asaprichie
JF-Expert Member
- Nov 29, 2014
- 292
- 227
Habari ya saizi Wakuu,
Leo nimeshuhudia njia mpya ya upokeaji rushwa kwa Trafki maeneo ya pale Goldstar ambapo ujenzi wa SGR unaendelea.
Wakati nimefika pale kituoni asubuhi ya saa 1 nikiwa nasubiri daladala za kwenda Gongo la Mboto nilikuta kituo kina raia mmoja tu ambae nae anaonekana sio mtu ambae anasubiri gari. Upande wa pili (kama mita 3 hivi) kulikuwa na trafiki anaongoza magari.
Sasa katika muda niliokaa pale nikawa nashangaa huyu jamaa ambae nimemkuta kituoni anapokea hela kwa kila daladala inayopita, yaani daladala zote zinazotokea Mnazi Mmoja lazima zipitie kituoni hapo halafu wanampa hela huyo jamaa kwa njia fulani hivi ya kisiri siri then daladala linaondoka.
Nikasema ebu ngoja nitulie kidogo nione kwanini wanampa hela. Baada ya muda nikaona anapokea simu, katika kuchunguza nikagundua kuwa alikuwa anaongea na Trafiki yule ambae yuko upande wa pili (nahisi hapa kuna ishara alimpa) maana gari iliyofuata haikutoa hela nikagundua kuwa trafiki yule anakula rushwa lakini mpokeaji ni huyo kijana aliyekuwa kituoni
Sent from my iPhone using JamiiForums
Leo nimeshuhudia njia mpya ya upokeaji rushwa kwa Trafki maeneo ya pale Goldstar ambapo ujenzi wa SGR unaendelea.
Wakati nimefika pale kituoni asubuhi ya saa 1 nikiwa nasubiri daladala za kwenda Gongo la Mboto nilikuta kituo kina raia mmoja tu ambae nae anaonekana sio mtu ambae anasubiri gari. Upande wa pili (kama mita 3 hivi) kulikuwa na trafiki anaongoza magari.
Sasa katika muda niliokaa pale nikawa nashangaa huyu jamaa ambae nimemkuta kituoni anapokea hela kwa kila daladala inayopita, yaani daladala zote zinazotokea Mnazi Mmoja lazima zipitie kituoni hapo halafu wanampa hela huyo jamaa kwa njia fulani hivi ya kisiri siri then daladala linaondoka.
Nikasema ebu ngoja nitulie kidogo nione kwanini wanampa hela. Baada ya muda nikaona anapokea simu, katika kuchunguza nikagundua kuwa alikuwa anaongea na Trafiki yule ambae yuko upande wa pili (nahisi hapa kuna ishara alimpa) maana gari iliyofuata haikutoa hela nikagundua kuwa trafiki yule anakula rushwa lakini mpokeaji ni huyo kijana aliyekuwa kituoni
Sent from my iPhone using JamiiForums