Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Ukipata chungu kipya usitupe cha zamani, Tanzania hatukuchagua kwa Mungu atupe banadari tumezaliwa tunakuta nature ina provide vitu vyote kwetu, hata kama Rwanda na Uganda watapitisha mizigo yao Kenya still Tanzania itaendelea kuwepo hata kama tutapata shida kwa muda flani kwani mapato yatapungua. Lakini ukweli unabaki pale pale kuwa kuna siku watatuhitaji bila ya wao kupenda kwa sababu kabla ya kufika Rwanda kupitia kutokea Kenya lazima upite Kenya ikiwa siku moja Rwanda watakua na mahusiano mabaya na Uganda hivyo nchi hiyo isiruhusu bidhaa za Rwanda kupita Uganda hapo moto utawaka, itawabidi watume ndege na uwe3zo huo hawana na watapiga magoti tena kututaka tupitishe mizigo yao kwetu tena. Sometimes one can not go against nature, utaumia sana, ni matumaini yangu watarudi tu tena kwa aibu kubwa sana ni muda tu ngoja tusubiri cinema hii tuone itaisha kwa style gani. Mungu ibariki Tanzania.
 
the 3ks wanayo road map yao ambayo ndani ya miezi nane impact itaonekana kwa kudorora kwa uchumi wa nchi.walimshadadia kenyatta wakati wa uchaguzi wakidhani wakuwa upande wao.
Ni hivi kenyata ni mjasilia mali anajua wapi pa kuwekeza at the right time, the guy knows sabotage strategies in business na ndicho yule dogo katufanyia leo tunalia na kagame, no ni yule dogo, mfaidikaji wa mgogoro huu ni kenya via mombasa port.mtalaumu kagame buuuuuuuuuuuuuuuuuureeeeeee!!! Think outside the box, just open the pandora box.kenya ni wafanya biashara wanajua mikakati ya kibiashara.

Wa-tz mmeingia kingi kwa mgogoro wa rwanda, no kenya behind the panorama

watz mmesahau waliotufanyia kenya jumuia ya afrika mashariki iliyokufa????jk umesahau kweli??????????????TULIONYA MAPEMA KUANZISHWA UPYA KWA JUMUIA YA AFRIKA MASHARIKI.TUNAANZA KUONA PICHA SASA.TULISEMA HAWA MAJIRANI WANA AGENDA ZAO ZA SIRI.
 
Madini kila kona, ziwa bahari maji kila kona, ardhi kubwa yeny rutuba, gas na makaa ya mawe ya kutosha. Kweli vijimzigo hivyo ndo vitasababisha mtetemeko wa uchumi,afterall mapato ya bandari kwa 90% yanaishia mikononi mwa mafisadi. Hapo hakuna kuteteleka kokote.

Viongozi wakisema tumetosha kufisadi ngoja tupige kazi ndani ya miaka miwili maendeleo yanapaa kama drones hata kama bandari tukiifunga ikapitisha mizigo zero.
 
acheni ubishi wa kitoto nyie for national's sake
 
Tatzo hujui ukweli kuhusu mizan..tatzo la mizan za bongo..znatofautiana.ukpima kibaha unambiwa iwepungua tone 3 ukifka moRO wanasema imezid 2 ukienda kihonda hapo hapo moro unambiwa ipo sawa..dodoma imezd...sasa jiulize hzo mizan znafanya vp kaz...watu ni rushwa njia nzma..na mwenye gari hakubali kulipa analipa mwenye mzgo.. so utaona wana haki ya kulalamika..istoshe.. tone znazo ruhuswa uganda. Zambia na Rwanda. Kenya ukija bongo unambia umezidsha mzani....inachosha
 
US offers $5m bounty for FDLR’s Mudacumura





The US government has offered US$5 million for information leading to the arrest, transfer and conviction of Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR) supreme commander, Sylvestre Mudacumura.
US Ambassador-at-Large for Global Criminal Justice Stephen J. Rapp announced this on Thursday during a tele-press conference.
Mudacumura is wanted by the International Criminal Court (ICC) on charges of crimes against humanity and war crimes, including murder, rape, torture and attacking civilians.
He is the overall commander of the FDLR, a DRC-based militia group largely blamed for the 1994 Genocide against the Tutsi.
Mudacumura’s name was added on the list of the most wanted fugitives, which also features several key architects of the Genocide, including Felicien Kabuga, Protais Mpiranya and Augustin Bizimana.
Uganda’s warlord Joseph Kony, leader of the notorious Lord’s Resistance Army (LRA), is also on the list.


Any more questions?

Nashukuru kwa hiyo taarifa.......Mkuu hakuna anayepinga unyama uliofanywa na baadhi ya watu kule Rwanda na wengine waliokimbia nje ya Rwanda.........na ndio maana kuna ICC....hii imetuathiri sana hata sisi Watanzania......kuna mahakama kule Arusha.........nilitoa mfano kuhusu Charles Taylor ambaye aliua thousands and thousands......where is he now?

Hamuwezi kupata amani kwa vita vya visasi........kwa sababu with time mtakuwa mna-run into matukio ya visasi kujirudia........

.....The point is an individual kutakiwa at a a price hakuondoi umuhimu wa mazungumzo ya kutafuta suluhu na hatimaye amani........Joseph Kony anaweza kuwa anatafutwa kwa gharama yeyote.......lakini Museveni yupo tayari kuzungumza....Sudan mambo yalikuwa hivyo hivyo .....Garrang alikuwa terrorist mbele ya Bashir....What is happening now? Bashir anatakiwa ICC!!......Angola mambo yalikuwa hivyo hivyo...Savimbi & Co. , Liberia Charles Taylor, Sierra Leon Foday Sankoh, Ivory Cost etc etc....kote huko kulikuwa na mazungumzo.......i.e. waasi Vs serikali

Muache Ku-support M23....na muache propaganda za kijinga....eti hamuwezi kuzungumza na waasi.....na msitake kuleta chokochoko hapa Tanzania na mkifikiri you are smart than us.......the reality of the matter ni Watanzania hatuna Ugomvi na Wanyarwanda.......isipokuwa mis-conception na tafsiri zisizo kutoka kwa viongozi wenu ambazo zinataka/zinatishia kuondoa mahusiano mazuri yaliyopo miongoni mwetu............na viongozi wa aina hiyo ni hatari.......

Rwanda mna sheria zenu, Kenya za kwao, Uganda za kwao, Burundi, DRC na Tanzania pia.......wahamiaji haramu ni tatizo la dunia ila linatofautiana kulingana na opportunities one country can attract.......kosa nikosa hata ka lilikuwa na miaka 50 bado nikosa......Tanzania tumewahi kuwa hadi na watu ndani ya serikali yetu sehemu nyeti na hata sasa tunao ambao baadhi yao baada ya kujulikana tuliwapa muda warekebishe makaratasi yao vinginevyo waondoke........
 
Leo nimegundua watz wengi ikitokea ghafla mtu kafukuzwa kazi basi anazimia au anapigwa stroke.Akili zetu ni kama zimefungwa vile ni kweli utendaji wa bandari yetu ni hovyo lakini kujitoa kwa hao watu hakumaanishi ndo mwisho wa sisi kuishi.maisha lazima yaendelee.Na tunavyo huzunika tunawapa hao watu credit kwamba tunawategemea sana ili uchumi wetu uende.Ni lazima tutumie akili zetu kujiletea maendeleo wenyewe sio mtu wa nje akizila basi Watz hamna maendeleo tuna lose soverignity hata kwa hizi nchi
 
Nina wasiwasi na kigezo cha rushwa sababu tafiti za hivi karibuni kenya wanaongoza kwa rushwa then Uganda afu sisi mi kwetu kuna udhaifu na mambo ya kijinga mengi.Kwa bahati mbaya ni Watanzania wachache wanao pata fursa za kuishi nchi hizi za jirani wengi wanaenda safari na kurudi ila ukienda huko Serikali zao zina madudu pengine hata yetu ni nafuu.Tumeichoka tu nchi yetu ila hamna nchi salama EAC tunazidiana viwango tu.suala la rushwa hatujawafikia wakenya jamani tuwe wakweli
 
Hatuwezi ku loose sovereignity yetu kijinga hivi eti vikwazo barabarani mizani mingi.Sasa kama kila mtu anayekuja na kutaka tufate yake kisa tunafanya nae biashara si utakuwa utumwa huu.Hivi wewe unaweza kukubali bosi wako akuingilie maisha yako binafsi na kukupangia taratibu anazotaka wewe uzifuate katika maisha ya binafsi tofauti na ofisi na wewe ufuate eti kisa anakupa mshahara.yaani tunataka kuyumbishwa hata na nchi zilizo sawa na sisi kiuchumu wazungu watutese na hawa tena tusijirahishe kiasi hiki
 
Ile ilikuwa fix ya M7 ili muingie kuminane za EAC za kuingiza ardhi kwenye jumuia.

Kifupi kenya kuna rushwa balaa hiyo ya bongo cha mtoto, nashangaa wachangiaji wanatoa data wapi? Kenya mhhh, Kenya huwezi chukua taxi pale airport kama huwajui, kenya huwezi tembea, Bora traffic wa bongo anakuomba rushwa, wa kenya anakutia ndani ukizubaa anakutwanga na risasi.
Ndugu mi nashangaa watu wanavyozani sisi tumekubuhu kwa rushwa hizo serikali ziko corrupt tz ina nafuu kiasi
 
UFAFANUZI KUHUSIANA NA MAKUBALIANO YA RWANDA, KENYA NA UGANDA KUFANYA MOMBASA KUWA KITUO CHA USHURU.

Utangulizi:

Marais wa nchi za Rwanda, Uganda na Kenya, walikutana mwanzoni mwa mwezi uliopita, ambapo mojawapo ya maazimio ya mkutano wao, ilikuwa ni kufanya Mombasa kuwa kituo cha kukusanya ushuru, na hivyo Uganda na Rwanda waanze kusafirisha mizigo yao moja kwa moja kutoka Mombasa. (Angalia ambatisho)

Ufafanuzi:

Chama cha Umoja wa Wasafirishaji wa Malori nchini (TATOA), kinaamini hatua hiyo itadhoofisha uchumi wa nchi yetu kwa kiasi kikubwa sana.

Na kama serikali yetu ikipuuzia kujiondoa kwa wateja hawa wawili, Rwanda na Uganda, huenda nchi nyingine zaidi zikazidi kujiondoa kutumia bandari ya Dar es Salaam.

TATOA inaamini maamuzi kama haya ya nchi za wenzetu ya kurahisisha taratibu za ulipaji ushuru pamoja na kuboresha utaratibu wa bandari ni muhimu kwa bandari yetu pia.

Ripoti ya Benki ya Dunia (WB) ilidhihirisha namna ambavyo bandari ya Dar es Salaam, ufanisi ukiboreshwa, inaweza ikawa mkombozi mkubwa wa uchumi wetu.

Faida za bandari hii kwa uchumi ni mtambuka, kwa hiyo TATOA haitapenda kuona mteja yoyote akijitoa kutumia bandari yetu, au kupungua kwa biashara kwa namna yoyote ile, na hivyo itapigania kwa kuishauri serikali katika kuboresha bandari yetu.

TATOA ni mmoja wa wadau muhimu kwenye sekta hii ya bandari, kwani biashara yake ni kusafirisha mizigo inayofika bandari ya Dar es Salaam kuwafikishia walengwa, hasa nchi zisizo na bandari (land locked countries) kama Congo, Zambia, Rwanda, Malawi,Uganda, Zimbabwe na Burundi.

Hivyo kuondoka au kupungua kwa namna yoyote ile kwa matumizi ya bandari yetu, ni hofu ya TATOA itaathiri uchumi kwa kiasi kikubwa.

Ieleweke kwamba, sekta ya usafirishaji wa malori ni muhimu kwa uchumi wetu. Sekta hii inatoa zaidi ya ajira milioni moja (1) za moja kwa moja, na nyingine zaidi ya milioni tatu (3) zisizo za moja kwa moja.

Sekta ya usafiirishaji wa malori pia, ni yapili kwenye uchangiaji wa pato la taifa (GDP).

Sekta hii pia, ni mojawapo ya sekta chache nchini ambazo zinagusa nyanja tofauti za kiuchumi kama, huduma za simu za kutuma pesa, matairi, spea pamoja na mafuta, ambazo zote zinafaidika na sekta hii.

Mabenki pia yamekuwa ni mojawapo ya taasisi zinazofaidika na sekta ya usafirishaji, ukiangalia kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo, huduma inayoongoza kwenye mabenki ni Vehicle Asset Financing.

Zaidi ya hayo, TATOA pia inachangia kwa kiasi kikubwa kwenye mfuko wa barabara, ambao ndio unatumika kuboresha barabara zetu nchini, kupitia matumizi ya mafuta, ambapo malori pekee yanatumia ziadi ya lita milioni mbili na laki tisa kwa siku kati ya lita milioni tatu na nusu.

Mwisho TATOA inaamini, uboreshaji wa reli ni muhimu kwa maendeleo ya sekta ya usafirishaji nchini, kwani miundo mbinu hii miwili, reli na barabara, inafanya kazi kwa pamoja.

Wakati reli inaweza kufikisha mzigo mpaka stesheni, malori yatahitajika kufikisha mzigo sokoni, au mahala pengine mteja atakapohitaji.

Mifano hai ni nchi ya Uingereza na Afrika Kusini, ambazo zina malori mengi pamoja na kuwa zina mfumo mzuri wa reli.

Lakini kwa nchi yetu, ambayo sekta ya reli bado inaboreshwa, tunaamini malori yataendelea kuwa na umuhimu mkubwa.

TATOA inaiomba serikali, kupitia wizara ya uchukuzi kufanyia kazi kero zilizopo katika bandari ya Dar es Salaam lakini pia kufanyia kazi mapendekezo yanayotolewa na wadau wa sekta ya usafirishaji.






​
 

Attachments

Say what you say lakini this is the disaster kwa uchumi wa TZ,politics lazima ziwekwe pembeni kwenye hili swala,bandari ya TZ inaingiza mapato mengi sana treasury na trucking business ambayo inachangia sana uchumi wa Taifa inategemea bandari ya Dar,something must be done sio kulaumu tuu ni visa vya Rwanda au plan ya Uhuru na M7,hapa ni biashara mbele sio politics tena,na wafanyabiashara wanaangalia maslahi wakipata deal nzuri Dar watarudi wote kutumia hiyo bandari
 
Ndugu mi nashangaa watu wanavyozani sisi tumekubuhu kwa rushwa hizo serikali ziko corrupt tz ina nafuu kiasi
Acha kutafuta mchawi,improve bandari na ondoa kero zote wanazolalamikia hao wasafirishaji then utaona wote wanarudi kuitumia hiyo bandari,wafanyabiashara wanaangalia profit kwanza sio siasa
 
Nimesikia baadhi ya vyombo vya habari vikisema eti ni hujuma! Come on! Tumerogwa?!

Siyo hujuma wala kurogwa. Kama ni kurogwa basi tunajiroga wenyewe. Tanzania hatuna customer care kwa wateja wetu. ndio maana Katupiga chini na soon atatutandika na bandari atachukua kiulainiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Chezea Banyamulenge wewe....
 
Kwani bandari ya tz inawafaidisha watanzania wangapi? Pia mizigo ya rwanda inayopitia tz ni ya bilioni ngapi? Bandari ya tz kitambo inaliwa na mafisadi. Kwa hyo kama walishndwa kuisimamia mpaka watu wakachoka watulie waangalie sekta zingine. Serikali itapata fundisho na itakua serious kusimamia masuala ya mapato. Watajiju mafisadi wanaofaidi bandarini.

Kazi tunayo hasa sie walalahoi...Hivi mwajua kuwa ikiwa serikali haitakusanya mapato wa kuumia ni mimi na wewe...Kifupi ni kwamba tutajziwa hadi kodi za haja kubwa na ndogo kama ilivyo sasa...Mafisadi wakosa fungu la kufisadi walazimisha kupata kutoka chanzo kingine nacho ni mwananchi masikini... Rais hawezi kosa suti kisa bandari makusanyo yamepungua na vile anapenda kwenda ughaibuni so lazima hela ipatikane kwa kila namna... Ni aibu na ni ngumu kuamini kama tunaweza adhirika kiasi hicho... Kweli, tuna kila kitu lakini hakuna wa kujigusa japo kidogo tu kuonyesha kuwa tunauwezo na hili ama lile...Ni kipi sisi tuanweza chenye kujivunia cha maendeleo?
 
Back
Top Bottom