Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
“HAKUNA Mwanaume amewahi kulalamika rushwa ya ngono,” amesema Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Stella Mafuru.
Amesema kesi zote zinazohusu rushwa ya ngono, zinatolewa na wanawake, lakini hakuna mwanaume yeyote ambaye amewahi kuripoti rushwa hiyo ya ngono ambayo kwa sasa imeingia kwenye kipengele pendwa cha uhujumu uchumi. Anasema: “Wanaume mjitokeze kama mnatengenezewa mazingira ya ngono na wanawake vunjeni ukimya”.
Kupitia marekebisho ya Sheria Namba 3 ya mwaka 2016 Sheria ya Uhujumu Uchumi ilifanyiwa mabadiliko na kutambua makosa yote yaliyopo ndani ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa isipokuwa kosa chini ya kifungu cha 15 ni makosa ya uhujumu uchumi.
Hivyo rushwa ya ngono kwa sasa ni kosa la uhujumu uchumi na adhabu yake sio faini tena ila ni kifungo cha miaka mpaka 20.
Stella amesema kwa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007 imetamka kosa hili chini ya kifungu cha 25 ambapo kwa tafsiri isiyo rasmi kifungu hicho kinasema:
“Mtu yeyote ambaye kwa kutumia nafasi yake au mamlaka yake katika kutekeleza majukumu yake anadai au nalazimisha upendeleo wa kingono au upendeleo mwingine wowote kama kigezo cha kutoa ajira, kupandisha cheo, kutoa haki au upendeleo wowote unaotambulika kisheria atakuwa ametenda kosa.”
Kwa mujibu wa takwimu za Takukuru zilizotolewa mwanzoni mwa mwaka huu, jumla ya kesi 23 ziliripotiwa na vyuo vya elimu ya juu ndio vinaongozwa kwa rushwa ya ngono.
Amesema kesi zote zinazohusu rushwa ya ngono, zinatolewa na wanawake, lakini hakuna mwanaume yeyote ambaye amewahi kuripoti rushwa hiyo ya ngono ambayo kwa sasa imeingia kwenye kipengele pendwa cha uhujumu uchumi. Anasema: “Wanaume mjitokeze kama mnatengenezewa mazingira ya ngono na wanawake vunjeni ukimya”.
Kupitia marekebisho ya Sheria Namba 3 ya mwaka 2016 Sheria ya Uhujumu Uchumi ilifanyiwa mabadiliko na kutambua makosa yote yaliyopo ndani ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa isipokuwa kosa chini ya kifungu cha 15 ni makosa ya uhujumu uchumi.
Hivyo rushwa ya ngono kwa sasa ni kosa la uhujumu uchumi na adhabu yake sio faini tena ila ni kifungo cha miaka mpaka 20.
Stella amesema kwa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007 imetamka kosa hili chini ya kifungu cha 25 ambapo kwa tafsiri isiyo rasmi kifungu hicho kinasema:
“Mtu yeyote ambaye kwa kutumia nafasi yake au mamlaka yake katika kutekeleza majukumu yake anadai au nalazimisha upendeleo wa kingono au upendeleo mwingine wowote kama kigezo cha kutoa ajira, kupandisha cheo, kutoa haki au upendeleo wowote unaotambulika kisheria atakuwa ametenda kosa.”
Kwa mujibu wa takwimu za Takukuru zilizotolewa mwanzoni mwa mwaka huu, jumla ya kesi 23 ziliripotiwa na vyuo vya elimu ya juu ndio vinaongozwa kwa rushwa ya ngono.