Katibu Mkuu wa TUICO afikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Shauri la Uhujumu Uchumi namba 2015/2024- Jamhuri dhidi ya Bw. BONIFACE YOHANA NKAKATISI- Katibu Mkuu Taifa wa CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA VIWANDA, BIASHARA-TAASISI ZA FEDHA, HUDUMA NA USHAURI (TUICO) imefunguliwa leo Januari 31, 2024 mbele ya Mh. Bittony Mwakisu (SRM) katika Mahakama ya wilaya Ilala.

Mshtakiwa ameshtakiwa kwa kosa la Kutumia madaraka yake vibaya kinyume na kifungu cha 31 na kosa la Ubadhirifu na Ufujaji wa fedha kiasi cha Tshs.238,545, 044/= kinyume na kifungu cha 28(2) vyote vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 329 ikisomwa pamoja na Sheria ya Uhujumu Uchumi,Sura ya 200,R.E 2022.

Mshtakiwa amekana makosa yote na kupelekwa mahabusu baada ya kutokukidhi masharti ya dhamana.

Kesi imeahirishwa hadi tarehe 05.02.2024 kwa ajili ya kutajwa.
 
Chama chochote ambacho watu wanachanga pesa, sijui umoja wa nini nini, ni kitu cha watu wachache kupiga pesa. Hata serikali yenyewe ni chama fulani kikubwa na kodi zetu ndiyo michango.
 
Chama chochote ambacho watu wanachanga pesa, sijui umoja wa nini nini, ni kitu cha watu wachache kupiga pesa. Hata serikali yenyewe ni chama fulani kikubwa na kodi zetu ndiyo michango.
KIKUNDI KIDOGO CHA WATU NDANI YA ccm NI WEZI , WAPIGA PESA KAMA HUYU ALIVYOFANYA. CCM NI KIKINDI CHA AKINA MAWAZIRI AND SOME FEW OTHERS OF THEM
 
Hivi vyama vimekuwa ni sehemu ya upigaji na inaonekana vina pesa sana... Nimeanza kuelewa hata bwana maganga akagomea uteuzi wa mh Rais Ili kulinda kiti chake pale CWT
 
Shauri la Uhujumu Uchumi namba 2015/2024- Jamhuri dhidi ya Bw. BONIFACE YOHANA NKAKATISI- Katibu Mkuu Taifa wa CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA VIWANDA, BIASHARA-TAASISI ZA FEDHA, HUDUMA NA USHAURI (TUICO) imefunguliwa leo Januari 31, 2024 mbele ya Mh. Bittony Mwakisu (SRM) katika Mahakama ya wilaya Ilala.

Mshtakiwa ameshtakiwa kwa kosa la Kutumia madaraka yake vibaya kinyume na kifungu cha 31 na kosa la Ubadhirifu na Ufujaji wa fedha kiasi cha Tshs.238,545, 044/= kinyume na kifungu cha 28(2) vyote vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 329 ikisomwa pamoja na Sheria ya Uhujumu Uchumi,Sura ya 200,R.E 2022.

Mshtakiwa amekana makosa yote na kupelekwa mahabusu baada ya kutokukidhi masharti ya dhamana.

Kesi imeahirishwa hadi tarehe 05.02.2024 kwa ajili ya kutajwa.
Huyu bwana ni miongo mingi sana yumo kwenye shuhuri hizi za wafanyakazi!! Sasa inavyoonekana ataishia pabaya.
 
Hao viongozi wa TUICO kuanzia ngazi chini wote watu wa dili tuu.
 
Back
Top Bottom