Rwanda - Tanzania Tensions Flare Again

Status
Not open for further replies.

Rwanda haijawahi kuwa biggest trading partner na haiji kuwa sababu ni ka nchi kadogo kenye population ndogo na uwezo mdogo wa wanunuzi.Rwanda kwa Tanzania muda mwingi amekuwa biggest problems partner.

Kupungua kwa wafanyabiashara wa Rwanda kutumia bandari ya Dar Kunaeleweka.Biashara ya kupitishia silaha za Rwanda za kupigia kongo imepigwa stop DAR PORT na upitishiaji madini yaliyoporwa kongo na wanyarwanda kupitia bandari ya Dar kumepigwa stop.Na majeshi ya Tanzania yako kule kongo kuhakikisha silaha haziingii zipitie mombasa au wapi na madini hayatoki.Hii imesababisha malori ya wanyarwanda yawe matupu hayana cha kubeba kupeleka bandari ya Dar wala cha kupeleka Rwanda kama walivyozoea.

Machache yaliyobaki ni ya mafuta na vitu vidogovidogo.
 
For no good reasons, but I feel it is high time Kagame and his team are removed from leadership....they have failed and must be out now..
Again, for no "good reasons"
 
mkuu hiyo sahau nilisoma article moja kwenye net ni kwamba wapiganaji wa fdlr na wale wa jeshi la congo huwa wanashirikiana hata kwenye vita si unajua tena the enemy of your enemy is your friend!!!!

Kiongozi ni kweli kabisa. Unajua DRC jeshi lake ni genge la wahuni wabakaji na waporaji, hakuna discipline kabisa. Hata silaha za majeshi ya UN wamepewa FDLR. Hushangai kwa nini majeshi ya UN yamesitisha mandate yake ya kuondoa majeshi ya "waasi" baada ya M23? Kuna vikundi zaidi ya 17 Eastern Congo lakini UN wanapotezea. Nia ya UN ni kuivamia Rwanda through their proxy - FDLR. They "allegedly" arm those rebels na ndio maana wanapata kiburi cha kuzunguka kujitapa kwa kuwa wanajua wana msaada mkubwa wa UN na France.
 
Mkuu, NasDaz, you said it very well.. You opened many's eyes that, "Kagame is afraid of FDRL becoming a Political Party"! That is nothing but a truth. Be blessed..
 
Haaa aaaahhh...kelele tuu mbona,waambie walianzishe tuu,anyway acheni kujidanganya na story zenu za kishabiki,war btn TZ and Rwanda will never happen period! Vita sio lelemama mjomba


Mkuu si story za kujidanganya, hapa JF kuna wengi tu hawampendi JK, but when it comes to Tanzania utashangaa. Huko Rwanda Kagame ni kama mungu. lakini hapa Tanzania JK ni rais tu, pamoja na hayo kumkejeli Rais wetu ni kutukejeli sisi.
Tanzania inajua vita si ushabiki, kwani tumewahi kupigana vita na si mara moja, wala mara mbili na si mara tatu. Tunajua vita si lele mama, karibu na kwenu huko kuna kaka zetu wamelala sehemu moja inaitwa Kaboya, kwa hiyo tunajua sana vita si lele mama, hasa baada ya vita kuvuruga uchumi wetu. But when it comes to us, we will not flatter.


For some reasons Kigali imeamua kuwa Tanzania si rafiki, si jirani na si ndugu. My meaning of Kigali here is, PK and Co, na sio wanyarwanda au watutsi. Ili tuwe wakweli ni lazima tuseme wazi kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda una mtikisiko, vitendo vya Kigali na kauli zao zinaonesha wazi kabisa kuwa Tanzania inatakiwa ku-act, otherwise PK and Co, wataendelea kusumbua Tanzania. How to do so, that is up for discussion.

Unajua kambare akishaota sharubu anajiona gege, lakini inawezekana kuwa sharubu sio ukubwa. Tanzania na watanzania hawajawahi kutegemea hata siku moja kuwa Rwanda itakuwa na tabia kama ya leo, ya dharau, kejeli, matusi na vitisho. Kwa mtu mwenye akili timamu hili jambo ni la kuliangalia kwa undani wake na kwa muktadha wa muda mrefu.

Hata siku moja Tanzania haijawahi kuamuliwa nani aje na nani asije, hata Marekani yenyewe haikuwahi kufanya hivyo. Leo kuwaalika watu wawili watatu kutoka Rwanda inakuwa tatizo, eti kisa Kigali anataka wasikaribishwe.....that is a pack of BS.

Ni tabia gani ya kusema adui yako ni adui yangu, ina maana wakati Habyarima alipokuwa madarakani tungesema watutsi hawatakiwa kuja Tanzania? Au kwa kuwa Kagame alikuwa mpinzani tungesema hatakiwi kuja Tanzania? au kwa kuwa RPF ilikuwa kundi la uasi lenye lengo la kupindua nchi tungesema halitakiwi Tanzania?

Unajua PK na bahati mbaya sana wengine ambao wanapenda kujiaidentify kuwa watutsi wanatoa lugha chafu sana, zinazwafanya baadhi ya watu hapa Tanzania waanze "kuwaelewa" machinjachinja. This is extremely dangerous, sick and bad. Kama kweli tuna nia ya kupambana na mchinjachinja, tusioneshe tabia zao.

When you exhibit exteremly ideologies, you are no different to an extremist. There is no where written that extreme genocidal ideologies and mentalities are restricted to Interhamwe. We now hear, see and smell extreme and genocidal (suicidal) tendencies in Kigali...in similar proportions to those we heard in 1992, 1993 and 1994 from Colonel Bagosora and Co. The worst part of all is that, the current Kigali tone is well playing into the interhamwe's core ideology, and have some believe that Bagosora's were right. This is very very dangerous.

Yule msh..nzi aliyesupervise genocide Rwanda alikuwa anasema haya haya ambayo baadhi ya watu humu (sorry to say...wanaojiita watutsi) wanafanya. Badala ya kuelemisha watu kuchangia kwa akili wanakuja na kejeli, matusi as if Tanzania ni kundi la wajinga, kama serikali ya Rwanda inavyofikiri. Ni hatari sana, ni bora watanzania tendelee kuwa neutral, kuhumiza wazungume kwa kuheshimiana, licha ya matauusi na kejeli zao. In the end kama likilipuka la kulipuka hatuwezi kufunga mipaka

Inasikitisha sana kuona baadhi ya member wenzetu kutoka Rwanda wanakamatika kirahisi sana kwenye mchezo wa interhamwe.
 
Acha ujinga wako, mbona siraha zilizotumika kuipindua serikali ya Habyarimana zilipita bandari hii hii ya Dar sasa iweje za FDLR zisipite Tanzania kwenda kuipndua serikali ya Kagame.Wacha double standard kijana
 
He is number one enemy of Tutsi, that can be understood!...Unless otherwise when you say kigali u mean tutsis. Hivi do you think mkiacha kutumia bandari ya Dar es Salaam sisi tutaumia kwa lipi? Nyie ndio maisha yatawawia magumu kwa sababu kwa kanuni ndogo za kuichumi lazima bidhaa zipande bei kwa mlaji wa mwisho kwani kutumia bandari ya mombasa it is obvious that, gharama zitakuwa kubwa. Nyie jirekebisheni, acheni tabia zenu za uhutu na ututsi na kujiona nyie watutsi ni bora zaidi ya watu wengine wote; haya yote hayatakuwepo. Kwa hiyo tofauti zenu za kubaguana kusikokuwa na msingi hakutufanyi sisi Watanzania tuingie kwenye huo UPUMBAVU wenu.
 
mkuu hiyo sahau nilisoma article moja kwenye net ni kwamba wapiganaji wa fdlr na wale wa jeshi la congo huwa wanashirikiana hata kwenye vita si unajua tena the enemy of your enemy is your friend!!!!

hivyo vita ambavyo fdlr na congo wanashirikiana huwa wanapigana na .....
 
Kachaguliwa na watutsi wenzake sio wanyarwanda......
 

Lakini Rwanda si mwenyekiti wa security council ya UN hiyo hiyo, inajivamia yenyewe au?
 

kama ambavyo UN haikushambulia RPA wakati kagame alikuwa anaua wanyarwanda kwa miaka minne, ndivyo hivyo hivyo ambavyo haiwezi kuishambulia FDLR ambayo ndio ilikuwa serikali! Elewa kuwa FDLR kumpindua kagame sio mapinduzi kivile actually ni kurudi madarakani tu. kagame hakutakiwa kuwapo pale ni accident of history tu.
 
Kachaguliwa na watutsi wenzake sio wanyarwanda......

Rushasha mkuu naomba nitofautiane na wewe hapa. Rais Kagame alishinda kwa kishindo kwa kuwa anakubalika na sehemu kubwa (majority) ya wanyarwanda. Tutsis make up a mere 15% of the population. Lazima ukubali kuwa aliungwa mkono na wanyarwanda bila kuangalia "ukabila".
 
I am happy that sometimes you can talk sensible things. This is good; ila sasa nyie ndio muache mambo yanu maovu yanayosababisha hizi "chuki" zitokee!
 

jMali you cant be serious chief. FAR walikosa uhalali wa kuwa sehemu ya serikali pale walipomuua Rais Habyarimana na kuendesha mauaji ya kimbari ya 1994. Haybarimana's was an oppressive regime on ethnic lines. Tutsis were second class citizens and faced persecution daily. Had it not been for RPF's moral certitude, that genocide would have claimed a lot more innocent civilians. I also find it hilarious that you think just because Rwanda is ceremonially chairing the UN Security Council then somehow the country has any real say on what goes on in the organization, ha ha ha. Ni hivi mkuu, UN inawasaidia FDLR ili wamtoe Rais Kagame, hili halina ubishi. Hujajibu swali; ni lini UN itatekeleza mandate yake ya kupigana na waasi wa FDLR?
 

Kiongozi katika mambo ambaya Mwalimu alichemsha ni kuvunja uhusiano wa ki-balozi na taifa la Israel. Hili taifa lilikuwa na msaada mkubwa sana kwa nchi yetu hasa katika nyanja za kilimo cha umwagiliaji, ujenzi, afya na jeshi. Kila nikipita Mlalakuwa JKT nakumbuka msaada wa Israel katika kuanzisha na kutrain National Service. In fact hata sare za JKT ni zile zile za IDF. Nikuulize, ni nini tulichofaidikia kama nchi na taifa kwa kuwaunga mkono wapalestina? Ni hao hao waarabu on the dusty streets of Ramallah, Gaza, Hebron etc tuliowaona wakishangilia kwa furaha pale balozi za America zilipopigwa na mabomu mwaka 1998 na mamia ya waKenya na waTanzania kupoteza maisha. Walichofurahishwa nacho ni nini hasa? Wakati huo huo IDF walituma wataalam wa uokozi, matibabu na hata kupeleka watu Israel for treatment. Huu ni mfano mmoja tu. Ili Tanzania ibarikiwe ni lazima irudishe uhusiano kamili na taifa la Israel.
 
Acha ujinga wako, mbona siraha zilizotumika kuipindua serikali ya Habyarimana zilipita bandari hii hii ya Dar sasa iweje za FDLR zisipite Tanzania kwenda kuipndua serikali ya Kagame.Wacha double standard kijana

Genocidaire mnanichekesha sana mnaposhindwa kutumia busara na kujibu hoja bila ya kutumia lugha za kejeli. Anyway, ni hivi si kweli kuwa silaha za RPA zilipitia Dar bali zilitoka Uganda. Rais Museveni kwa wingi wa fadhila zake kwa makamanda wa RPF waliomsaidia kuung'oa utawala dhalimu Uganda na kwa kutambua ulazima wa kusitisha mauaji ya halaiki ya watu wasio na hatia nchini Rwanda chini ya Rais Habyarimana na genge lake la wauaji, aliamua kuwapa silaha RPA. Wakati huo baadhi ya watanzania wakiwauzia silaha FAR na magenge mengine ya wahuni DRC na Burundi. Unafikiri silaha walizokuwa wanatumia CNDD-FDD na wengine walipata wapi? Unawajua arms brokers wakubwa Tanzania ni nani? Kama hujui tulia.
 

Mkuu mimi ni Mtanzania lakini nakubaliana na nyinyi katika hii mada,Tatizo letu Watanzania tumelishwa simulizi za uongo na Watawala wetu kwa muda mrefu mno.Hili suala kupelekwa kwa baadhi ya militias huko DRC linaeleweka kuna baadhi ya Watanzania wanahusika na hii biashara ni kweli.
 

Weka takwimu hapa.Idadi ya wanyarwanda wote jumla ni kiasi gani (Rwanda population).Halafu lete takwimu inayoonyesha waliojiandikisha kupiga kura walikuwa wangapi? Na mwisho onyesha waliompigia kura walikuwa wangapi.
Kushinda kwa kishindo kunaweza kuwa kwa waliojiandikisha na kupiga kura wa kabila lake hasa.Sehemu kubwa ya population ukakuta ilisusa haikujiandisha kwa hasira na haikwenda kupiga kura.

Ushindi pia unatakiwa kufanyiwa analyisis.Kwa maeneo n.k.Kusema tu mtu kashinda kwa kishindo haitoshi.
 

You are spot on Mkuu,We need diplomatic relations with Israeli back!!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…