mathcom
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,396
- 519
Hao majirani walishaamua kutugawa tu tangia Kikwete atoe tamko la kukomesha mauaji yanayofanywa na M23 wakiongozwa na Rwanda na Uganda. Hayo mambo mengine wanashingizia tu, hata tungeliwaruhusu wapitishe hayo mafuta bure basi wasingepitisha!! Wameamua kututenga wakijua kwamba tutayumba kiuchumi, hilo wala lisitutishe jambo la kwanza ni kujitoa katika jumuiya yao ya kipuuzi (EAC), kuhimizana uzalendo na kuanza kupigania upya maendeleo ya uchumi wetu! Vyanzo vya mapato ni vingi mno, tunatakiwa kuwa wazalendo wa kweli kweli sasa kupigania nchi yetu na kuikomboa kutokana na hawa wakoloni waafrica! Kama wao wanatembeleana kwa kutumia ID sisi tutaanzisha mfumo wa VISA ambao kila atakaeingia nchini mwetu kutokea hayo mataifa matatu (RUK) alipie VISA!