Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Katibu wa Baraza la Wadhamini la CHADEMA Anthony Komu amesema usitishwaji wa Ruzuku kwa vyama vya siasa utakiathiri chama hicho kwa kiwango kikubwa.
Kiongozi huyo mwenye mamlaka ya kifedha ndani ya CHADEMA amesema chama hicho kinategemea asilimia 45% ya Ruzuku ya kila mwezi kulipa mishahara ya wafanyakazi na watendaji wa chama kote nchini.
Komu amesema ingawa wana vyanzo vingine vya mapato lakini havitoshi bila kutegemea Ruzuku.
Komu amesema pia usitishwaji huo wa Ruzuku utaathiri kwa kiwango kikubwa mipango ya chama hasa uimarishwaji wake katika operesheni zinazoendekea kote nchini.
Kiongozi huyo amelaani uamuzi wa Kibabe wa Kamati ya bunge kuzuia Ruzuku kwa vyama vyote huku CHADEMA wakiwa hawana kosa lolote na wakiwa wameshakabidhi mahesabu yao ofisi ya msajili wa vyama siku nyingi.
Source:Mwananchi.
Kiongozi huyo mwenye mamlaka ya kifedha ndani ya CHADEMA amesema chama hicho kinategemea asilimia 45% ya Ruzuku ya kila mwezi kulipa mishahara ya wafanyakazi na watendaji wa chama kote nchini.
Komu amesema ingawa wana vyanzo vingine vya mapato lakini havitoshi bila kutegemea Ruzuku.
Komu amesema pia usitishwaji huo wa Ruzuku utaathiri kwa kiwango kikubwa mipango ya chama hasa uimarishwaji wake katika operesheni zinazoendekea kote nchini.
Kiongozi huyo amelaani uamuzi wa Kibabe wa Kamati ya bunge kuzuia Ruzuku kwa vyama vyote huku CHADEMA wakiwa hawana kosa lolote na wakiwa wameshakabidhi mahesabu yao ofisi ya msajili wa vyama siku nyingi.
Source:Mwananchi.