako.

Nimejaribu kuongea na wazee wengi mara nyingi hujutia maisha ambayo waliyatumia vibaya kwa kufanya starehe mbalimbali na kuziacha familiya zao solemba.Mara nyingi huwa wanaondoka na majuto hayo kwani kunakuwa hakuna room ya waho kufanya masahihisho.
Tujitahidi kuishi na kujali familiya zetu kwa viwangu vyetu.

Ishi duniani kwa upendo wa kweli ni njia pekee ya kutokuogopa kifo.

ACHA CHUKI - ACHA CHUKU - LET LOVE LEAD .
 
Back
Top Bottom